Thursday, March 8, 2012

MAISHA YA MASIKINI KILA SIKU

APRIL 18, 2012 , KATAVI MPANDA  

MAFUTA NI ISSUE??????????????

 MATATIZO YA UHABA WA MAFUTA BADO YANAENDELEA KATIKA MKOA WA KATAVI HAPA CHINI TUMEKUWEKEA PICHA ZILIZOPIGWA JANA KATIKA KITUO KIMOJA CHA MAFUTA KATIKA MAKAO MAKUU YA MKOA WA KATAVI MPANDA MJINI.










HAPA CHINI NI GARI LILILOKUWA LIKIELEKEA MISHAMO LIKIENDESHWA NA DEREVA AKIWA AMELEWA CHAKARI NA KUSABABISHA AJALI NYUMA YA UKUTA WA KANISA KATOLIKI MPANDA ENEO LA SHULE YA MSINGI MSAKILA JUZI MAJIRA YA SAA SITA MCHANA, MADEREVA WALEVI TUWAPIGE VITA 




mkurugenzi wa blog hii Wilbroard Sumia, anawapongeza wale wote walioingia katika bunge la Afrika Mashariki katika kipindi kijacho

    POSHO IMEISHA SAFARI BADO


DC MPANDA AWAFUNDA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI
 MKUU WA WILAYA YA MPANDA MKOA WA KATAVI, DR RAJABU RUTENGWE 
Na  Willy Sumia, Mpanda
SERIKALI wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi imewaagiza watendaji wa kata na vijiji kuwajibika katika maeneo yao ya kazi ili kuleta ufanisi katika utendaji wa kazi
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Mpanda, Dr Rajabu Rutengwe Machi 9, 2012 katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda wakati akifunga kikao cha ushauri cha wilaya ya Mpanda DCC
Mkuu huyo wa wilaya amesema hivi sasa watendaji wengi wamekuwa wakisubiria maagizo katika utendaji kazi wao bila kujali kuwa kutenda kazi zao bila maagizo ni nguzo ya utendaji kazi  wao
Amesema katika miji mingi wilayani Mpanda uchafu umeendelea kuchukua nafasi kubwa kuliko hali inayotakiwa kwani katika hali halisi hakuna haja ya kuwa na miji michafu wakati kila mji una watendaji wa serikali wanaotakiwa kuwajibika
Ametoa mfano wa mji wa Ikola kuwa kituo kikuu cha magonjwa wa kuhara na kutapika ugonjwa ambao kimsingi unasababishwa na uchafu hivyo endapo watendaji wataweza kuwajibika na kufanya kazi ipasavyo uchafu ungeondoka wenyewe hata hao wagonjwa wangeeleweka kuwa wametoka mbali
Ameziagiza serikali za vijiji na kata kuwajibika katika suala la mifugo iliyoingia kiholela katika maeneo yao kwani amesema kuwa taarifa za uhakika zinaelekeza kuwa upo ushahidi wa kutosha kuwa wapo baadhi ya watendaji wa kata na vijiji wamekuwa wakichukua pesa ili kuruhusu mifugo kuingia katika maeneo yao
“ ndugu zangu nawaeleza kitu kimoja kikubwa ni kuwa waliokula pesa watazitapika maana naagiza au ng’ombe waondoke wewe ubaki au wewe uondoke  ng’ombe wabaki, sina namna lazima uwajibike kwa ng’ombe uliowapokea” amesema mkuu wa wilaya
Kwa upande mwingine mkuu wa wilaya ameshukuru maafisa mipango wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda kwa kufanya vema katika maandalizi ya miradi ya maendeleo inayoleta mafanikio makubwa katika vijiji na kuweza kuondoa kero mbalimbali kwa wananchi wa wilaya yake
Mkuu wa wilaya ametoa taarifa katika kikao hiki kuwa kuanzia Machi 12, 2012 ataanza ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika kila kata ambapo ataweza kupokea taarifa za miradi, taarifa ya kazi, kukagua miradi na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara katika kila palipo na mradi wa maendeleo
Mada zilizojadiliwa katika kikao cha leo cha DCC ni pamoja na kupitia mpango na bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Mpanda ya mwaka 2012/2013, kupitia mpango wa bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Mlele kwa mwaka 2012/2013 pamoja na uzoefu wa nchi ya Japan katika ugatuaji wa madaraka.
mwisho
HAPA KAZI TU!!!! Mmoja wa madaktari akitoa huduma ya kinywa na meno kwa mwanafunzi wa shule ya msingi Msakila mjini Mpanda katika mkoa wa Katavi, Katavi ni miongoni mwa mikoa ambayo haijaguswa na mgomo wa madaktari uliotokea mwezi uliopita na mwezi huu.
MKOA WA KATAVI NA FURSA ZINAZOPATIKANA: MKUU WA WILAYA ATEMBELEA KATA ZA H/MJI - 

UNAMAONI GANI ?  tuandikie kwa email willysumia@gmail.com

BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA BAJETI YA BIL. 14
BARAZA la madiwani la halmashauri ya mji Mpanda katika mkoa wa Katavi limepitisha mapendekezo ya bajeti ya hamashauri hiyo kwa kipindi cha mwaka 2012/2013 kwa ajili  ya shughuli za maendeleo
Baraza hilo lilioketi leo Machi 9, 2012 limekubali kuyapitisha makadirio na makisio ya bajeti ya halmashauri hiyo ambapo mweka hazina wa Halmashauri hiyo Tatu Kisori amesema katika kipindi cha 2012/13 halmashauri imepanga kukusanya kiasi cha shilingi 606,847,000 kutoka katika vyanzo vya ndani ambapo pia halmashauri yake inatarajia kupokea ruzuku toka serikali kuu kiasi cha shilingi 6,441,517,240.
Amesema katika ruzuku ya serikali kiasi cha shilingi 5,338,014,240/= ni malipo ya mishahara kwa watumishi wa kada mbali mbali na shilingi 1,103,503,000/= ni za matumizi ya kawaida na kufafanua kuwa katika bajeti hiyo mishahara ni ongezeko la asilimia 20 kutoka shilingi 4,265,057,000/= hadi 5,338,014,240/=
Akizungumzia miradi ya maendeleo mweka hazina huyo alisema katika bajeti ya maendeleo halmashauri yake inatarajia kutumia shilingi 3,870,010,627/= kutoka serikali kuu, katika fedha hizo miradi ya maji imepewa kipaumbele kikubwa kwa kutengewa asilimia 34 ambayo ni shilingi 1,300,288,600/= ikifuatiwa na idara ya utawala kwa asilimia 26 sawa na shilingi 1,027,733,000/= pamoja na elimu ya sekondari iliyopewa shilingi 614,474,000/= sawa na asilimia 16.
Tatu Kisori pia amewasilisha bajeti ndogo ya maombi maalum ya nje ya ukomo wa bajeti kutokana na baadhi ya shughuli muhimu kushindwa kuingia katika bajeti kutokana na viwango vidogo vya bajeti vilivyowekwa na TAMISEMI na hivyo kuathiri bajeti kushindwa kuingizwa vitu muhimu ili kufikia malengo na kuondoa kero zilizoko katika jamii
Kisori amesema kutokana na hali hiyo halmashauri imelazimika kuomba fedha nje ya bajeti ya kawaida kiasi cha shilingi 3,558,000,000/= kwa ajili ya kununulia gari la kuzoa taka ngumu mjini Mpanda, kununulia gari la kunyonya maji machafu mjini, matengenezo ya gari la zimamoto na ujenzi wa sekondari ya Kata ya Kakese pamoja na kuweka miundombinu ya umeme katika shule za sekondari zote.
Aidha baraza la madiwani la halmashauri ya mji Mpanda limeridhia na kupitisha makisio ya bajeti ya hamashauri hiyo katika kipindi cha Julai 2012 hadi juni 2013 kiasi cha shilingi 14,688,051,240/= ikiwa ni mapato ya ndani na ruzuku ya serikali kwa ajili ya maendeleo ya halmashauri ya Mji Mpanda
Awali akiwasilisha mapitio ya bajeti ya 2011/2012 Kisori amesema halmashauri yake ilipanga kukusanya kiasi cha shilingi 823,164,000/= kutoka katika vyanzo vya ndani na kuweza kukusanya kiasi cha shilingi 241,873,480/= katika kipindi cha Julai 2012 hadi januari 2012 sawa na asilimia 29.38 ya makisio ambapo kiasi hicho kimefikiwa kwa kutumia mawakala wa ukusanyaji wa ushuru.
Amesema katika kipindi cha bajeti 2011/12 halmashauri ilipanga kuingiza mapato ya shilingi 70,350,000/= kutokana na vyanzo vya mapato vilivyofutwa na kuweza kukusanya shilingi 42,028,500/= sawa na asilimia 60 ya makisio.
Katika hatua nyingine baraza hilo limetoa Baraka zote kwa shirika la nyumba la Taifa kuenza ujenzi wa majengo katika mji wa Mpanda baada ya kuridhia malipo ya shilingi milioni 100 ikiwa ni kwa ajili ya eneo la jingo la starehe maarufu kwa jina la jengo la Paradise eneo litakalojengwa gorofa nne kwa ajili ya matumizi ya kibenki, ofisi na maduka ya biashara
Aidha baraza hilo limepokea na kuridhia maombi ya mamlaka ya viwanja vya ndege nchini juu ya kuomba upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mpanda utakaopelekea kuhamishwa kwa baadhi ya wakazi wa eneo la Nsemulwa Uwanja wa ndege ili kupisha upanuzi huo.
Imeelezwa katika baraza hilo kuwa upanuzi huo taathiri baadhi ya wananchi watakaotakiwa kipisha upanuzi huo baada ya kulipwa fidia na mamlaka husika katika kipindi kifupi kijacho kwani ujenzi unatarajia kuanza katika kipindi kifupi kijacho.\\
MAAFISA WATENDAJI WAAGIZWA KUSHUGHULIKIA MIFUGO HARAMU

Na  Willy Sumia, Mpanda
SERIKALI wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi imewaagiza watendaji wa kata na vijiji kuwajibika katika maeneo yao ya kazi ili kuleta ufanisi katika utendaji wa kazi
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Mpanda, Dr Rajabu Rutengwe Machi 9, 2012 katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda wakati akifunga kikao cha ushauri cha wilaya ya Mpanda DCC
Mkuu huyo wa wilaya amesema hivi sasa watendaji wengi wamekuwa wakisubiria maagizo katika utendaji kazi wao bila kujali kuwa kutenda kazi zao bila maagizo ni nguzo ya utendaji kazi  wao
Amesema katika miji mingi wilayani Mpanda uchafu umeendelea kuchukua nafasi kubwa kuliko hali inayotakiwa kwani katika hali halisi hakuna haja ya kuwa na miji michafu wakati kila mji una watendaji wa serikali wanaotakiwa kuwajibika
Ametoa mfano wa mji wa Ikola kuwa kituo kikuu cha magonjwa wa kuhara na kutapika ugonjwa ambao kimsingi unasababishwa na uchafu hivyo endapo watendaji wataweza kuwajibika na kufanya kazi ipasavyo uchafu ungeondoka wenyewe hata hao wagonjwa wangeeleweka kuwa wametoka mbali
Ameziagiza serikali za vijiji na kata kuwajibika katika suala la mifugo iliyoingia kiholela katika maeneo yao kwani amesema kuwa taarifa za uhakika zinaelekeza kuwa upo ushahidi wa kutosha kuwa wapo baadhi ya watendaji wa kata na vijiji wamekuwa wakichukua pesa ili kuruhusu mifugo kuingia katika maeneo yao
“ ndugu zangu nawaeleza kitu kimoja kikubwa ni kuwa waliokula pesa watazitapika maana naagiza au ng’ombe waondoke wewe ubaki au wewe uondoke  ng’ombe wabaki, sina namna lazima uwajibike kwa ng’ombe uliowapokea” amesema mkuu wa wilaya
Kwa upande mwingine mkuu wa wilaya ameshukuru maafisa mipango wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda kwa kufanya vema katika maandalizi ya miradi ya maendeleo inayoleta mafanikio makubwa katika vijiji na kuweza kuondoa kero mbalimbali kwa wananchi wa wilaya yake
Mkuu wa wilaya ametoa taarifa katika kikao hiki kuwa kuanzia Machi 12, 2012 ataanza ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika kila kata ambapo ataweza kupokea taarifa za miradi, taarifa ya kazi, kukagua miradi na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara katika kila palipo na mradi wa maendeleo
Mada zilizojadiliwa katika kikao cha leo cha DCC ni pamoja na kupitia mpango na bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Mpanda ya mwaka 2012/2013, kupitia mpango wa bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Mlele kwa mwaka 2012/2013 pamoja na uzoefu wa nchi ya Japan katika ugatuaji wa madaraka.
mwisho

RAIS JAKAYA KIKWETE KESHO KULIHUTUBIA TAIFA ,MGOMO WA MADAKTARI WAWEZA KUZUNGUMZIWA

Taarifa zilizotua hivi punde kupitia mwanahabari wa mtandao huu wa www.sumiampanda.blogspot.com kutoka chumba cha habari cha radio Uhuru zinadai kuwa Rais Jakaya Kikwete kesho ijumaa saa 10 jioni atalihutubia Taifa kupitia wazee wa mkoa wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Diamond Jubilee na hutuba yake kurushwa moja kwa moja (live) na TV na radio nchini.


SERIKALI YATANGAZA RASMI MIKOA MIPYA MINNE NA WILAYA 19

Waziri mkuu Mizengo Pinda

Habari ambayo imetua hivi punde katika mtandao huu wa www.sumiampanda.blogspot.com inadai kuwa serikali imetoa matangazo rasmi ya Serikali (Government Notices) kuhusu uanzishaji wa mikoa mipya minne na wilaya mpya 19 ambayo yamechapishwa tangu Machi 2, mwaka huu.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema matangazo hayo ambayo yalisainiwa na Rais Jakaya Kikwete tangu Machi mosi, 2012, yanabainisha mikoa mipya kuwa ni Geita, Katavi, Njombe na Simiyu. Mikoa hii imechapishwa katika Tangazo la Serikali Na. 72.
Wilaya 19 ambazo zimeanzishwa na kuchapishwa katika Tangazo la Serikali Na.73 ni Buhigwe, Busega, Butiama, Chemba, Gairo, Ikungi na Itilima. Wilaya nyingine ni Kakonko, Kalambo, Kaliua, Kyerwa, Mbogwe, Mkalama na Mlele. Nyingine ni Momba, Nyang’hwale, Nyasa, Uvinza na Wanging’ombe.
Kwa mujibu wa matangazo hayo makao makuu ya mikoa hiyo mipya minne yatakuwa kama ifuatavyo: Geita (Geita), Simiyu (Bariadi) Njombe (Njombe) na Katavi (Mpanda).
Mikoa hiyo itakuwa na wilaya zifuatazo; Geita utakuwa na wilaya tano za Bukombe, Chato, Geita, Mbongwe na Nyang’hwale. Mkoa wa Katavi utakuwa na wilaya mbili za Mlele na Mpanda. Mkoa wa Njombe utakuwa na wilaya nne za Makete, Njombe, Ludewa na Wanging’ombe wakati mkoa wa Simiyu utakuwa na wilaya tano za Bariadi, Busega, Maswa, Meatu na Itilima.
Makao makuu ya wilaya mpya zilizoanzishwa ni kama ifuatavyo: Buhigwe (Buhigwe); Busega (Nyashimo); Butiama (Butiama); Chemba (Chemba); Gairo (Gairo); Ikungi (Ikungi) Itilima (Lagangabilili); Kakonko (Kakonko); Kalambo (Matai) na Kaliua (Kaliua).
Nyingine ni Kyerwa (Rubwera); Mbogwe (Mbogwe); Mkalama (Nduguti); Mlele (Inyonga); Momba (Chitete); Nyang’hwale (Kharumwa); Nyasa (Mbamba Bay); Uvinza (Lugufu) na Igwachanya (Wanging’ombe).
Julai 2010, kabla Rais Kikwete hajatoa hotuba ya kulivunja Bunge, Serikali ilitoa uamuzi wa kuunda mikoa mipya minne na wilaya mpya 21. Hata hivyo, baada ya kuhakiki mipaka ya maeneo hayo yote na kuandaa maelezo ya mipaka hiyo vizuri (boundary descriptions), wilaya zilipunguzwa na kubakia 19.
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 3021,
DAR ES SALAAM.
ALHAMISI, MACHI 8, 2012.
www.katavim.blogspot.com

MKOA WA KATAVI NA FURSA ZINAZOPATIKANA: MKUU WA WILAYA ATEMBELEA KATA ZA H/MJI

DC MPANDA ATOA SIKU KUMI NA NNE WALOFAULU KURIPOTI SHULENI
SERIKALI ya wilaya ya Mpanda mkoa tarajiwa wa Katavi imeuagiza uongozi wa Kata ya Ilembo mjini Mpanda kuwasilisha kwake majina ya wahamiaji haramu walioingia katika kata hiyo ili waweze kushughulikiwa mapema iwezekanavyo
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya hiyo Dr Rajabu Rutengwe katika mkutano wa hadhara mara baada ya kuelezwa kero kubwa ya wakulima na wafugaji iliyopo katika kata hiyo iliyodumu kwa takribani miaka mine sasa.
Awali akitoa ufafanuzi wa kaero hiyo afisa mtendaji wa kata ya Ilembo Marry Ngomarufu amesema kuwa ofisi ya kata imeweza kutumia ofisi ya polisi na mahakama kushughulikia migogoro hiyo ingawa bado hali haijaweza kutengamaa kiasi cha kutosha
Mkuu wa wilaya ya Mpanda amesema migogoro mingi ya wahamiaji haramu hasa wafugaji toka mikoa ya kanda ya Ziwa kutokana na baadhi ya wananchi kuuziana maeneo na wafugaji kwa tamaa ya pesa kwa wenye mashamba na badala yake wameuza fursa zao na kuleta migogoro kwa sababu majirani na eneo lililonunuliwa na wafugajia au mfugaji mmoja wao wakauwa wanaendelea kulima na hiyo inakuwa ni sehemu ya chakula cha mifugo na ng’ombe hawana mipaka kama binadamu
Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara Ilembo mkuu wa wilaya amesema urithi pekee kwa motto ni elimu na siyo majumba na magari hivyo amewataka wananchi mahala popote wasimamie watoto kusoma kwa bidii na kuzitumia kwa uhakika fursa za kupata elimu zilizopo b ila kujali kipato cha mzazi au mlezi kwani ni hazina ya baadae kwa wilaya, mkoa na hata taifa kwa ujumla
Amesema hivi sasa serikali imeweka mazingira ya kuhakikisha kuwa watoto wote wanapata elimu ya msingi na sekondari hata kama hawana uwezo kifedha kwani hivi sasa kila kata ina sekondari yake inayotoa fursa kwa watoto wote walioko katika kata kuendelea na masomo ya sekondari pindi wanapofaulu mtihani wa darasa la saba.
Pia mkuu wa wilaya hiyo Dr Rajabu ameagiza watoto wa kike kumi na mmoja waliofaulu kuingia kidato cha kwanza hawajaripoti shuleni wafike shuleni ndani ya kipindi cha siku kumi na nne kuanzia Machi 6, 2012 wawe wamshaanza masomo na taarifa toka kwa mkuu wa shule iwasilishwe kwake baada ya siku kumi na nne kabla serikali ya wilaya haijaanza kuwafuatilia kisheria kwa nini hawajaripoti shuleni kuanza na masomo ya sekondari.
Amewasihi wananchi kuanza kujenga majengo yanayoendana na hadhi ya manispaa kwani muda wa miezi michache ijayo halmashauri ya mji Mpanda utakuwa na hadhi ya manispaa baada ya mkoa wa Katavi kuanza ili kuanza na kasi ya maendeleo ya mkoa wa Katavi ambao umenza kukimbia kimaendeleo kabla ya kuanza kazi rasmi.
Amewahimiza wananchi wa Ilembo kuanza kufanya miradi ya ufugaji kuku hasa akina mama ambao wanaweza kuwa karibu na mifugo hiyo kwani hivi sasa kuku mmoja anauzwa kwa bei ya shilingi elfu kumi na mbili kwa kuku mmoja mdogo na hivyo ukianza kufuga makoo mmmoja akapewa pumba anaweza kuzaa vifaranga mia moja na arobaini kwa mwaka sawa na kuingiza kipato cha shilingi milioni mbili na laki nne kwa mwaka kutoka kwenye kuku mmoja.
Amesema mkoa utakapoanza wageni wanaohitaji kula kuku wataongezeka mara dufu ya sasa na bei itaongezeka mara mbili ya sasa,
“Mnapopita mjini fikeni nyumbani kwangu muone kuku ninaofuga ni wakubwa na ni wengi na nikiwaingiza sokoni sikosi shilingi elfu kumi na tano taslimu” alisema mkuu wa wilaya
Ametoa mfano wa mhe. Waziri Mkuu Mhe. Pinda ambaye anafuga nyuki ambao ni wadudu lakini wana faida kubwa kwa mfugaji na mlaji wa asali kwani hivi sasa bei ya lita moja ya asali ni shilingi elfu kumi wakati mzinga mmoja unaweza kutoa lita arobaini za asli kwa msimu mmoja tu sawa na kuwa utaweza kuvuna shilingi laki nne za mauzo ya asali kwa msimu mmoja, je kwa mwenye mizinga kumi atapata kiasi gani kwa msimu ihali hana gharama ya kuwalishia wala kuweka dawa
Ametoa wito mkwa wananchi kuanza kuzitumia fursa zilizopo za shughuli za kiuchumi ili kusaidia kuwa na miradi inayoweza kusaidia kuondokana na kero za ukosefu wa kipato
Aidha amewasihi wananchi kuanza kujiandaa kwa sense ya watu na makazi itakayofanyika mwezi Agosti mwaka huu kwani tayari maandali yameanza kufanyika na shughuli za msingi za maandalizi ya sense zimekamilika bado mambo machache.


TUMIENI MAJIKO RAFIKI WA MAZINGIRA - MAKAMU WA RAIS
WAKAZI wa mkoa wa Rukwa wametakiwa kutumia majiko yanayotumia kuni na mkaa kidogo ili kupunguza uharibifu wa mazingira katika mkoa huo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Mohamed Gharib Bilal, alitoa rai hiyo jana katika mkutano wa Hadhara katika uwanja wa kumbu kumbu ya Nelson Mandela mjini Sumbawanga
Alisema hivi sasa mkoa wa Rukwa umeanza kupoteza misitu mingi kutokana na kushamiri kwa vitengo vya uharibifu wa mazingira katika maeneo mengi ya mkoa huo vinavyochangiwa na shughuli mbali mbali za binadamu
Alisema kuchoma moto kiholela kunachangia sana kuua mbegu za miti na misitu mingi kuendelea kuteketea kwani miti iliyopo nayo inaendelea kuteketezwa na wachoma mkaa pamoja na matumizi ya kuni kwa ajili ya kupikia.
“hivi sasa ukipita katika maeneo karibu yote vijijini hasa vijiji vya wilaya ya Sumbawanga kumebaki upara licha ya kuwa maeneo hayo yalikuwa na misitu minene tena ya kutisha” alisema Dr Bilali
Alisema umefika wakati wananchi wa Rukwa waanze kubadili tabia na kuona suala la uharibifu wa mazingira kuwa ni sawa na janga la mkoa mzima na lianze kushughulikiwa kwa mikakati maalumu itakayosimamiwa vema na kupunguza uharibifu uliopo sasa.
Alisema kuwa moto kichaa ni moto ambao unachomwa pasipo misingi ya kiutaalamu kwani hata wanaosafisha mashamba wanatumia kuchoma moto na kuuacha unaendelea kuangamiza misitu mingine
Katika mkoa wa Rukwa kumekuwa na utamaduni wa kuchoma moto hasa nyakati za kiangazi kwa lengo la kuwinda, kuchimba panya, kusafisha mashamba baada ya kuvuna mazao pamoja na kutenga maeneo ya kuchungia mifugo yao.
Maeneo yaliyoathirika na uharibifu wa mazingira kwa kiwango kikubwa ni pamoja na wilaya ya Nkasi, Sumbawanga vijijini , wilaya ya kalambo na kata za Inyonga, Kasokola, Mpanda mjini, Magamba, Nsimbo, Uruila na Mtapenda katika wilaya ya Mpanda.
MWISHO
MKOA WA KATAVI NA FURSA ZINAZOPATIKANA: MKUU WA WILAYA ATEMBELEA KATA ZA H/MJI
 Pia fungua www.sumiampanda.blogspot.com

Monday, February 21, 2011

HABARI ZA MICHEZO

April 19, 2012
TAARIFA TOKA TFF LEO ,25 TWIGA STARS KAMBINI APRILI 20
Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Charles Boniface Mkwasa ameita wachezaji 25 watakaoingia kambini kesho (Aprili 20 mwaka huu) kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Zimbabwe inayotarajiwa kuchezwa Aprili 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Mechi hiyo ni sehemu ya maandalizi ya Twiga Stars kabla ya mechi ya mashindano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Ethiopia itakayochezwa Mei 26 mwaka huu jijini Addis Ababa kabla ya timu hizo kurudiana jijini Dar es Salaam wiki mbili baadaye.
Baada ya kuripoti kambini jioni, wachezaji hao watafanyiwa vipimo vya afya (medical examination) siku inayofuata (Aprili 21 mwaka huu) na kuanza mazoezi Aprili 22 mwaka huu. Kambi ya timu hizo itakuwa kwenye hosteli za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ya Ruvu mkoani Pwani.
Wachezaji walioitwa ni Amina Ally kutoka Sekondari ya Lord Baden, Asha Rashid, Aziza Mwadini (New Generation, Zanzibar), Etoe Mlenzi (JKT Mbweni), Evelyne Sekikuto (Mburahati Queens), Fadhila Hamad (Uzuri Queens), Fatuma Bashiri (Simba Queens), Fatuma Khatib (Mburahati Queens) na Fatuma Mustafa (Sayari).
Wengine ni Fatuma Omari (Sayari), Hanifa Idd (Uzuri Queens), Maimuna Said (JKT Mbweni), Mariam Aziz (Tanzanite), Mwajuma Abdallah (Tanzanite), Mwanahamisi Omari (Mburahati Queens), Mwanaidi Tamba (Mburahati Queens), Mwapewa Mtumwa (Sayari) na Rehema Abdul (Lord Baden).
Kikosi hicho pia kina akina Rukia Khamis (Sayari), Semeni Abeid (Tanzanite), Siajabu Hassan (Evergreen), Sophia Mwasikili (Luleburgaz Spor Kulubu, Uturuki), Veneranda Mtamo (Tanzanite), Zena Khamis (Mburahati Queens) na Zena Said (Uzuri Queens).
KUONA NGORONGORO HEROES, SUDAN 3,000/-
Kiingilio cha chini cha mechi ya kuwania kucheza Fainali za Afrika kwa vijana chini ya miaka 20 kati ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Sudan itakayochezwa Jumamosi (Aprili 21 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 3,000.
Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni, na viingilio vingine vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C na B wakati VIP itakuwa ni sh. 15,000.
Sudan inatarajia kuwasili leo mchana kwa ndege ya Ethiopian Airlines ikiwa na msafara wa watu 30 na itafikia hoteli ya Rungwe iliyoko maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam. Jioni itafanya mazoezi Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.
Ngorongoro Heroes tayari iko kambini chini ya Kocha Kim Poulsen, na leo inaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Sudan yenyewe itafanya mazoezi kwenye uwanja huo kesho.
Kesho (Aprili 20 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutakuwa na mkutano kati ya makocha wa timu zote mbili na Waandishi wa Habari.
MKUTANO MKUU TFF APRILI 21, 22
Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) utafanyika kwa siku mbili (Aprili 21 na 22 mwaka huu) kwenye ukumbi wa NSSF Waterfront jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa mkutano huo watawasili jijini kesho (Aprili 20 mwaka huu) na watafikia kwenye hoteli ya Royal Valentino. Wajumbe wanatoka katika vyama vya mpira wa miguu vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu ya Vodacom.
Mkutano huo utakaoanza saa 3 asubuhi utakuwa na ajenda kumi na moja. Baadhi ya ajenda hizo ni hotuba ya Rais wa TFF, taarifa ya utendaji ya mwaka 2011, bajeti ya mwaka 2012 na taarifa ya ukaguzi wa hesabu (audited accounts).
JKT RUVU, SIMBA ZAINGIZA MIL 30/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya JKT Ruvu na Simba lililochezwa jana (Aprili 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 30,095,000.
Jumla ya watazamaji 8,362 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio vya sh. 3,000, sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 15,000. Watazamaji 7,310 kati ya hao walishuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 3,000.
Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 4,590,762.71 kila klabu ilipata sh. 4,455,551.19, uwanja sh. 1,485,183.73.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 1,485,183.73, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 297,036.75 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 297,036.75.
Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 742,591.86, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 148,518.37 na asilimia 10 ya gharama za mechi ni sh. 1,485,183.73.
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000 na nauli ya ndani kwa mtathmini wa waamuzi sh. 10,000.
Mwamuzi wa akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa kamishna, mtathmini wa waamuzi na waamuzi sh. 120,000, gharama ya tiketi sh. 3,750,000, maandalizi ya uwanja (pitch) sh. 400,000, umeme sh. 300,000, usafi na ulinzi kwa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000.
Gharama nyingine ni Jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila tiketi; kila klabu ilipata sh. 585,340 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kilipata sh. 510,720.
SIMBA, MORO UNITED KUCHEZA USIKU
Mechi ya Ligi ya Vodacom kati ya Simba na Moro United iliyokuwa ichezwe Aprili 5 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imerudishwa nyuma hadi Jumatatu ya Aprili 23 mwaka huu kwenye uwanja huo huo na itaanza saa 1 kamili usiku.
Mabadiliko hayo yamefanyika ili kuipa Simba fursa ya kujiandaa vizuri kwa mechi yao ya Kombe la Shirikisho la Afrika dhidi ya Al Ahly Shandy ya Sudan itakayochezwa Aprili 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Pia mechi kati ya Azam na Mtibwa Sugar iliyokuwa ichezwe Aprili 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam imesogezwa mbele hadi Aprili 22 mwaka huu kupisha mechi ya U20 kati ya Tanzania na Sudan itakayochezwa Aprili 21 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi nyingine mbili zimefanyiwa marekebisho; Coastal Union na Kagera Sugar zilizokuwa zicheze jijini Tanga, Aprili 29 mwaka huu, mechi yao imesogezwa hadi Aprili 30 mwaka huu ili kupisha shughuli za Mei Mosi kwenye Uwanja wa Mkwakwani. Nazo Azam na Toto Africans zilizokuwa zicheze Aprili 26 mwaka huu Uwanja wa Chamazi, sasa zitacheza Aprili 28 mwaka huu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Imewekwa na Francis Godwin ni Iringa na matukio 0



Monday, January 31, 2011

FOCUS 2011 - KATAVI REGION ISSUES

Na Willy Sumia, Mpanda
Machi 20,2011
HALMASHAURI ya Mji wa Mpanda mkoa wa katavi imeweza kukusanya mapato kwa asimia 110 kutokana na majaribio ya mabadiliko ya utaratibu wa ukusanyaji mapato ya Halmashauri hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Mji ndugu Joseph Simon Mchina aliliambia JamboLeo juzi kuwa katika kipindi cha mwezi Februari halmashauri yake iliamua kufanya utafiti wa namna ya kuborsha mapato ya halmashauri hiyo kutokana na vyanzo vyake viwili vya mapato kati ya vilivyopo katika halmashauri yake.
Alisema kuwa maeneo ambayo waliamua kuyafanyia utafiti na katika ushuru wa masoko ili kuwa njia bora ya ukusanaji ushuru wa masoko manne yaliyoko Mpanda mjini ambapo kwa kuanzia Mchina alisema halmashauri yake iliamua kufanyia utafiti soko kuu la wilaya ya Mpanda lililoko chini ya halmashauri yake.
Alisema katika utafiti huo ulikuja baada ya halmashauri kunekana haipati mapato ya kutosha kutoka katika vyanzo vyake vya mapato licha ya kuwa na vyanzo vingi hali iliyopelekea kuongeza ushuru kwa wafanyabiashara wa masoko ya mjini hapa hali iliyozua kukuelewana baina ya halmashauri na wafanyabiashara hao hadi suluhu ilipopatikana ya kushusha ushuru huo.
Alisema kimsingi lengo la kutafuta namna ya kuongeza mapato iliendelea kubaki pale pale na hivyo kuipelekea halmashauri kuamua kutafuta namna bora ya ukusanyaji ushuru ili kuziba mianya ambayo ingebainika kukosesha mapato halmashauri.
Kaimu mkurugenzi Mchina alisema kuwa halmashauri iliwahamasisha wafanyabiashara wenyewe kulipia ushuru wa biashara zao katika ofisi za halmashauri bila kupitia kwa mzabuni na watendaji wa soko ambapo kabla ya kuendesha zoezi hilo halmashauri ilikuwa ikikusanya asilimia 30-40 kwa mwezi lakini baada ya kukusanya kwa wafanyabiashara katika kipindi cha mwezi februari halmashauri imeweza kukusanya kwa asilimia 110.
Alisema hapo awali halmashauri ilikuwa ikikusanya kiasi cha shilingi milioni 2.2 – milioni 2.5 kwa mwezi katika soko kuu lakini kwa kubadili mfumo wa ulipaji ushuru moja kwa moja kwa wafanyabiashara hao katika mwezi februari halmashauri iliweza kukusanya shilingi milioni 4.8 katika makusanyo lengwa ya shilingi milioni 4 kwa mwezi.
Kufuatia mafanikio hayo kaimu mkurugenzi huyo alidai kuwa hivi sasa halmashauri yake inaangalia uwezekano wa kuwa na utaratibu mpya wa ukusanyaji mapato ya ushuru wa masoko baada ya kubaini kuwa mzabuni anayepewa jukumu la kukusanya mapato anapata pesa nyingi lakini anawasilisha kidogo katika halmashauri.
Alisema endapo wataamua kubakiza wazabuni katika ukusanyaji mapato ya halmashauri atapendekeza iwe ni kwa baadhi ya mapato yasiyohesabika tu na kuwa uzoefu umeoneka kwa mamlaka ya mapato nchini kupokea mapato yak e moja kwa moja toka kwa wafanyabiashara na kufanikiwa bila kupitia kwa mzabuni isipokuwa kwa baadhi ya mapato kama vile kodi za vyombo vya moto.
Kwa muda mrefu halmashauri ya mji wa Mpanda imekuwa ikikabiliwa na ukata kutokana na makusanyo duni ya mapato ya halmashauri hali inayopelekea kushindwa kukabiliana na baadhi ya kero za mji huo ikiwa ni pamoja na changamoto ya mifereji kukosekana katika barabara nzuri za mji huo.
Mwisho.
POLISI
JESHI la polisi mkoani Rukwa linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kukutwa na meno 147 ya kiboko na tembo yenye thamani ya Tshs 6,580,000 katika wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi.

Tukio hili limetokea Januari 23 mwaka huu majira ya sa saa 5:00 usiku baada ya jeshi la polisi pamoja na askari wa wanyama pori wa mbuga ya Taifa ya Katavi kuweka mtego nje kidogo ya kijiji cha Stalike Wilayani Mpanda.

Wananchi baada ya kubaini kuwepo kwa njama za kusafirisha meno ya kiboko na Tembo akiyatoa katika Hifadhi ya Taifa ya katavi walitoa taarifa kwa Askari wa wanyamapori na kuandaliwa mtego ulifanikisha kunasa meno 146 ya tembo na kiboko na Risasi tisa za bunduki mbili za aina ya SMG na SAR.

Aliyekamatwa na men ohayo ni ndugu Mussa David (35) mkazi wa kijiji cha Muze Wilayani Sumbawanga mkoa wa Rukwa kati ya hayo meno 74 ya Kiboko yalikuwa yamehifadhiwa ndani ya begi la nguo pamoja na jino moja la tembo.

Mbali na meno aliyokutwa nayo aliweza kueleza kinaga ubaga kuwa mengine yapo nyumbani kwake katika kijiji cha Muze ambako askari hao walipofika nyumbani kwake aliwaonesha shehena ya meno 72 ya kiboko hivyo kufanya idadi ya meno kuongezeka na kufikia 146 yenye thamani ya shilingi milioni 2,500,000 na jino moja la Tembo lenye thamani ya shilingi milioni 4,080,000.

Mara baada ya kukamatwa na nyara hizo aliweza kukiri kuwa amekuwa kinara wa biashara haramu ya meno ya tembo nay a kiboko na kuwa soko lake kubwa liko nchini za Burundi na Congo DRC.

Akithibitisha tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa Isuto Mantage amesema meno, hayo yalikutwa yamefukiwa chini ya ardhi pamoja na risasi Tisa za bunduki aina ya SMG na SAR shambani kwa ndugu Romwadi Isobila(46) na kwamba watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi wa awali kukamilika.

MWISHO


January 15, 2011
WANAFUNZI  2136 wa Kata ya Kibaoni wilaya ya Mpanda mkoani Katavi watanufaika na msaada wa Kilogramu 450 za sukari zilizotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Katavi.
Sukari hiyo iliyokabidhiwa juzi Januari 14,2011 na Msaidizi wake katika jimbo la Katavi Charles Kanyanda imegawiwa kwa shule za kata ya Kibaoni za Msingi na shule ya sekondari ya kata hiyo iitwayo Mizengo Pinda sekondari itawasaidia wanafunzi kupata uji wakati wa masomo katika shule hizo.
Akikabidhi sukari hiyo ndugu Kanyanda ambaye ni msaidizi wa Mheshimiwa Pinda katika jimbo la Katavi ambalo kata ya Kibaoni ni mojawapo katika ya kata zinazounda jimbo hilo alisema kuwa sukari hiyo imetolewa na mbunge wao Mheshimiwa Pinda kwa lengo la kuanzisha utaratibu wa kutoa
chakula cha mchana kwa wanafunzi kama ambavyo serikali imekuwa ikisisitiza kuwepo kwa utaratibu huo mashuleni.
Alisema serikali za vijiji zitambue kuwa shule zilizoko katika maeneo yao ni mali ya serikali ya kijiji na hivyo ziatakiwa kuanza kuwajibika kwa masuala yote ya uendeshaji wa shule hizo hasa katika kuhakikisha wanafunzi wanaanza kupata mlo wa mchana mashuleni ili kupunguza utoro na kuongeza ufanisi mashuleni
Mheshimiwa Waziri Mkuu ametoa sukari kiasi cha mifuko 45 ya kilogramu hamsini kila mmoja kwa shule ya msingi Kakuni iliyoko kijijini kwao
Kibaoni, mifuko 15 yenye uzito wa kilogramu 50 kila mmoja kwa shule ya sekondari ya Mizengo Pinda na shule za msingi za Ilalangulu na Mirumba kiasi cha mifuko 15 kila moja mifuko yenye uzito wa kilogramu hamsini kila mfuko.
Afisa kutoka idara ya Elimu ya Halmashauri ya wilaya ya Mpanda ndugu Venance Tesha akitoa shukrani kwa niaba ya Halmashauri alisema kuwa sukari iliyotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa shule za Kata ya Kibaoni ni changamoto kwa wazazi wa kata hiyo kuanza kujipanga ili kuuendeleza utaratibu wa utoaji uji na chakula mashuleni mara baada ya sukari hiyo kuisha.
“Wazazi na walezi wa kata hii mnatakiwa kuanza kujipanga sasa ili kuendesha michango itakayoendeleza utaratibu wa utoaji chakula mashuleni pindi sukari hii itakapoisha!!” alisema Tesha
Alisema licha ya kuwa Halmashauri inamshukuru Mheshimiwa Pinda bali inatoa shukrani za dhati na  pongezi nyingi kwake kwa kutoa sukari ambayo imewapa changamoto halmashauri kuhakikisha utaratibu huo wa kutoa chakula mashuleni hasa katika shule za msingi unaendeshwa katika shule zote wilayani Mpanda.
“Labda niseme kwamba kitendo alichokifanya Mheshimiwa Pinda ni kutupatia shughuli ya kufanya kwakuwa kama bosi wako kaanzisha uji shuleni katika kata zilizoko jimboni kwake wewe unangoja nini
kuanzisha huo utaratibu katika maeneo mengine, lazioma kama halmashauri tumshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kutuamsha” Alisema Tesha.
Baadhi ya walimu wa shule za msingi katika kata ya kibaoni wakizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano hayo walisema kuwa mpango wa utoaji uji shuleni utapunguza utoro na kuongeza ufanisi kwa wanafunzi katika kujifunza.
“Unajua mwanafunzi wakati wa mchana huwa hawasomi hata kama wako darasani kwa sababu ya njaa! Hata kama mwalimu ukiingia unagundua kuwa humu darasani wanaonisikiliza ni wachache wengine wanakuwa wameshabanwa na njaa na hivo kumbu kumbu inakuwa imepungua sana” alisema mwalimu Mwakifuna wa shule ya msingi Kakuni
Alifafanua kuwa licha ya kuwa uji utapunguza utoro mashuleni lakini pia utajenga mazingira bora ya kujifunza katika vipindi vya mchana na kujenga hamasa ya kuanza shule  kwa watoto wanaokwepa kuanza shule katika jamii.
Walimu hao walimuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu siku moja afike shuleni hapo kushuhudia namna wanafunzi wanavyoufurahia uji wakiwa shuleni na kushirikiana nao japo siku moja.
MWISHO.
Na Willy Sumia, Katavi
ASKARI wa jeshi la mgambo katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda Mkoa mpya wa Katavi wamenusurika kipigo kutoka kwa wafanya biashara wa masoko matatu tofauti  kufuatia kupandishwa kwa ushuru wa masoko hayo.
Vurugu zilianza mara baada ya askari hao kufika katika masoko yaliyoko mjini hapa  kukusanya ushuru ambao umegomewa na wafanya biashara hao kwa madai ya ongezeko kubwa la ushuru kuliko hali halisi ya kipato cha biashara zao sokono hapo.
Tukio hilo limetokea jana katika muda tofauti mara baada ya askari wa mgambo hao pamoja na wakala wa kukusanya ushuru wa masoko ya mji kufika katika maeneo yao kwa lengo la kukusanya ushuru ambao unapingwa na wafanya biashara hao kwa kile kinachodaiwa na wafanya biashara hao kuwa ni ongezeko kubwa la ushuru.
Akizungumzia matukio hayo katibu wa wafanyabiashara wa Mji huo Amani Mahela ametoa wito kwa Mkurugenzi wa Mji kufika kwenye masoko hayo na kufanya mazungumzo na wafanya biashara badala ya utaratibu anaoutumia sasa wa kutoa matangazo kwenye vyombo vya habari akiwataka walipe ongezeko hilo la ushuru kabla ya kufanya mazungumzo nao.
Diwani wa kata ya Kashaulili John Matongo  amesema kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji ameitisha kikao cha Madiwani wa kata tatu na viongozi wa wafanyabishara toka katika masoko yaliyo na mgogoro wa
ushuru  ili kujadili namna ya kutatua tatizo hilo
Halmashauri ya Mji wa Mpanda imebandika matangazo katika masoko hayo matatu akiwaeleza wafanya biashara kuwa wale ambao hawatakuwa tayari
kulipa ongezeko la ushuru waondoke katika maeneo ya masoko hayo Kaimu mkurugenzi wa Mji Mpanda Josefu Mchina aliwaeleza waandishi wa habari ofisini kwake kuwa ushuru ni suala la kisheria na huwa lina
mchakato wake katika kuuanzisha, kuongeza  au kuupunguza kabla ya kuanza utekelezaji hivyo ushuru unaolalamikiwa ni halali kisheria na pia umezingatia hali halisi ya bishara na mahitaji ya maendeleo katika
masoko na mji kwa ujumla.


Na WALTER  Mguluchuma
Mpanda
Madiwani wa chama cha mapinduzi (CCM) katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda wamesusia sherehe ya kumuaga Mkurugenzi wao kutokana na itikadi za siasa
Tukio hilo limetokea hapo jana ambapo Halmashauri ya Mji wa Mpanda iliandaa sherehe ya kumuaga Mkurugenzi wao ambaye alikuwa anastaafu utumishi Bwana Henry Haule
Sherehe za kumuaga Mkurugenzi huyo zilifanyika katika Ukumbi wa Katavi Resort mali ya Abrahamu Kombe ambaye anadaiwa na Madiwani hao kuwa aliwasariti kwenye uchaguzi Mkuu na kuisaidia Chadema
Madiwani hao baada ya kupata taarifa za sherehe za kumuaga mkurugenzi wao kweny Ukumbi wa Katavi walianza kupinga na kutaka sherehe hizo zifanyike kwenye Ukumbi wa Idara ya Mji ambao hata hivyo ulikuwa umeandaliwa kwa shughuli za Mkutano wa wawekezaji na Waziri Mkuu
Sherehe hizo zilianza huku ndani ya Ukumbi kukiwa na madiwani wawili wa kata za kashaulili na makanyagio ambao ni wa Chadema
Wakati sherehe zikiendelea madiwani hao waliendelea na kikao chao nje ya Ukumbi huo kwa lengo la kuendelea na msimamo wao huo Hata hivyo wakati sherehe zikienda mwisho waliingia madiwani wawili wa Chama hicho ambao ni Enock Gwambasa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji huo pamoja na diwani Willy Mbogo
Walipo hojiwa Madiwani hao sababu iliowafanya waingie mwishoni mwa sherehe walisema tulikuwa na mvutano na wenzetu ila sisi tumeamua kuingia kwenye sherehe
Na Peti Siyame umbawanga
MWENDESHA  pikipiki  aitwaye Ramadhani  Sood (25)  amefariki  dunia baada ya kugongwa na  gari  katika kijiji cha  Makanyagio  katika barabara  ya Mpanda –Shanwe iliyopo  wilayani Mpanda katika mkoa wa Rukwa.
Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Isuto Mantage  alisema  kuwa  ajali hiyo  ililihusisha   basi la abiria aina  ya scania  yenye  namba  za usajili  T 519  ACV iliyokuwa ikiendeshwa  na dereva  aitwaye Masoud
Musa (32) mkazi wa  Makanyagio  mjini Mpanda
Kwa mujibu wa Kamanda huyo wa Polisi  gari  hilo  la  abiria lilimgonga  mwendesha pikipiki  Ramadhani  mkazi wa Makanyagio aliyekuwa  akiendesha pikipiki aina ya  Honda  yenye  namba  za
usajiri  T. 612 ANT na kumsababishia  majeraha  makubwa .
“Ramadhani  aliyekuwa  mahututi  ambapo  alikuwa na  majeraha makubwa mwilini  alifariki  muda mfupi  baada ya kufikishwa  kwenye  hospitali  ya  wilaya ya Mpanda  kwa matibabu” alisema  Mantage .
Kamanda Mantage  alisema kuwa  chanjo  cha  ajali  hiyo  bado hakijajulikana  na kwamba  dereva  wa  gari  alikamatwa  na atafikishwa  mahakamani  mara  baada ya  uchunguzi  wa awali kukamilika

Monday, September 13, 2010

GAZETI LA LEO - MPANDA

NKASI - WAMPEMBE - 17 MBARONI KWA KUVAMIA KITUO CHA POLISI
WATU kumi na saba wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Rukwa kwa tuhuma za kuvamia kituo cha polisi kwa lengo la kutaka kukiteketeza kituo hicho kwa moto.
Kamanda wa polisi mkoani Rukwa Isuto Mantage amesema Novemba 30,2010 ofisini kwake kuwa wanaoshikiliwa ni wanakijiji wa kijiji cha Wampembe wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa baada ya jaribio la kutaka kukitekeza kwa moto kituo kidogo cha polisi cha Wampembe kwa lengo la kumuua mtu mmoja waliyekuwa wanadai kuwa ni mchawi.
Amesema kuwa awali katika kijiji hicho kulitokea msiba wa kijana aliyetajwa kwa jina la Joseph Kapelo (19) baada ya kuugua muda mfupi mnamo Novemba 22, 2010 ambapo kijana huyo aligua majira ya saa mbili asubuhi nakufariki saa tano mchana kifo kilichozua mijadala kijijini hapo wakazi wengi wakidai kuwa marehemu alikuwa amefariki kutokana na imani za kishirikina.
Amefafanua kuwa baada ya kupata taarifa za kifo hicho wananchi walianza kukusanyika katika msiba na kuanza kupanga mikakati ya kummaliza baba wa marehemu aliyetajwa kwa jina la ndugu Daudi Kapelo (76) kwa madai kuwa ndiye aliyamuua mwanae huyo kwani ni miezi miwili tu tangu kijana mwingine mtoto wa huyo mzee alifariki katika mazingira ya kutatanisha kama ilivyotokea katika huo msiba.
Amesema kuwa wakati wananchi hao wakipanga mikakati hiyo taarifa zilifika kituo kidogo cha polisi Wampembe ambapo polisi wa kituo hicho waliweza kuchukua hatua ya kumuokoa Mzee huyo lakini kabla hawajafika msibani tayari Mzee huyo alikuwa ameshaanza kushambuliwa na wananchi na kuokolewa na polisi na mgambo na kasha kuchukuliwa na kwenda kuhifadhiwa kituo cha polisi kwa usalama wake.
Amesema wakati wananchi hai wakielekea kuzika walichukua jeneza la marehemu na kwenda nalo hadi kituo cha polisi ambapo waliliweka jeneza hilo hapo kituoni na kudai wanataka Mzee Daudi Kapelo atolewe humo ndani wammalize naye akazikwe na mwanae na kuanza kushambulia kituo hicho kwa mawe hali iliyopelekea askari kupiga risasi hewani lakini wananchi hao hawakuweza kuogopa na kuanza kumshambulia askari huyo na kuibua mapigano baina ya askari na wananchi wapatao 300.
Amesema kuwa wananchi hao baada ya kutawanyika walikimbia wote wakiwa tayari wameshawasha moto kituo cha polisi kikiungua ambapo askari polisi na mgambo kwa kusaidiana na viongozi wa kijiji walifanikiwa kuuzima moto huo na wananchi hao waliweza kurudi usiku wakachukua maiti ya merehemu na kwenda kuzika usiku huo huo.
Amesema mapambano hayo yaliendelea ambapo mwananchi mmoja Imelda Kayanda (46) alipigwa risasi na kufariki na Agnes Kisori(21) alijeruhiwa mguuni huku vitu vilivyoharibiwa vikiwa ni pamoja na solar panel ya kituo, vioo vya kituo vyote kwa pamoja vikiwa na thamani ya shilingi laki tano.
Amesema majeruhi walipelekwa kituo cha afya Wampembe na baadae hospitali ya wilaya ya Nkasi kupata matibabu ambapo hali zao zimeelezewa kuwa zinaendelea vema.
Amesema tayari jeshi la polisi limewakamata ndugu Zakaria Francis (28), Ikombe Yustini (39), Stephano Kambe (18), Benard Kabeja (16) na John Kapandila (22).
Wengine waliokamatwa amewataja kuwa ni ndugu Said Diwali (36), Vido Tuwakazi (21), Abdalah Vicent (19), Sylveter Kapala (17), Richad Bushota (19), John Mathias (58), Wilbroad Chambi (16) na Kapondo Anatoli (23) na wengine wane wote wakazi wa kijiji cha Wampembe wilaya ya Nkasi.
Kamanda wa Polisi amesema wakati watuhumiwa hao wote watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika na kuwa wengine waliokimbia watafuatiliwa hadi wakamatwe ili sheria ichukue mkondo wake.
Aidha kamanda Mantage ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na tabia mbaya ya kuvamia vituo vya polisi nchini hapa nchini kuwa vinalipeleka taifa kusikojulikana kutokana na ukweli kuwa hizo ni dalili za kuondoa misingi ya amani na utulivu katika jamii.
MWISHO
MBUNGE mmoja wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Mpanda amelalamikiwa kuwafanyia kitu mbaya vijana watatu akiwemo mlemavu asiyekuwa na uwezo wa kutembea.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa mbunge huyo mwenye sifa ya kuitwa Mbuyu mdogo amewadhulumu vijana watatu waliokuwa watumishi wa ofisi yake ya bunge katika jimbo lake ofisi zilizoko mjini Mpanda baada ya kuwatumikisha bila kuwalipa mishahara yao halali.
Wakiongea kwa uchungu vijana hao pamoja na binti mmoja mlemavu wa miguu aisyeweza kutembea kwa miguu ya kawaida walidai kuwa mbunge huyo amewadhulumu zaidi ya shilingi miliono moja na laki nane zikiwa ni mishahara na posho za kazi zaidi ya shilingi milioni moja na laki mbili.
Kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Peter Pulwila Panta aliyekuwa ameajiriwa kwa kazi ya udereva na kupewa kitambulisho chenye nambari 001 alisema wamekuwa wakimdai mbunge huyo mishahara yao lakini cha kusikitisha amekuwa akidai kuwa hizo pesa hajaletewa kutoka ofisi ya bunge kitu ambacho si kweli kutokana na maelezo yaliyoko katika barua yenye kumb namba FA.155/2006/01/70.
Alisema licha ya kuwa barua inaagiza kuwalipa mshahara wa kiasi cha shilingi 150,000 kwa mwezi lakini yeye aliwaeleza kuwa watakuwa wanalipwa shilingi laki moja kila mwezi na kuwa alikuwa anakidai kuwa anawalipa kutokana na mshahara wake wa ubunge ihali barua inaonesha kuwa fedha hizo zinatumwa kila mwezi katika akaunti ya mbunge huyo kwa ajili ya mishahara na posho.
Naye binti mwenye ulemavu aliyekuwa akifanya kazi kama mhudumu wa ofisi ya mbunge huyo alisema kuwa tangu mwaka 2005 alikuwa akifanya kazi na kupewa hela ya soda tu shilingi 20,000/= tu kila anapodai mshara wake na kuwa ukosefu wa mshahara kumepelekea mwanaye anayesoma katika shule ya sekondari Mwese kuzuia kuendelea masomo kutokana na madeni ya ada.
Alipofuatwa na mwandishi wa habari ofisini kwake kujua kulikoni anadaiwa na watumishi wake akiwemo mlemavu wa miguu lakini mbunge huyo hakuweza kupatikana badala yake alikuwepo mtu aliyejieleza kuwa ni katibu wa mbunge huyo ingawa alikataa ktaja jina lake aliyeeleza kuwa mbunge wake yuko katika kikao CCM
Juhudi za kumtafuta kwa simu mbunge huyo zilifanikiwa ambapo mbunge huyo alijibu katika simu kuwa anahitaji kuonana na mwandishi wa habari.
Cha kushangaza ni kuwa alikwenda mwandishi ofisini kwake kuzungumzia suala la madeni na kuzomewa alikozomewa wakati wa mkutano wa hadhara katika kijiji kimoja mbunge huyo alimsihi mwandishi huyo asiandike taarifa yoyote mbaya kumhusu na kumpatia kiasi cha shilingi elfu ishirini kwa ajili ya kumziba mdomo pesa ambazo mwandishi alizikataa na kuondoka
Uchunguzi umebaini kuwa madai hayo na mengine mengi yalishawahi kufikishwa katika ofisi za CCM wilaya ya Mpanda na kukosa suluhu ambapo mbunge huyo amekuwa akijinadi kuwa ni mtaalamu wa propaganda, mbuyu mdogo anataka kugombea mwakani kutetea kiti cha ubunge hivyo wasimjadili kuhusu madeni yake.
Mbunge huyo alijikuta akitemwa katika kura ya maoni ndani ya chama chake katika uchaguzi mkuu wa 2010 nchini Tanzania
MWISHO

MILIONI KUMI HIZI ZIMETUMIKA KWELI NAMNA HII
ZAIDI ya shilingi milini 10.1 zimetumika kwa ajili ya kuwanunulia sare za shule na kuwalipia ada na chakula watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu wilaya ya Mpanda mkoani Rukwa
Mratibu wa asasi isiyokuwa ya kiserikali ya SHDEPHA + tawi la Mpanda Mwalimu Euzebius Ngulusha alisema hayo jana (Novemba 3, 2009) wakati wa hafla fupi ya kuwakabidhi sare, chakula na mahitaji ya shuleni watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi wapatao 54 iliyofanyika katika ukumbi wa SHDEPHA + mjini Mpanda.
Alisema katika kipindi cha Januari hadi Oktoba mwaka huu zaidi ya shilingi milini 10.1 zimetumika kuwahudumia watoto 204 wanaoishi katika mazingira hatarishi, yatima na watoto wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wilayani Mpanda fedha ambazo zimetoka kwa wafadhili mbalimbali ikiwa ni pamoja na shirika la Kimarekani la WALTER REED la nchini Marekani.
Alisema shirika lake limelipia ada za sekondari na kuwanunulia sare za shule watoto wanaosoma katika shule za sekondari wapatao 150 kwa gharama ya shilingi 8,304,300/= na watoto wanaosoma shule za Msingi wapatao 35 na wachache wanaotoka katika mazingira hatarishi.
Alisema kiasi cha shilingi 1,800,000 zimetumika kuwanunulia mahitaji ya shuleni kama vile daftari, kalamu, vihifadhio, mifuko ya shule na vifaa vya kuchorea vya wanafunzi hao ili nao wajisikie kama sehemu ya jamii.
Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mji wa Mpanda afisaelimu wa sekondari wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Said Mwapongo aliwashukuru viongozi wa asasi hiyo ya SHDEPHA + kwa kufanya kazi ya kuwasaidia wanaohitaji katika jamii na kuvishinda vishawishi wanavyokumbana navyo vishawishi ambavyo amesema vinawapelekea kushikwa na tamaa ya kutumia fedha hizo bila kujali ni za nani.
Alisema moyo wa kuwafikishia walengwa ambao hawakujua kama wanaletewa nini ni moyo wa kipekee na wa kiungwana ambapo amewasihi kutokukata tamaa na kuwa Mungu peke yake ndiye atakayewalipa kwa kazi njema hiyo.
Mwapongo aliwasihi wanafunzi hao kuitumia misaada waliyoipata na wanayoendelea kuipata kwa kusoma kwa bidii, kuwa na heshima katika jamii ili kuwawezesha kufikia malengo yao ambayo ni kuwaondoa katika lindi la maisha ya masikitiko na umasikini uliopindukia.
MWISHO

WANANCHI HAWA WAMECHUKIA DILI ZA POLISI AU NI HASIRA KWELI?
WANANCHI wenye hasira wamefanikiwa kuliua jambazi lililokuwa likitafutwa na jeshi la polisi mkoani Rukwa baada ya kumkuta akiiba magunia ya mpunga
Akiyeuwawa ametajwa kwa jina la Revocatus Benedicto Katunga mwenye umri wa miaka 33 mkazi wa Nsemulwa mjini mpanda ambaye aliuwawa na wananchi Septemba 23,2009 saa kumi na mbili asubuhi mara baada ya kukutwa akiiba magunia ya mpunga katika mashine ya kusaga ya mfanyabiashara anayejulikana kwa jina la Kasimu lyanga maarufu kwa jina la Usayi.
Kamanda wa polisi mkoani Rukwa Isuto Mantage aliwaeleza waandishi wa habari kuwa siku ya tukio marehemu anayesadikiwa kuwa ni jambazi sugu aliyekuwa anatafutwa na jeshi hilo alikutwa na wananchi akiwa katika harakati za kuiba magunia ya mpunga ambapo alikuwa ameshaiba magunia manne ya kuyatoa nje ya jingo hilo .
Alisema baada ya kumkuta marehemu huyo wananchi hao walianza kumhoji lakini akawa anawajibu maneno ya jeuri kwa sauti kubwa iliyowaamusha majirani wengine waliofika hapo na kumkuta jambazi huyo aliyekuwa akitafutwa na jeshi la polisi mkoani Rukwa kwa tuhuma za kushiriki katika matukio kadhaa ya uhalifu walianza kumpa kipigo hadi akapoteza fahamu ndipo wakawaita polisi kituo cha Mpanda.
Alisema kamanda Mantage kuwa polisi walipofika eneo la tukio walimchukua marehemu na kumwahisha hospitali ambako kabla ya kupewa huduma yoyote alifariki akiwa eneo la hospitali.
Kamanda alisema hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo ambapo alieleza kuwa marehemu alikuwa akitafutwa kwa kosa la kuvunja na kuiba vitabu katika shule ya msingi Katavi iliyoko mjini Mpanda na pia alikuwa na kesi mahakani ya kuiba kwa kutumia silaha
Kwa upande wao wananchi wa eneo la Mpanda Hoteli mjini Mpanda walionesha kusikitishwa kwao na mwenendo wa utendaji kazi wa jeshi la polisi wilayani Mpanda kwani jambazi huyo alikuwa ameshikana kukamatwa na jeshi hilo hadi walipomkamata wananchi wenyewe na kumpa hukumu ya kifo licha ya kuwa alikuwa na matukio mengi ya kutafutwa.
the end

Sunday, August 22, 2010

CHAKACHUA YA PINDA YAISUMBUA CHADEMA

Na Willy Sumia, Mpanda
WAZIRI mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda ambaye amepita bila kupingwa katika kinyang’anyiro cha ubunge katika jimbo la Katavi mkoa wa Katavi kumeelezewa na wananchi wa jimbo lake kuwa ni uamuzi wa siku nyingi kabla hajateuliwa kuwa Waziri Mkuu.
Hayo yalielezwa na baadhi ya wananchi wa jimbo hilo katika mahojiano ya hivi karibuni na waandishi wa Habari mara baada ya tume ya uchaguzi jimbo la Katavi kutangaza kuwa Pinda amepita bila kupingwa kutokana na wagombea wane wa CUF, CHADEMA, NLD na CHADEMA kujitoa katika kinyang’anyiro hicho kwa barua.
Wananchi hao wanaotoka katika vijiji vya Ilunde, Ilela, Majimoto, Kasansa na Kilida walidai kuwa tangu Pinda awe mbunge wa jimbo lao lililokuwa awali likiitwa jimbo la Mpanda Mashariki kumekuwa na maendeleo makubwa pamoja na mabadiliko ya kiuchumi kwa wananchi hao.
Ndugu Hussein Omari mkazi wa kijiji cha Inyonga alisema kuwa wananchi wa tarafa ya Inyonga walikuwa wakiteseka sana kutokana na kukosekana kwa barabara ya uhakika na mawasiliano ya simu lakini tangu Pinda awe mbunge wao wameweza kupata miundombinu hiyo kwa kasi ya ajabu.
Mmoja wa wagombea waliokuwa wametangaza nia ya kugombea katika jimbo hilo ndugu Sebastiani Kasinge alisema kuwa mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Katavi kwa Pinda alipata upinzani mkubwa sana toka kwa wananchi wa jimbo hilo, ndugu zake na hata ndani ya Chama chake cha CHADEMA.
Alisema kuwa uamuzi wake wa kuchukua fomukatika jimbo hilo ulipelekea mvutano mkubwa ndani ya CHADEMA na kupelekea mbunge wa jimbo la Mpanda kati CHADEMA Said Arfi kutangaza kujitoa katika uchaguzi iwapo chama chake kingesimamisha mgombea jimbo la Pinda ambapo mwenyekiti wa CHADEMA mwasisi aliamua kujivua uanachama wa CHADEMA na kuhamia chama kingine cha siasa katika kikao kilichokuwa kikijadili wagombea.
Chanzo cha uhakika cha habari toka katika chama cha CHADEMA kimeeleza kuwa CHADEMA ndio waliokuwa wakishinikiza Pinda apite bila kupingwa katika jimbo hilo lakini baadhi ya viongozi wa CCM walikuwa wakitaka kuwepo na mgombea ili wapate mshiko wa kampeni katika jimbo hilo na kutofautiana na katibu wa CCM wa wilaya Mohamed Omary Nyawenga aliyeonekana akifanya juhudi za kweli kuhakikisha Pinda anapita bila kupingwa akishirikiana na baadhi ya wananchi wa Inyonga.
MWISHO