Friday, October 26, 2012

WALOTEKA BASI LA SUMRY KATAVI MBARONI

Basi mojawapo la kampuni ya Sumry linalotoa huduma katika mikoa ya Rukwa na Katavi

WATUHUMIWA wa utekaji wa basi la sumry katika tukio la wiki iliyopita wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Katavi wakiwamo wakimbizi kutoka nchi jirani ya Burundi.
Jeshi la polisi mkoani Katavi limetoa taarifa kuwa jumla ya watuhumiwa kumi na mbili wamekamatwa kwa tuhuma za kuliteka basi la kampuni ya usafishaji ya Sumry High Class lenye namba T107BHT wiki iliyopita katika kijiji cha Magamba wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi kilometa nne toka Mpanda mjini.
Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Katavi Joseph Myovella alisema Oktoba 26, 2012 kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa wakiuza simu za mkononi zilizochukuliwa katika tukio la utekaji wa basi la Sumry ambapo baada ya kuhojiwa walikiri na kuwataja waliokuwa nao.
Alisema katika upelelezi kwa kutumia tekionolojia ya mawasiliano mtambo maalum uliweza kubaini kuwapo matumizi ya simu zilizochukuliwa katika eneo la mkoa wa Katavi ndipo waliweza kufuatilia vipimo na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wakiziuza simu hizo licha ya kuwa zilikuwa zimebadilishwa laini zake.
“Kwakutumia tekinolojia tumeweza kuzisoma simu zilizochukuliwa katika tukio hilo zikisomeka katika mtandao kuwa zinatumika katika eneo la mkoa wetu wa Katavi tukaanza kuzifuatilia hadi tukafanikiwa kuwakamata watuhumiwa moja baada ya wmingine hadi kufikia idadi ya kumi na mbili” alisema Myovella.
Alifafanua kuwa hivi sasa bado jeshi lake linaendelea na uchunguzi zaidi na hivyo majina ya watuhumiwa yatawekwa wazi mara baada ya kukamilika upelelezi ambapo silaha zilizotumika zilikuwa ni mapanga, nondo na fimbo.
Jeshi hilo lilitoa wito kwa wananchi kutokununua simu zinazouzwa mitaani kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kuingia kwenye mkubo wa utekaji basi kwa sababu sasa hivi tekinolojia inayotumika inaonesha mtumiaji wa simu iliyochukuliwa katika utekaji wa basin a mahali alipo mtumiaji kiasi kwamba endapo mtu atanunua simu hiyo atakamatwa na kwa utaratibu wa upelelezi atajumuishwa katika orodha ya watuhumiwa.
Alisema kati ya watuhumiwa hao kumi ni Watanzania na wawili ni Raia wan chi jirani ya Burundi wanaoishi kama wakimbizi katika makazi ya wakimbizi ya Katumba.

Moja ya mabasi ya kampuni ya Sumry likiwa tayari kuanza safari zake.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Watu wanane wenye silaha zikiwamo za jadi wameliteka basi la abiria la Sumry baada ya kuweka kizuizi cha magogo na mawe katika msitu wa Msaginya kijijini Magamba wilayani Mlele katika Mkoa wa Katavi katika barabara kuu ya Sumbawanga – Mpanda.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, uhalifu huo ulifanyika saa sita usiku wa kuamkia jana ambapo gari hilo lenye namba za usajili T107 BHT lililokuwa likisafiri kwenda mjini Mpanda likitokea mjini Sumbawanga.

Akifafanua, alisema basi hilo lilipofika eneo hilo lenye mteremko na kona kali ambalo lipo kilometa 15 kutoka Mpanda Mjini, lilikumbana na vizuizi vya mawe na magogo ndipo lilipolazimika kusimama ghafla.

Inadaiwa kuwa ndipo walipojitokeza watu wanane waliokuwa mafichoni wakiwa na silaha za jadi zikiwamo mapanga, nondo, mawe na visu na kuwalazimisha abiria wote kushuka ambapo walipekuliwa na kuporwa simu za mkononi 15 na kiwango kikubwa cha fedha, thamani halisi haijafahamika.

Kwa mujibu wa taarifa nyingine kutoka eneo hilo zinadai kuwa baadhi ya abiria walidhalilishwa kwa kuvuliwa nguo maungoni mwao wakati walipokuwa wakipekuliwa na watu hao ambao kila aliyeshuka garini, alilazimishwa kukabidhi chochote alichokuwa nacho kisha walilazimishwa kulala chini.

Kwa mujibu wa mtoa habari kutoka eneo la tukio ambaye hakuwa tayari jina lake liandikwe alisema baadhi ya abiria walikumbwa na adha hiyo walikuwa wanawake na watoto ambapo mmoja wao alikuwa mtawa wa kike ambaye inadaiwa alikuwa akisafiri kwenda Mwanza.
Hata hivyo, Kamanda huyo alikanusha abiria yeyote aliyevuliwa nguo ila walilazimishwa kulala chini baada ya kuamriwa kushuka garini na gari hilo baadaye liliwafikisha abiria wake hadi Mpanda Mjini.
Kwa mujibu wa Kidavashari kutokana na tafrani hiyo, watu wanane wakiwamo dereva wa gari, Said Chile na utingo wake ambaye jina lake halikufahamika mara moja walijeruhiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya mjini Mpanda kwa matibabu.

Kamanda alisema Polisi inafanya msako mkali kuwasaka watu hao ambao hadi sasa hawajapatikana na haijulikani walikojificha kwani walikimbia kusikojulikana baada ya kufanya uhalifu huo. (Na Ziro99 blog)

Wednesday, October 24, 2012

CCM INAKERWA NA RUSHWA NDANI YAKE

MWENYEKITI WA CCM TAIFA RAIS KIKWETE AWAONYA UVCCM

 


Meza kuu ikiwa na bango lenye ujumbe mzito kutoka katika nukuu za Mheshimiwa Rais na Mwenyekiti  wa Chama Cha Mapinduzi, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Katibu wa Halmashauri kuu Taifa (NEC) Siasa na Mahusiano ya Kimataifa Mhe. January Makamba akisalimiana na wageni waalikwa kutoka katika jumuiya za vijana vyama mbalimbali kusini na afrika ya kati.

Makatibu wa halmashauri kuu (NEC) kutoka Kulia Uchumi na Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba, Siasa na Mahusiano ya Kimataifa Mhe. January Makamba na Itikadi na Uenezi Ndugu. Nape Nnauye.

Vijana wa Chama Cha Mapinduzi ambao pia ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa nane wa Umoja wa Vijana wa CCM.

Vijana mbalimbali ambao wanawakilisha mikoa wakiwa na mabango ambayo yanaonyesha Mikoa wanayotoka.

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi akisalimiana na viongozi mbalimbali wa chama hicho ambao walimpokea akiwa anaingia katika ukumbi wa mkutano wa nane wa vijana wa chama cha mapinduzi.

Kaimu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Ndugu Benno Malisa  akimueleza jambo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Jakaya Kikwete katika Mkutano huo.

MWENYEKITI CCM TAIFA AWAPA UKWELI UVCCM

Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wanaendelea na Mkutano Mkuu wa Taifa ambapo wanatarajia kuchagua viongozi mbalimbali katika ngazi ya Taifa ya jumuiya hiyo, ambapo jumla ya wagombea 133 wamejitokeza kuwania nafasi hizo ambazo ni nafasi ya Mwnyekiti, Makamo Mwenyekiti, Wajumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC) kupitia jumuiya ya vijana, ambapo nafasi (6) zinatoka bara na (4) zinatoka Tanzania Visiwani, nafasi nyingine ni Baraza Kuu Taifa, Viti 5 Bara na 5 Zanzibarm Nafasi ya Uwakilishi WAZAZI Taifa na mwisho ni nafasi ya uwakilishi UWT Taifa.

Mkutano Mkuu huo wa UVCCM umefunguliwa Na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ambae pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, ulianza Rasmi, saa 4 asubuhi, ambapo Mhe. Rais alifanya ufunguzi kwa Hotuba makini, iliyoeleza mambo makubwa na ya msingi juu ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM).

Mhe. Jakaya Kikwete alisisitiza na kukumbusha juu ya Lengo kuu na Dhumuni Kuu la Chama Cha Mapinduzi lililotajwa katika katiba yake Ibara ya 5 ambayo inaeleza bayana kuwa ni kushinda uchaguzi na kushika dola.

Lakini pia akaeleza kuwa CCM kinategemea jumuiya yake hiyo kufanya kazi ya siasa miongoni mwa vijana wa Tanzania na kushawishi wakubali kuwa wanachama na wapenzi wa CCM. Akasisitiza kuwa matumaini makubwa ya msingi kuliko yote ya Chama Cha Mapinduzi ni kuona jumuiya yake hiyo inakuwa MKOMBOZI wa vijana.

 Mhe. Kikwete akawataka wahakikishe kuwa wanapata Viongozi ambaowataongoza vyema, watakaoongoza juhudi za kuendeleza, kutetea na kulinda maslahi ya CCM. Viongozi wanaoijua na kuipenda jumuiya ya Vijana.

UBABE WA VIONGOZI WA KISIASA MATOKEO HAYA HAPA

Nyumba ya walinzi wa shamba la Efatha Ministry lililoteketezwa kwa moto na wanakijiji wenye hasira katika kijiji cha Sikaungu wilaya ya Sumbawanga mkoani  Rukwa.

Masalia ya moja ya nyumba iliyoteketezwa kabisa kwa moto kufuatia vurugu zilizotokana na mgogoro wa ardhi

Masalia ya matrekta yaliyoteketezwa na wanakijiji kwa moto mali ya Efatha Ministry

Katibu mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Jobu Masami akizungumza na makamanda mjini Mpanda. PICHA NA MALASO EARNEST

 Katibu Mkuu wa wizara ya ulinzi na JKT Jobu Masami akisalimiana na makamanda wanaoendesha zoezi la kusafirisha mahindi kutoka mikoa ya Rukwa na Katavi mara baada ya kuwasili mjini Mpanda hivi karibuni. PICHA