Tuesday, November 27, 2012

INVESTMENT PROFILE KATAVI REGION




Pamoja na jeshi la polisi mkoa wa Iringa kuwabana madereva wanaoruhusu abiria wao kuning'inia katika magari ila bado wanaendelea kutenda kosa sasa ni nani wa kumuwajibisha mwenzake? hili ni eneo la posta mjini Iringa, ni kazi nzuri ya www.francisgodwin.blogspot.com




Monday, November 26, 2012

CHOZI HILI LINAMAANISHA ..........

BI REHEMA MOHAMMED AKITANGAZA KUHAMA CHADEMA NA KUHAMIA CCM KATIKA MKUTANO WA CCM ARUSHA MWISHONI MWA WIKI.....



Rehema Mohammed alikuwa Diwani Chadema kabla ya kuhamia CCM kufuatia mkutano wa CCM ulioongozwa na katibu mkuu wa CCM Taifa, Abdalahman Kinana.

Sunday, November 25, 2012

MKOA WA KATAVI WAZINDULIWA RASMI

Dkt.Bilal Azindua Mkoa Wa Katavi

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungao ya Tanzania Dkt Mohamed Gharib Bilal akizindua rasmi mkoa wa Katavi kwa kuweka jiwe la msingi katika kilima cha kijiji cha Kabungu kwa ajili ya kujenga kituo cha kumbukumbu ya historia ya mkoa wa Katavi, kulia kwake ni mkuu wa mkoa hu Dr Rajabu M. Rutengwe akishuhudia jana Novemba 25, 2012
Mkuu wa wilaya ya mpanda, Paza Tusamale Mwamlima akimkaribisha makamu wa Rais wilayani kwake katika hafla ya uzinduzi wa mkoa wa Katavi na Tathmini ya uwekezaji kwa mwaka mmoja.


Kijiji Cha Kabungu ndipo palipozaliwa Wilaya ya Mpanda Mwaka 1947 na Boma la mtawala wa kwanza wa kikoloni Mpanda lilijengwa hapo
 
Makamu wa Rais Akizungumza na wafanyakazi wa benki ya NMB wakati alipotembelea katika banda hilo leo njini Mpanda Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Rutengwe.
 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mizengo Pinda akizungumza na wana Katavi wakati wa uzinduzi wa mkoa wa mpya wa Katavi  kwenye viwanja vya Kashaulili mjini Mpanda leo.
Wananchi wa Mkoa wa Katavi wakishangilia
Baada ya uwekaji wa jiwe la msingi kijijini Kabungu, Makamu wa Rais alirejea mjini mpanda katika viwanja vya Kashaulili ambapo kumefanyika shughuli mbalimbali za  uzinduzi rasmi wa mkoa huo na hotuba mbalimbali zikiendana na sherehe za  ngoma za makabila mbalimbali  ya asili ya mkoa wa Katavi


 Makamuwa Rais Dkt. Gharib Bilal akikaribishwa na mkuu wa wilaya ya Mpanda Mh. Paza Tusamale Mwamlima huku akipungia mkono wananchi waliofika kumlaki na kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi katika kijiji cha Kabungu nje kidogo ya mji wa Mpanda.
 Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kabungu wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi kuzindua mkoa wa Katavi, kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajab Rutengwe na kutoka kulia ni Mke wa Makamu wa Rais Mama Zakia Bilal na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi Bw. Abdallah Mselem Said
 Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Uwezeshaji na Uwekezaji Dkt Mary Nagu, Mke wa Makamu wa Rais mama Zakia Bilal na Mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda wakiimba wimbo mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Kashaulili mjini Mpanda tayari kwa Sherehe za uzinduzi wa mkoa wa Katavi
 
Baadhi ya wawekezaji waliohudhuria katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye viwanja vya Kashaulili.
 
Mkuu wa mkoa wa Katavi akiongea na kukaribisha viongozi mbalimbali kutoka salam zao kutoka mikoa waliyotoka na wizara mbalimbali.
 
Waziri wa Ardhi na makazi Goodluck Ole Medeye akizungumza na wana Katavi na kuwaasa mambo mbalimbali kuhusu ardhi yao hasa katika suala zima la uwekezaji, ambapo amewaambia wasiuze ardhi bali waingie ubia na wawekezaji ili kunufaisha vizazi vyao pia.
 
Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda akiwasalimia wananchi wa Katavi na kuwapongeza kwa kupata mkoa mpya wa Katavi.
 
Mama Aisha Bilal akisalimia wananchi wa katavi katika sherehe hizo.
 
Kwaya ya Vijana ya Moravian mjini Mpanda wakitumbuiza katika uzinduai huo uliofanyika kwenye viwanja vya Kashaulili mjini Mpanda.
 
Martha Mbogo mwimbaji wa kundi la Katavi Curture Group akiimba wakati kundi hilo lilipokuwa likitumbuiza katika uzinduzi huo mjini Mpanda.

 Watoto Daniel Ntwangile na Christina Benedicto wakitunzwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda mara baada ya kuimba na kucheza vizuri na Kwaya ya Vijana Moravian Mjini Mpanda wanaofuatia ni Waziri wa Uwezeshaji na Uwekezaji Dkt Mary Nagu, Mke wa Makamu wa Rais mama Zakia Bilal na Mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda wakijiandaa na wao kuwatunza

MILANGO YA KATAVI YAFUNGUKA .....

DKT GHARIB BILAL AZINDUA UWANJA NDEGE WA MPANDA NA KONGAMANO LA TATHMINI YA UWEKEZAJI UKANDA WA ZIWA TANGANYIKA

 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. Gharib Bilal na Mkewe mama Aisha Bilal wakishuka kwebye ndege mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda mkoani Katavi kwa ajili ya uzinduzi wa mkoa mpya wa Katavi unaofanyika mjini mpanda kesho, Makamu wa Rais pia amezinddua uwanja wa ndege wa Mpanda na kuzindua Kongamano la Tathimini ya Mkutano wa Uwekezaji Ukanda wa Ziwa Tanganyika  uliofanyika Oktoba 17 mwaka jana na kushirikisha mikoa mitatu ya Rukwa, Kigoma a kufanyika mjini mpanda ambapo  sasyamekuwa makao makuu ya Mkoa wa Katavi.
 
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akisalimiana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda, kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Rutengwe na katikati ni mama Tunu Pinda.
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal kushoto akijadiliana jambo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati wa Kongamano la kutathmini Mafanikio na Changamoto baada ya mkutano wa Uwekezaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika Kigoma na Rukwa uliofanyika Oktoba 17 mwaka jana mjini Mpanda
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza katika uzinduzi wa Uwanja wa ndege wa Mpanda, kshoto ni Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal na kulia ni mama Zakia Bilal.
 
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akizungumza wakati wa uzinduzi wa  uwanja wa ndege wa Mpanda mkoani Katavi leo mchana.
 
Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar Chambo akitoa taarifa ya ujenzi wa uwanja huo kwa Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal wakati wa uzinduzi mjini mpanda leo.
 
Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizeba akimkaribisha Makamu wa Rais ili kuongea na wananchi wakati wa uzinduzi wa uwanja huo mjini Mpanda leo
 
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa uwanja wa ndege wa Mpanda baada  ya kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo, kulia ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mizengo Pinda na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizeba, kushoto ni Mama Zakia Bilal mke wa Makamu wa Rais.

 Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye, Dkt. Mary Nagu Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji Ofisi ya Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda Mke wa Waziri Mkuu na Mama Zakia Gharib Bilal Mke wa Makamu wa Rais wakiwa katika uzinduzi huo 
Makamu wa Rais akisalimiana na Mary Nagu Waziri wa Uwekezaji na Uwekezaji mara baada ya kuwasili mjini Mpanda leo Katikati ni Mwenyekiti wa CCM Katavi Mselem na kutoka kulia ni Mbunge wa Mpanda mjini CHADEMA Mh.Said Arfi na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt Charles Tizeba.
 
Makamu wa Rais Dkt Gharib Bilal akivishwa skafu na vijana wa chipukizi mjini Mpanda mara baada ya kuwasili mkoani Katavi leo.
 
Makamu wa Rais akisalimiana akipungia mkono wananchi waliofika kumlaki kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda mkoani Katavi leo, kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Katavi Dkt Rajab Rutengwe na kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa Bw. Mselem.

MILANGO YA KATAVI YAFUNGUKA .....

DKT GHARIB BILAL AZINDUA UWANJA NDEGE WA MPANDA NA KONGAMANO LA TATHMINI YA UWEKEZAJI UKANDA WA ZIWA TANGANYIKA

 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. Gharib Bilal na Mkewe mama Aisha Bilal wakishuka kwebye ndege mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda mkoani Katavi kwa ajili ya uzinduzi wa mkoa mpya wa Katavi unaofanyika mjini mpanda kesho, Makamu wa Rais pia amezinddua uwanja wa ndege wa Mpanda na kuzindua Kongamano la Tathimini ya Mkutano wa Uwekezaji Ukanda wa Ziwa Tanganyika  uliofanyika Oktoba 17 mwaka jana na kushirikisha mikoa mitatu ya Rukwa, Kigoma a kufanyika mjini mpanda ambapo  sasyamekuwa makao makuu ya Mkoa wa Katavi.
 
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akisalimiana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda, kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Rutengwe na katikati ni mama Tunu Pinda.
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal kushoto akijadiliana jambo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati wa Kongamano la kutathmini Mafanikio na Changamoto baada ya mkutano wa Uwekezaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika Kigoma na Rukwa uliofanyika Oktoba 17 mwaka jana mjini Mpanda
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza katika uzinduzi wa Uwanja wa ndege wa Mpanda, kshoto ni Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal na kulia ni mama Zakia Bilal.
 
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akizungumza wakati wa uzinduzi wa  uwanja wa ndege wa Mpanda mkoani Katavi leo mchana.
 
Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar Chambo akitoa taarifa ya ujenzi wa uwanja huo kwa Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal wakati wa uzinduzi mjini mpanda leo.
 
Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizeba akimkaribisha Makamu wa Rais ili kuongea na wananchi wakati wa uzinduzi wa uwanja huo mjini Mpanda leo
 
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa uwanja wa ndege wa Mpanda baada  ya kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo, kulia ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mizengo Pinda na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizeba, kushoto ni Mama Zakia Bilal mke wa Makamu wa Rais.

 Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye, Dkt. Mary Nagu Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji Ofisi ya Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda Mke wa Waziri Mkuu na Mama Zakia Gharib Bilal Mke wa Makamu wa Rais wakiwa katika uzinduzi huo 
Makamu wa Rais akisalimiana na Mary Nagu Waziri wa Uwekezaji na Uwekezaji mara baada ya kuwasili mjini Mpanda leo Katikati ni Mwenyekiti wa CCM Katavi Mselem na kutoka kulia ni Mbunge wa Mpanda mjini CHADEMA Mh.Said Arfi na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt Charles Tizeba.
 
Makamu wa Rais Dkt Gharib Bilal akivishwa skafu na vijana wa chipukizi mjini Mpanda mara baada ya kuwasili mkoani Katavi leo.
 
Makamu wa Rais akisalimiana akipungia mkono wananchi waliofika kumlaki kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda mkoani Katavi leo, kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Katavi Dkt Rajab Rutengwe na kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa Bw. Mselem.

NHC KATAVI KUMEKUCHAAA.....

Jiwe la msingi Ilembo NHC Mpanda

 Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu akiwa sambamba na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye wakikagua mojawapo ya nyumba za mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Ilembo, Mpanda Katavi jana
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mkurugenzi wa Utawala na Uendeshaji wa Mikoa, Raymond Mndolwa huku Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye wakishuhudia kwenye uzinduzi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Ilembo, Mpanda Katavi jana
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk mohammed Gharib Bilal, akizindua ujenzi wa nyumba za gharama nafuu NHC Ilembo huku Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye wakishuhudia kwenye uzinduzi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Ilembo, Mpanda Katavi jana
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk mohammed Gharib Bilal, akizindua ujenzi wa nyumba za gharama nafuu NHC Ilembo huku Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye wakishuhudia kwenye uzinduzi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Ilembo, Mpanda Katavi jana

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk mohammed Gharib Bilal, akipeana mkono na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye  kwenye uzinduzi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Ilembo, Mpanda Katavi jana. Picha zote za kwa hisani ya SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA  
Makamu wa Rais Dkt. Gharib Bilal akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Mh. Venance Mwamoto wakati wa mapokezi hayo, kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajab Rutengwe.

Shirika la Nyumba lazindua Ujenzi nyumba za gharama nafuu Katavi

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja Mawasiliano wa Shirika la Nyumba la Taifa, Yahya Charahani kwenye maonyesho yanayoshirikisha taasisi, asasi na vitengo mbalimbali vya umma na watu binafsi mjini Mpanda jana. Maonyesho hayo ya wiki moja ni sehemu ya uzinduzi rasmi wa mkoa wa Katavi unaofanyika rasmi kesho.
 Ujenzi wa Majengo ya nyumba za gharama nafuu za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilembo Mpanda mkoani Katavi yakiwa katika hatua za awali za ujenzi wake ambao baada ya kukamilika zitajengwa nyumba 94 za kuishi kwaajili ya watu wa kipato cha chini.
 Ujenzi wa Majengo ya nyumba za gharama nafuu za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilembo Mpanda mkoani Katavi yakiwa katika hatua za awali za ujenzi wake ambao baada ya kukamilika zitajengwa nyumba 94 za kuishi kwaajili ya watu wa kipato cha chini.
Mkurugenzi wa Utawala na Uendeshaji wa Mikoa wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Raymond Mndolwa akieleza jambo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemiah Kyando Mchechu kwenye Ujenzi wa Majengo ya nyumba za gharama nafuu za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilembo Mpanda mkoani Katavi yakiwa katika hatua za awali za ujenzi wake ambao baada ya kukamilika zitajengwa nyumba 94 za kuishi kwaajili ya watu wa kipato cha chini.
Meneja wa NHC Mbeya ambaye pia ni Mhandisi Msimamizi wa Mradi wa Ujenzi wa Majengo ya nyumba za gharama nafuu za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilembo Mpanda mkoani Katavi, Malissa (kushoto) akizungumza na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC, Geofrey Msella wakati huku Mkurugenzi Mkuu Nehemia Kyando Mchechu (katikati) akisikiliza .

Jiwe la Msingi la nyumba za gharama nafuu za NHC Ilembo, Mpanda mkoani Katavi.