Monday, January 31, 2011

FOCUS 2011 - KATAVI REGION ISSUES

Na Willy Sumia, Mpanda
Machi 20,2011
HALMASHAURI ya Mji wa Mpanda mkoa wa katavi imeweza kukusanya mapato kwa asimia 110 kutokana na majaribio ya mabadiliko ya utaratibu wa ukusanyaji mapato ya Halmashauri hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Mji ndugu Joseph Simon Mchina aliliambia JamboLeo juzi kuwa katika kipindi cha mwezi Februari halmashauri yake iliamua kufanya utafiti wa namna ya kuborsha mapato ya halmashauri hiyo kutokana na vyanzo vyake viwili vya mapato kati ya vilivyopo katika halmashauri yake.
Alisema kuwa maeneo ambayo waliamua kuyafanyia utafiti na katika ushuru wa masoko ili kuwa njia bora ya ukusanaji ushuru wa masoko manne yaliyoko Mpanda mjini ambapo kwa kuanzia Mchina alisema halmashauri yake iliamua kufanyia utafiti soko kuu la wilaya ya Mpanda lililoko chini ya halmashauri yake.
Alisema katika utafiti huo ulikuja baada ya halmashauri kunekana haipati mapato ya kutosha kutoka katika vyanzo vyake vya mapato licha ya kuwa na vyanzo vingi hali iliyopelekea kuongeza ushuru kwa wafanyabiashara wa masoko ya mjini hapa hali iliyozua kukuelewana baina ya halmashauri na wafanyabiashara hao hadi suluhu ilipopatikana ya kushusha ushuru huo.
Alisema kimsingi lengo la kutafuta namna ya kuongeza mapato iliendelea kubaki pale pale na hivyo kuipelekea halmashauri kuamua kutafuta namna bora ya ukusanyaji ushuru ili kuziba mianya ambayo ingebainika kukosesha mapato halmashauri.
Kaimu mkurugenzi Mchina alisema kuwa halmashauri iliwahamasisha wafanyabiashara wenyewe kulipia ushuru wa biashara zao katika ofisi za halmashauri bila kupitia kwa mzabuni na watendaji wa soko ambapo kabla ya kuendesha zoezi hilo halmashauri ilikuwa ikikusanya asilimia 30-40 kwa mwezi lakini baada ya kukusanya kwa wafanyabiashara katika kipindi cha mwezi februari halmashauri imeweza kukusanya kwa asilimia 110.
Alisema hapo awali halmashauri ilikuwa ikikusanya kiasi cha shilingi milioni 2.2 – milioni 2.5 kwa mwezi katika soko kuu lakini kwa kubadili mfumo wa ulipaji ushuru moja kwa moja kwa wafanyabiashara hao katika mwezi februari halmashauri iliweza kukusanya shilingi milioni 4.8 katika makusanyo lengwa ya shilingi milioni 4 kwa mwezi.
Kufuatia mafanikio hayo kaimu mkurugenzi huyo alidai kuwa hivi sasa halmashauri yake inaangalia uwezekano wa kuwa na utaratibu mpya wa ukusanyaji mapato ya ushuru wa masoko baada ya kubaini kuwa mzabuni anayepewa jukumu la kukusanya mapato anapata pesa nyingi lakini anawasilisha kidogo katika halmashauri.
Alisema endapo wataamua kubakiza wazabuni katika ukusanyaji mapato ya halmashauri atapendekeza iwe ni kwa baadhi ya mapato yasiyohesabika tu na kuwa uzoefu umeoneka kwa mamlaka ya mapato nchini kupokea mapato yak e moja kwa moja toka kwa wafanyabiashara na kufanikiwa bila kupitia kwa mzabuni isipokuwa kwa baadhi ya mapato kama vile kodi za vyombo vya moto.
Kwa muda mrefu halmashauri ya mji wa Mpanda imekuwa ikikabiliwa na ukata kutokana na makusanyo duni ya mapato ya halmashauri hali inayopelekea kushindwa kukabiliana na baadhi ya kero za mji huo ikiwa ni pamoja na changamoto ya mifereji kukosekana katika barabara nzuri za mji huo.
Mwisho.
POLISI
JESHI la polisi mkoani Rukwa linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kukutwa na meno 147 ya kiboko na tembo yenye thamani ya Tshs 6,580,000 katika wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi.

Tukio hili limetokea Januari 23 mwaka huu majira ya sa saa 5:00 usiku baada ya jeshi la polisi pamoja na askari wa wanyama pori wa mbuga ya Taifa ya Katavi kuweka mtego nje kidogo ya kijiji cha Stalike Wilayani Mpanda.

Wananchi baada ya kubaini kuwepo kwa njama za kusafirisha meno ya kiboko na Tembo akiyatoa katika Hifadhi ya Taifa ya katavi walitoa taarifa kwa Askari wa wanyamapori na kuandaliwa mtego ulifanikisha kunasa meno 146 ya tembo na kiboko na Risasi tisa za bunduki mbili za aina ya SMG na SAR.

Aliyekamatwa na men ohayo ni ndugu Mussa David (35) mkazi wa kijiji cha Muze Wilayani Sumbawanga mkoa wa Rukwa kati ya hayo meno 74 ya Kiboko yalikuwa yamehifadhiwa ndani ya begi la nguo pamoja na jino moja la tembo.

Mbali na meno aliyokutwa nayo aliweza kueleza kinaga ubaga kuwa mengine yapo nyumbani kwake katika kijiji cha Muze ambako askari hao walipofika nyumbani kwake aliwaonesha shehena ya meno 72 ya kiboko hivyo kufanya idadi ya meno kuongezeka na kufikia 146 yenye thamani ya shilingi milioni 2,500,000 na jino moja la Tembo lenye thamani ya shilingi milioni 4,080,000.

Mara baada ya kukamatwa na nyara hizo aliweza kukiri kuwa amekuwa kinara wa biashara haramu ya meno ya tembo nay a kiboko na kuwa soko lake kubwa liko nchini za Burundi na Congo DRC.

Akithibitisha tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa Isuto Mantage amesema meno, hayo yalikutwa yamefukiwa chini ya ardhi pamoja na risasi Tisa za bunduki aina ya SMG na SAR shambani kwa ndugu Romwadi Isobila(46) na kwamba watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi wa awali kukamilika.

MWISHO


January 15, 2011
WANAFUNZI  2136 wa Kata ya Kibaoni wilaya ya Mpanda mkoani Katavi watanufaika na msaada wa Kilogramu 450 za sukari zilizotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Katavi.
Sukari hiyo iliyokabidhiwa juzi Januari 14,2011 na Msaidizi wake katika jimbo la Katavi Charles Kanyanda imegawiwa kwa shule za kata ya Kibaoni za Msingi na shule ya sekondari ya kata hiyo iitwayo Mizengo Pinda sekondari itawasaidia wanafunzi kupata uji wakati wa masomo katika shule hizo.
Akikabidhi sukari hiyo ndugu Kanyanda ambaye ni msaidizi wa Mheshimiwa Pinda katika jimbo la Katavi ambalo kata ya Kibaoni ni mojawapo katika ya kata zinazounda jimbo hilo alisema kuwa sukari hiyo imetolewa na mbunge wao Mheshimiwa Pinda kwa lengo la kuanzisha utaratibu wa kutoa
chakula cha mchana kwa wanafunzi kama ambavyo serikali imekuwa ikisisitiza kuwepo kwa utaratibu huo mashuleni.
Alisema serikali za vijiji zitambue kuwa shule zilizoko katika maeneo yao ni mali ya serikali ya kijiji na hivyo ziatakiwa kuanza kuwajibika kwa masuala yote ya uendeshaji wa shule hizo hasa katika kuhakikisha wanafunzi wanaanza kupata mlo wa mchana mashuleni ili kupunguza utoro na kuongeza ufanisi mashuleni
Mheshimiwa Waziri Mkuu ametoa sukari kiasi cha mifuko 45 ya kilogramu hamsini kila mmoja kwa shule ya msingi Kakuni iliyoko kijijini kwao
Kibaoni, mifuko 15 yenye uzito wa kilogramu 50 kila mmoja kwa shule ya sekondari ya Mizengo Pinda na shule za msingi za Ilalangulu na Mirumba kiasi cha mifuko 15 kila moja mifuko yenye uzito wa kilogramu hamsini kila mfuko.
Afisa kutoka idara ya Elimu ya Halmashauri ya wilaya ya Mpanda ndugu Venance Tesha akitoa shukrani kwa niaba ya Halmashauri alisema kuwa sukari iliyotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa shule za Kata ya Kibaoni ni changamoto kwa wazazi wa kata hiyo kuanza kujipanga ili kuuendeleza utaratibu wa utoaji uji na chakula mashuleni mara baada ya sukari hiyo kuisha.
“Wazazi na walezi wa kata hii mnatakiwa kuanza kujipanga sasa ili kuendesha michango itakayoendeleza utaratibu wa utoaji chakula mashuleni pindi sukari hii itakapoisha!!” alisema Tesha
Alisema licha ya kuwa Halmashauri inamshukuru Mheshimiwa Pinda bali inatoa shukrani za dhati na  pongezi nyingi kwake kwa kutoa sukari ambayo imewapa changamoto halmashauri kuhakikisha utaratibu huo wa kutoa chakula mashuleni hasa katika shule za msingi unaendeshwa katika shule zote wilayani Mpanda.
“Labda niseme kwamba kitendo alichokifanya Mheshimiwa Pinda ni kutupatia shughuli ya kufanya kwakuwa kama bosi wako kaanzisha uji shuleni katika kata zilizoko jimboni kwake wewe unangoja nini
kuanzisha huo utaratibu katika maeneo mengine, lazioma kama halmashauri tumshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kutuamsha” Alisema Tesha.
Baadhi ya walimu wa shule za msingi katika kata ya kibaoni wakizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano hayo walisema kuwa mpango wa utoaji uji shuleni utapunguza utoro na kuongeza ufanisi kwa wanafunzi katika kujifunza.
“Unajua mwanafunzi wakati wa mchana huwa hawasomi hata kama wako darasani kwa sababu ya njaa! Hata kama mwalimu ukiingia unagundua kuwa humu darasani wanaonisikiliza ni wachache wengine wanakuwa wameshabanwa na njaa na hivo kumbu kumbu inakuwa imepungua sana” alisema mwalimu Mwakifuna wa shule ya msingi Kakuni
Alifafanua kuwa licha ya kuwa uji utapunguza utoro mashuleni lakini pia utajenga mazingira bora ya kujifunza katika vipindi vya mchana na kujenga hamasa ya kuanza shule  kwa watoto wanaokwepa kuanza shule katika jamii.
Walimu hao walimuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu siku moja afike shuleni hapo kushuhudia namna wanafunzi wanavyoufurahia uji wakiwa shuleni na kushirikiana nao japo siku moja.
MWISHO.
Na Willy Sumia, Katavi
ASKARI wa jeshi la mgambo katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda Mkoa mpya wa Katavi wamenusurika kipigo kutoka kwa wafanya biashara wa masoko matatu tofauti  kufuatia kupandishwa kwa ushuru wa masoko hayo.
Vurugu zilianza mara baada ya askari hao kufika katika masoko yaliyoko mjini hapa  kukusanya ushuru ambao umegomewa na wafanya biashara hao kwa madai ya ongezeko kubwa la ushuru kuliko hali halisi ya kipato cha biashara zao sokono hapo.
Tukio hilo limetokea jana katika muda tofauti mara baada ya askari wa mgambo hao pamoja na wakala wa kukusanya ushuru wa masoko ya mji kufika katika maeneo yao kwa lengo la kukusanya ushuru ambao unapingwa na wafanya biashara hao kwa kile kinachodaiwa na wafanya biashara hao kuwa ni ongezeko kubwa la ushuru.
Akizungumzia matukio hayo katibu wa wafanyabiashara wa Mji huo Amani Mahela ametoa wito kwa Mkurugenzi wa Mji kufika kwenye masoko hayo na kufanya mazungumzo na wafanya biashara badala ya utaratibu anaoutumia sasa wa kutoa matangazo kwenye vyombo vya habari akiwataka walipe ongezeko hilo la ushuru kabla ya kufanya mazungumzo nao.
Diwani wa kata ya Kashaulili John Matongo  amesema kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji ameitisha kikao cha Madiwani wa kata tatu na viongozi wa wafanyabishara toka katika masoko yaliyo na mgogoro wa
ushuru  ili kujadili namna ya kutatua tatizo hilo
Halmashauri ya Mji wa Mpanda imebandika matangazo katika masoko hayo matatu akiwaeleza wafanya biashara kuwa wale ambao hawatakuwa tayari
kulipa ongezeko la ushuru waondoke katika maeneo ya masoko hayo Kaimu mkurugenzi wa Mji Mpanda Josefu Mchina aliwaeleza waandishi wa habari ofisini kwake kuwa ushuru ni suala la kisheria na huwa lina
mchakato wake katika kuuanzisha, kuongeza  au kuupunguza kabla ya kuanza utekelezaji hivyo ushuru unaolalamikiwa ni halali kisheria na pia umezingatia hali halisi ya bishara na mahitaji ya maendeleo katika
masoko na mji kwa ujumla.


Na WALTER  Mguluchuma
Mpanda
Madiwani wa chama cha mapinduzi (CCM) katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda wamesusia sherehe ya kumuaga Mkurugenzi wao kutokana na itikadi za siasa
Tukio hilo limetokea hapo jana ambapo Halmashauri ya Mji wa Mpanda iliandaa sherehe ya kumuaga Mkurugenzi wao ambaye alikuwa anastaafu utumishi Bwana Henry Haule
Sherehe za kumuaga Mkurugenzi huyo zilifanyika katika Ukumbi wa Katavi Resort mali ya Abrahamu Kombe ambaye anadaiwa na Madiwani hao kuwa aliwasariti kwenye uchaguzi Mkuu na kuisaidia Chadema
Madiwani hao baada ya kupata taarifa za sherehe za kumuaga mkurugenzi wao kweny Ukumbi wa Katavi walianza kupinga na kutaka sherehe hizo zifanyike kwenye Ukumbi wa Idara ya Mji ambao hata hivyo ulikuwa umeandaliwa kwa shughuli za Mkutano wa wawekezaji na Waziri Mkuu
Sherehe hizo zilianza huku ndani ya Ukumbi kukiwa na madiwani wawili wa kata za kashaulili na makanyagio ambao ni wa Chadema
Wakati sherehe zikiendelea madiwani hao waliendelea na kikao chao nje ya Ukumbi huo kwa lengo la kuendelea na msimamo wao huo Hata hivyo wakati sherehe zikienda mwisho waliingia madiwani wawili wa Chama hicho ambao ni Enock Gwambasa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji huo pamoja na diwani Willy Mbogo
Walipo hojiwa Madiwani hao sababu iliowafanya waingie mwishoni mwa sherehe walisema tulikuwa na mvutano na wenzetu ila sisi tumeamua kuingia kwenye sherehe
Na Peti Siyame umbawanga
MWENDESHA  pikipiki  aitwaye Ramadhani  Sood (25)  amefariki  dunia baada ya kugongwa na  gari  katika kijiji cha  Makanyagio  katika barabara  ya Mpanda –Shanwe iliyopo  wilayani Mpanda katika mkoa wa Rukwa.
Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Isuto Mantage  alisema  kuwa  ajali hiyo  ililihusisha   basi la abiria aina  ya scania  yenye  namba  za usajili  T 519  ACV iliyokuwa ikiendeshwa  na dereva  aitwaye Masoud
Musa (32) mkazi wa  Makanyagio  mjini Mpanda
Kwa mujibu wa Kamanda huyo wa Polisi  gari  hilo  la  abiria lilimgonga  mwendesha pikipiki  Ramadhani  mkazi wa Makanyagio aliyekuwa  akiendesha pikipiki aina ya  Honda  yenye  namba  za
usajiri  T. 612 ANT na kumsababishia  majeraha  makubwa .
“Ramadhani  aliyekuwa  mahututi  ambapo  alikuwa na  majeraha makubwa mwilini  alifariki  muda mfupi  baada ya kufikishwa  kwenye  hospitali  ya  wilaya ya Mpanda  kwa matibabu” alisema  Mantage .
Kamanda Mantage  alisema kuwa  chanjo  cha  ajali  hiyo  bado hakijajulikana  na kwamba  dereva  wa  gari  alikamatwa  na atafikishwa  mahakamani  mara  baada ya  uchunguzi  wa awali kukamilika