Sunday, April 15, 2012

BREAKING NEWS - KATAVI ya TANZANIA

TTCL WON A 6.7 US DOLLARS CONTRACT TO SUPPLY 1.244 GIGABYTES OF INTERNET BANDWIDTH TO RWANDA FOR 10 YEARS

Kwsho tutawaletea changamoto za TTCL hapa mjini Mpanda  



TTCL’s CEO Mr. Said Amir Said (left) and the Head of Information and Communication Technology department at the Rwanda Development Board (RDB) Patrick Nyirishema signing the contract.
TTCL’s Chief Marketing and Sales Officer Mr. Ernest Nangi (Left), TTCL’s Company Secretary Mrs. Gilder Kibola and Head Products Development Mr. Ernest Isaya.
TTCL’s Chief Executive Officer Mr. Said Amir Said speaking with Journalist in Rwanda after signings business Contract.

MASHIMO HAYA KWELI HALMASHAURI WAPO????

AFISA MAZINGIRA AMEUGUA TANGU LINI????? 







APRIL 18, 2012


MWANAHABARI SYROSE BHANJI AULA UBUNGE BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI

Shy-Rose Bhanji
Mwandishi wa habari mwandamizi wa siku nyingi, Shyrose Bhanji amekuwa miongoni mwa wagombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki ambao waliibuka kidedea katika uchaguzi uliofanyika jana mjini Dodoma.

Katika uchaguzi huo wagombea tisa kati ya 32 waliowania nafasi hiyo, walifamikiwa kuibuka kidedea na kupata tiketi ya kuwakilisha Tanzania katika bunge hilo.


Wagombea walioshinda nafasi kwa wanaume Tanzania Bara na idadi ya kura kwenye mabano ni Adam Kimbisa (210), Benard Murunya (135) na Makongoro Nyerere (123), na walioanguka ni Lifa Chipaka (8), William Melecela (42), Dk. Evans Rweikiza.


Upande wa wanawake, walioshinda ni Angela Kizigha (166), Shyrose Bhanji (120), ambao ndiyo watakaiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki, na walioshindwa ni Janeth Mbene, Fancy Nkuhi, Janeth Mmari na Dk. Godbertha Kinyondo.

Kundi la wagombea kutoka Zanzibar, walioshinda ni Abdalah Ali Mwinyi (237), Maria Yahya Ussi (91). Walioanguka ni Ahmada Hamad Khatib, Dk. Haji Mwita Haji, Khamis Jabir Makame, Dk. Said Gharib Bilal na Zubeir Ali Maulid.

Kwa upande wa kundi la upinzani, walioshinda ni Nderakindo Kessy (NCCR-Mageuzi) na Twaha Issa Taslima (CUF). Mgombea wa CHADEMA Antony Komu aliangushwa vibaya kwenye kinyang’anyiro hicho. Wengine walioshindwa ni Dk. Fortunatus Masha (UDP), Anthony Komu (CHADEMA), Juju Danda (NCCR-MAGEUZI), Michael Mrindoko (TLP), Mwaiseje Polisya (NCCR-MAGEUZI).

Wabunge wa CHADEMA ambao awali walitangaza kususia uchaguzi huo, walishiriki ikiwa ni pamoja na kusimamisha mgombea wake Anton Komu, ambaye alibwagwa vibaya.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bunge, Freeman Mbowe, alisema hawatashiriki uchaguzi kwa madai ya kutokuwa huru na haki.


Mbowe, ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, alisema wabunge wa chama hicho watatoka nje na hawatakuwa tayari kuwasikiliza wagombea wala kupiga kura na kwamba CHADEMA kushiriki uchaguzi huo ni kutowatendea haki Watanzania, lakini katika hali ya kushangaza wabunge hao wakiongozwa na Mbowe walishiriki uchaguzi huo na hawakutoka ukumbini.

Awali, CHADEMA lilitaka kupewa nafasi moja kwa ajili ya chama hicho pekee badala ya kushindaniwa na wapinzani wote kama kanuni inavyoelekeza.

‘Sisi kama Chadema hatutashiriki katika uchaguzi huo wala hatutashiriki kupiga kura wala kusikiliza tutatoka nje tuache waendelee,’ alisema.

Hata hivyo, Naibu Spika Job Ndugai, alisema hoja hiyo ya CHADEMA haina msingi na kwamba, nafasi mbili walizopewa wapinzani zitahusisha vyama vyote vya upinzani.
Awali, wagombea waliingia katika nafasi hiyo ni Bernard Murunya, Adam Kimbisa, Makongoro Nyerere, Mrisho Gambo, Siraju Kaboyonga, William Malecela, Dk. Evans Rweikiza, Elibariki Kingu na Dk. Edmund Mndolwa wote kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM). Pia, yumo John Lifa-Chipaka wa TADEA.
Kwa upande wa wanawake mchuano kuwania nafasi hiyo ulikuwa kwa Engela Kizigha, Fancy Nkuhi, Dk. Godbertha Kinyondo, Janet Mmari, Janeth Mbene, Mariam Ussi Yahya na Sebtuu Mohamed Nassor, Shyrose Bhanji, Sofia Ali Rijaal wote kutoka CCM wakati mgombea kutoka upinzani ni Rose Mwalusamba (CUF).
Waliowania nafasi ya kuwakilisha Zanzibar katika Bunge la Afrika Mashariki walikuwa ni Abdullah Ali Hassan Mwinyi, Dk. Ahmada Hamad Khatib, Dk. Haji Mwita Haji, Khamis Jabir Makame, Dk. Said Gharib Bilal na Zubeir Ali Maulid wote kutoka CCM.


Kwa upande wa wagombea wa vyama vya upinzani, walikuwemo Dk. Fortunatus Masha (UDP), Anthony Komu (CHADEMA), Juju Danda (NCCR-MAGEUZI), Micah Mrindoko (TLP), Mwaiseje Polisya (NCCR-MAGEUZI), Nderakindo Kessy na Twaha Issa Taslima (CUF).
Adamu Kimbisa

Angela Kizigha

Makongoro Nyerere(picha na habari kwa hisani Nkoromo Daily Blog)

 NG'OMBE WANAVOIVAMIA KATAVI KWA SPEED

SASA BASI - RC KATAVI

 PICHA JUU: Lori lenye namba T847ANJ na Teller lake lenye namba T122AHH likiwa na ng'ombe katika kituo cha polisi Mpanda baada ya kukamatwa Aprili 16, 2012.

Mawaziri wamjibu Mbowe

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman
 Mbowe, akizungumza na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, wakati 
wa kumbukumbu ya hayati Edward Moringe Sokoine, nje ya Kigango cha 
Sokoine, Parokia ya Dakawa mjini Morogoro juzi. Picha na Merina Robert.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akizungumza na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, wakati wa kumbukumbu ya hayati Edward Moringe Sokoine, nje ya Kigango cha Sokoine, Parokia ya Dakawa mjini Morogoro juzi. Picha na Merina Robert.
Dk. Nagu, Ole Medeye wamtaka atoe ushahidi Magufuli ataka akamuulize Waziri Mkuu SIKU moja baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, kumwambia Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwamba baadhi ya mawaziri wanawatisha wananchi ili wasiwachague wagombea wa upinzani, mawaziri hao wameamua kujibu mapigo. Wakizungumza kwa nyakati tofauti mjini hapa jana, mawaziri hao wameonyesha kutoridhishwa na kauli ya Mbowe, kwa kuwa hakuna ushahidi dhidi ya maneno yaliyosemwa. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, alisema hakumbuki alichozungumza wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, uliomalizika hivi karibuni. “Sikumbuki kama alichosema Mbowe ni sahihi, kwa sababu kule tulikuwa kwenye kampeni, kila mmoja alikuwa akitumia silaha zake. “Katika kipindi cha miaka 10 ambayo nilikuwa Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Arusha, Jimbo la Arumeru Mashariki lilikuwa kwenye himaya yangu, ndiyo maana nilikwenda kupiga kampeni kukisaidia chama changu. “Pamoja na hayo, Mbowe wakati mwingine aachane na maneno ya kwenye kampeni kwa sababu katika kipindi hicho kunakuwa na mambo mengi sana na kama mtu ukitaka kufuata mambo ya kampeni unaweza kusababisha mambo mengine yasiyofaa,” alisema Dk. Nagu. Wakati Dk. Nagu akisema hayo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck ole Medeye, ambaye ni mmoja wa walioshutumiwa na Mbowe, alisema hakumbuki na wala hajui kama alisema maneno hayo. Kutokana na hali hiyo, alimtaka Mbowe awasilishe bungeni ushahidi wa alichokisema ili kuondoa utata. “Hilo suala silikumbuki kwa sababu ninachojua hayo mambo yaliripotiwa na magazeti tu. Lakini kama Mbowe ana uhakika na anachokisema, alete bungeni mikanda ya mikutano hiyo, ikiwa ni pamoja na ya upande wake ili ukweli ujulikane,” alisema ole Medeye. Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, yeye binafsi amekuwa akifanya kazi bila upendeleo, ikiwa ni pamoja na kutembelea majimbo yote, yakiwamo yanayoongozwa na vyama vya upinzani. Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, aling’aka na kukataa kuzungumzia tuhuma hizo. Badala yake alitaka akaulizwe Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwa vile ndiye aliyeulizwa na Mbowe. Juzi wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Mbowe aliwashitaki mawaziri hao, kwamba wanawatisha wananchi ili wasichague wapinzani. Akizungumza wakati akiuliza swali lake, Mbowe alisema, Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe pole kwa misiba iliyolipata taifa kwa siku za hivi karibuni. “Kwa muda mrefu kumekuwapo na matamko ya viongozi wa Serikali na wakati mwingine matamko ya viongozi wa CCM kwa wananchi, kwamba maeneo yatakayochagua wapinzani hayatapelekewa fedha za maendeleo na Serikali. “Sasa tunaomba utuambie kama suala hili lipo, ili tuweze kujua ukweli halisi,” alihoji Mbowe. Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu alisema suala hilo halipo kwa kuwa Serikali imekuwa ikipeleka fedha za maendeleo katika maeneo yote bila kujali yanaongozwa na chama gani cha upinzani. “Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili limeulizwa kwa ujumla sana ingawa muulizaji anajua siyo kweli. Hakuna mahali popote ambapo tumeshindwa kupeleka fedha za maendeleo kwa sababu yanaongozwa na Chadema, CUF au chama chochote. “Kwa maana hiyo, naomba Watanzania tuendelee kutimiza demokrasia, kama kuna kauli zingine katika chaguzi, hizo zinatoka kwa bahati mbaya, sisi tutaendelea kutii sheria na kanuni za kazi,” alisema Waziri Mkuu. Pamoja na kutoa majibu hayo, Mbowe alisimama tena na kuuliza swali la nyongeza, huku akisema ushahidi wa kauli za vitisho za mawaziri hao anazo na kutoa mfano kwa baadhi ya chaguzi zilikotolewa. “Mheshimiwa Waziri Mkuu, pamoja na masikitiko yako, kauli hizo zipo na zimekuwa zikitolewa mara kwa mara na baadhi ya mawaziri. “Kwa mfano, hivi karibuni Waziri Nagu (Mary Nagu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji), alitoa kauli hizo wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo Jimbo la Arumeru Mashariki, mwingine ni Waziri Magufuli (John Magufuli, Waziri wa Ujenzi) alitoa kauli kama hizo wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo kule Igunga. “Mwingine ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi (Goodluck ole Medeye) ambaye alitoa kauli hiyo kule Arusha,” alisema Mbowe.

JAMBO UNALOWEZA KULISHANGAA

APRIL 15, 2012 SUNDAY
VIGOGO WAASISI WA FREEMASONS NCHINI TANZANIA NA KUENEA KWA U FREEMASONS KATIKA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI...2
Januari 2005 nchini Isarel ‘walipata’ kiongozi mpya wa Freemasons, Chaim Henry Gehl, ambapo sherehe yao ilifanywa katika Hoteli ya Sheraton iliyopo Herzlia. 
Wageni walitokana Uingereza, Ujerumani,Uholanzi, Austria, Luxemborg,Romania,Italia,Bulgaria na China. Kiongozi huyo alikuwa akikabidhiwa madaraka kutoka kwa Sami Raphaeli, mhasibu mstaafu wa benki mstaafu wa hekalu la Caspi lenye namba 56 lililopo mjini Haifa. Huyu cheo chake cha utendaji mkubwa katika freemasons ni 33rd degree alichotunukiwa mwaka 2003. Naam katika kuselebuka huko ndipo wakajigamba kwamba mnamo Oktoba 9, 2004 kulifanywa sherehe ya kutimiza miaka 100 ya Freemasons katika eneo la afrika mashariki. 
 Hapa kwetu Tanzania haikusemwa sana, ingawaje Jayantilal Kashavji Chande , au Sir Andy Chande katika mahojiano yake na mwandishi wa Ernest C. Ambali(The Guardian, Oktoba 8, 2004) haikuelezwa mahali patakapofanyiwa sherehe hizo. Katika mahojiano yale Sir Andy Chande alieleza kuwa mgeni rasmi alikuwa Rais Benjamini Mkapa na mkewe Mama Anna Mkapa. Pia kulikuwapo na wafanyabiashara wakubwa,wanadiplomasia,mawaziri n.k 
Sir Andy Chande akiwa nchini India katika mji wa Chennai kuzindia hekalu lao East Star alieleza  kwamba ‘marais wawili wa kwanza wa Tanzania (hawakuwa freemasons) lakini walifahamu ni nini’. Je unahitaji akili gani kuwatambua marais wako? Unahitaji Mungu akuongezee ubongo gani ili utambue kuwa ni akina nani wanaozungumziwa? Ndiyo maana nasema tatizo siyo kasi uliyonayo bali kule uendako!
Tukubaliane, kuwa kwa kiasi Fulani inajionyesha ikulu zetu zimezingirwa na Freemasons. Na katika mahojiano hayo hakusemwi ni Dar es Salaam eneo gani ambao sherehe hiyo ilifanywa, lakini katika kumsimika Chaim Henry Gehl (kule Israel)ilitajwa Hoteli ya Royal Palm ambapo wageni 350 walihudhuria.
 Katika miaka hii 100(108) ikaelezwa kuwa Freemasons walianza kujenga hekalu lao la kwanza la Harmony namba 3084 mwaka 1904 mjini Zanzibar. Katika uzinduzi wa jengo hilo Zanzibar inaelezwa Rais Theodore Roosecelt alikuwapo, Duke of York(ambaye baadaye alikuja kufahamika kama Mfalme George VI)na Duke of Connaugh na Strathean walikuwepo pia. 
Ukimsoma mwanahistoria Robert Muchembled(katika; A History of the Devil) ameorodhesha majina yenye kuabudiwa kwa ibada za kishetani lakini tunayathamini na kupofushwa nayo. Nami kwa matendo wanayoyatenda hapa duniani sina soni kusimamia hoja yangu kuwa ni ubatili mtupu waufanyao).
Naweka orodha ya mambo wanayojigamba Freemasons kujinasibu kwa miaka yao 100(108) ndani ya afrika mashariki huku wakibainisha kuwa makao makuu ya eneo zima ni barabara ya Nyerere, jijini Nairobi(soma;The Guardian, 0ktoba 8, 2004). Katika mahojiano hayo ndipo kukaorodheshwa ‘misaada’(ibilisi?), eti Kindwitwi Leprosy Centre(Utete), Mama Theresa Home for the children, shule ya vipofu(Pongwe, jijini Tanga), na Leprosy Projects (jijini Arusha). Montessori School (jijini Mwanza), Mnazi Mmoja Hospitali (iliyopo Zanzibar), Missionaries of Charity, shule ya walemavu (Buguruni, jijini Dar es salaam), wamejenga madarasa shule ya msingi Kinondoni(Dar es salaam) na kutoa pauni za Uingereza 15,000 mnamo mwaka 1996 katika ajali ya Mv Bukoba. Ukiangalia ‘misaada’ yao unapumbazika kuwa ni hisani ya hali juu Na tatizo kubwa linalotukabili, ni utegemezi ambao huzaa utumwa na kukengeuka akili zetu. Tunaishi huru mitaani lakini tupo gerezani, tunakwenda kasi sana lakini hatuangalii tunakokwenda, hatutaki kujua nini hiki tunachosaidiwa? Ni mungu gani aliruhusu mashoga na wasagaji wasimame madhabauni/altareni? Naam ndivyo tunavyouvaa uovu, ndivyo yanakotakiwa Uganda Museven aliruhusu hali hiyo. Na wenyewe husingizia haki za kiraia au dini za kiraia, inaeleweka kuwa Marekani imejngwa na Freemasons kwani wanajieleza kwa mengi tu. Je nasi tuwe na akina Jack Straw wetu bungeni? Tuvuje jasho kwa kupitisha sheria za kuruhusu mashoga, wasagaji halafu tuseme mungu anaruhusu hayo?
VIGOGO  WA FREEMASONS  KATIKA  UKANDA  WA AFRIKA MASHARIKI  NA AFRIKA  KWA UJUMLA
Sir.Andy chande ajitokeza na kusema kuwa yeye ni mmoja wa freemason afrika mashariki .Pia hakuwa nyuma kuwataja viongozi wanaohusika kwenye chama hicho akiwemo rais mstaafu wa awamu ya tatu Mh.Benjamin Mkapa .
Pia alimtaja steven kanumba, msanii nguli hapa Tanzania,Baba Riz raisi wa Tz,lowassa,AY,Mr. Blue,na wengineo wengi. Pia hakusita kumtaja yoweri museveni raisi wa uganda,Obama raisi wa marekani,George Bush,Bill Clinton,George washington,Elizabeth malkia wa uingereza na wengineo wengi.
 Sir.Andy Chande alitaja yeye kwenye chama hicho ni Grand District Master akiwa amebobea kwa miaka 18 iliyopita. 
Alipoulizwa makao yao makuu hapa Tanzania yapo wapi alijibu bila kusita "we are located at sokoine Drive behind kilimanjaro hotel here in Dar es salaam" (tunapatikana barabara ya sokoine nyuma ya hoteli ya kilimanjaro). 
Pia Sir. Andy alisema wananyaraka zote za kumiliki jengo hilo toka serikalini. Aliongezea kuwa vikao vyao hufanyika kwa siri nyakati za usiku na mtu akishaingia kwenye chama hiko hatotoka tena
HUU NI MUHTASARI TU TULIOFANIKIWA KUUPATA KUTOKA KWA MPEKUZI BLOGER KAMA ALIVYONUKUU KIPINDI CHA RADIO YA CLOUDS FM CHA NJIA PANDA MACHI 11, 2012 .
BLOGER
UNAIKUMBUKA HABARI HII???

Edward Lowasa, atabiriwa na TB Joshua?

Pichani Lowasa akiwa kanisani kwa TB Joshua kama anavyoonekana kwenye Emmanuel TV, 12 June 2011
MBINU za Edward Lowassa kutaka kurejea kileleni katika ulingo wa kisiasa zimemnasa mbunge wa Kilindi (CCM), Beatrice Shelukindo, imefahamika.
Beatrice ambaye alikuwa akijitambulisha kuwa mmoja wa “wapambanaji dhidi ya ufisadi,” waliopachikwa jina la “Mitume kumi na miwili,” sasa anatajwa kuhamia rasmi mtandao wa Lowassa.
Gazeti hili limepata ushahidi wa maandishi ya mkono wa Beatrice mwenyewe yanayoonyesha kuwa amekuwa mfuasi muhimu wa Lowassa kiasi cha kushawishi wengine kujiunga katika mtandao wake.
Akiandika kwa Pindi Chana, mbunge wa Viti Maalum (CCM), tarehe 14 Februari mwaka huu, Beatrice alieleza mambo matatu katika ujumbe wake kwa Chana.
Kwanza, kumshukuru Chana kwa kukubali kulinda kura zake. Pili,  kumshawishi kumuunga mkono Lowassa. Tatu, kumweleza juu ya ulokole wake na “mtumishi aliyepakwa mafuta” kutoka Nigeria.
Beatrice anamwambia Chana kuwa Lowassa ndiye kampeni meneja wake. Hii ilikuwa katika uchaguzi wa makamishina wa Bunge; nafasi aliyogombea na kushinda.
“Mungu ni wa ajabu, (Lowassa) ameniombea kura pasipo maelezo. Ameandaa lunch na dinner (vyakula vya mchana na usiku) ambako amekuwa akiniombea kura. Ana njia za ajabu za kufanya mambo. Ahsante kwa kukubali kuhesabu kura,” inasema sehemu ya ujumbe huo.
Chana, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, ndiye alihesabu kura za Beatrice kwenye uchaguzi wa kutafuta makamishina wa Bunge.
Ni kwenye ujumbe huo ambamo Beatrice anatoboa kuwa siri ya ushindi wake ni Lowassa aliyekuwa kampeni meneja wake.
Katika kusisitiza hoja yake, Beatrice anasema, “Nimezungumza na TB Joshua wa Emmanuel TV Nigeria aliyenipa unabii kuwa rais ajaye Tanzania ni Edward Lowassa, nikamuambia haiwezekani kwani amechafuka sana.”
Anasema Joshua alimjibu, “…alikuwa amechafuka sasa amesafishwa kwani katubu. Akaniambia his past is over (maisha yake ya nyuma si kitu). Akaongeza kwa kusema, wewe Beatrice ningeangalia your past (maisha yako ya nyuma) pengine nisingekuombea kabisa. Akasema my past is over (hajali maisha yangu ya nyuma),” inasema sehemu ya ujumbe huo wa Beatrice.
Hata hivyo, Beatrice hakueleza katika waraka wake kwa Chana maisha yake ya nyuma yalikuwa vipi. Wala hajaeleza alifanya nini, hadi kuamini kuwa kama Nabii Emmanuel angeyatazama, basi asingemuombea.
Kuvuja kwa taarifa hizi kumekuja wiki tatu baada ya Lowassa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje.
Mume wa Beatrice, William Shelukindo alikuwa mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambayo iliongoza harakati za kuundwa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba tata wa Richmond.
Ni taarifa ya kamati hiyo iliyosababisha Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa waziri mkuu, Februari 2008.
Kwa mujibu wa watu waliokaribu na Beatrice na kwa ushuhuda wake mwenyewe, mwanasiasa huyo ameamua kujisalimisha kwa Lowassa kwa kile kinachoelezwa kuwa “Lowassa ndiye rais ajaye wa Tanzania.”
Aidha, kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja huku kukiwa na juhudi kubwa zinazofanywa na Lowassa na kundi lake kutaka kujisafisha kwa lengo la kujitosa katika kinyang’anyiro cha urais mwaka 2015.
Miongoni mwa mikakati aliyojiwekea Lowassa na kundi lake ni kujitokeza katika maeneo yote muhimu na kutoa kauli ambazo zitafanya wananchi waanze kumkubali kuwa ni kiongozi anayefaa.
Katika kutekeleza mkakati huo, Januari mwaka huu, Lowassa alijitokeza kuzungumzia vurugu zilizotokea mkoani Arusha zilizotokana na mvutano katika uchaguzi wa meya wa jiji hilo kati ya CCM na CHADEMA.
Katika mnyukano huo, watu watatu walipigwa risasi na polisi na kufariki dunia baada ya polisi kutumia nguvu isiyo ya kawaida kuzima maandamano ya CHADEMA.
Kauli hiyo ya Lowassa ilikuwa tofauti na msimamo wa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba aliyemtaka kuwasilisha maoni yake katika vikao vya chama badala ya kutumia vyombo vya habari.
Kauli nyingine ya Lowassa ilihusu nyongeza ya viwango vya mishahara kwa wafanyakazi, kutokana na kile alichoita mfumuko wa bei kuwa mkubwa.
Bali wiki moja iliyopita, Naibu Katibu Mkuu wa vyama vya wafanyakazi nchini (TUCTA), Nicholas Mganya alimtuhumu Lowassa kwa kutoa kauli hiyo akisema ana ajenda ya siri nyuma yake.
Mgaya alisema TUCTA haihitaji msaada wa Lowassa katika kusimamia madai yao. Alisema “mbunge huyo wa Monduli inaonekana ana ajenda yake mgongoni.”
Hatua nyingine ya Lowassa katika kujikarabati kisiasa ni kugombea na kupata nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
Lowassa amekuwa pia akihudhuria hafla nyingi, hasa za madhehebu ya Kikiristo (KKKT) ambao anaonekana akitoa maoni mbalimbali kama ilivyokuwa Jumapili iliyopita ukumbi wa Dimaond Jubilee kwenye uzinduzi wea albamu ya moja ya kwaya za injili.
Kwenye kusanyiko hilo, Beatrice naye alikuwepo. Lowassa alimtaka asome maoni ya gazeti la The Citizen juu ya ushirikina uliokithiri nchini; jambo ambalo Lowassa alizungumzia kwa urefu.
MwanaHALISI lilipowasiliana na Beatrice ili kupata maoni yake juu ya ushwahiba wake mpya na Lowassa, mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo:
Mwandishi: Tusaidie maelezo kidogo juu ya ujumbe uliomwandikia Mheshimiwa Pindi Chana kumjulisha kuwa uliambiwa Edward Lowassa atakuwa rais. Ni kweli?
Beatrice: Barua ameandika nani na umeipata wapi?
Mwandishi: Hii barua fupi – memo ndani ya Bunge, uliposema Mheshimiwa Lowassa ambaye amesimamia vizuri kura zako za ukamishna wa Bunge.
Beatrice: Sina taarifa hiyo. Wala siikumbuki. Unajua ndani ya Bunge tunaandikiana mambo mengi, tena mengine ya utani tu. Na mimi na Mheshimiwa Chana sote ni “walokole,” tunafanyiana utani sana.
Mwandishi: Kwani mheshimiwa Shelukindo, mkiwa ndani ya bunge kuna utani mwingi, kwamba huwa mnaandikiana utani sana?
Beatrice: Kabisa, unajua tunaandika mambo mengi. Na kama unaandika kwa utani kwa mwenzako inabaki hivyo ni utani tu. Sasa tatizo hao wanaowaletea mambo haya wanatumia mambo haya kutafuta mipango yao ya kufikia mwaka 2015.
Alisema, “Mimi najua hakuna anayenibeba ndugu yangu. Mimi ni very solid (ngangari), sibebeki. Nakwambia, mbona mimi nina nguvu nyingi mimi mwenyewe; sihitaji kubebwa. Najua wanajaribu kuonyesha tunabebwa, lakini huo ni ujinga wao wa kufikiri.
Mwandishi: Mheshimiwa Shelukindo, kwani nyie waheshimiwa huwa mnatafutana (kufitiniana)?
Beatrice: Hiyo inafanyika sana, watu wakishakuwa na mambo yao wanatumia wengine kutimiza dhamira zao. Lakini mimi ninafikiria wananchi. Nimeshaamua kwamba Beatrice nashughulikia shida za wananchi jimboni. Ninatafuta njia za kuwaondolea umasikini, njaa na mambo kama hayo. Sasa wengine wanatafuta tu pa kunishika.
Mwandishi: Kwa hiyo Mh. Lowassa ndiye alikuwa kampeni meneja wako katika kutafuta ukamishna pale bungeni, au siyo Mheshimiwa?
Beatrice: Lakini kama anafanya kazi ya kampeni vizuri; ni vizuri tu. Isipokuwa kila mtu anajichukulia mwenyewe alivyo. Mimi ni mtu wa kazi sihitaji kusimamiwa hivyo. Na hebu tujadili hili; unajua kaka nyinyi mnafanya kazi kubwa. Sasa hii kusikia, sijui MwanaHALISI hivi, sijui hivi, pengine kuna watu wanachomekea vitu vyao. Tunapenda kazi yenu.
Mwandishi: Mheshimiwa nakushukuru sana.
Beatrice: Karibu sana tutafanya kazi pamoja.
Akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, mume wa Beatrice, William Shellukindo, alikuwa na msimamo mkali dhidi ya watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini na hiyo ndiyo inayoelezwa kuwa sababu ya kushindwa kwake ubunge katika mchakato wa ndani ya CCM.
Shellukindo alikuwa mbunge wa jimbo la Bumbuli mkoani Tanga kwa zaidi ya miaka 20, alishindwa katika kura za maoni na January Makamba, mtoto wa katibu mkuu wa CCM anayetajwa kuwa mfuasi wa mtandao wa Lowassa.
S0urce by Mwanahalisi – 9 March 2011

  MUNGU AKUPE PUMZIKO LA AMANI STEVEN KANUMBA

Jeneza lenye Mwili wa Marehemu,Steven Kanumba likiwasili kwenye Viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es Salaam siku ya mazishi yake

(Rest In Peace) RIP - STEVEN KANUPA

MAREHEMU STEVEN KANUMBA ENZI ZA UHAI WAKE

 Marehemu Steven Kanumba akiwa na Pacho Mwamba.
 Steven Kanumba''The great'' with the greatest Nigeria musician 2Face Idibia.
 Ama K.Abebrese and Steven Kanumba ''The great'' smilling for a camera.
 Marehemu Steven Kanumba akiwa na Jackline Walper katika moja ya filamu.
 Marehemu Steven Kanumba akiwa ofisini kwa mkurugenzi Myamba na Nteze.
Mtangazaji na mwandishi wa TBC1 Jane John akifanya mahojiano na Marehemu Steve Kanumba enzi za uhai wake.

MAGAZETI YA LEO;

----PINDA AMZIMA FREEMAN MBOWE, 

---ULAJI WAKITHIRI SERIKALINI-CAG, 

----BABA MZAZI WA LULU AIBUA MAZITO

BABA YAKE ELIZABETH MICHAEL 'LULU' ATAKA JAMII ISIMHUKUMU MWANAWE, HAKI ITENDEKE, AELEZA USHIRIKA WA LULU NA KANUMBA
 Imeandikwa na Daniel Mjema wa Gazeti la Mwananchi.
BABA mzazi wa msanii wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu,' ameitaka jamii kutomhukumu mwanawe kutokana na kifo cha msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba, badala yake iache vyombo vya sheria vifanye kazi yake.
Mzazi huyo, Michael Edward Kimemeta anayeishi mjini Moshi, amewaomba Watanzania kuiachia Mahakama iamue kama mtoto wao anahusika katika kifo hicho ama la.
Kimemeta, ameeleza kuwa binti yake ana umri wa miaka 16 tofauti na inavyoelezwa kuwa ana miaka 18.
Juzi Lulu alifikishwa katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka ya mauaji ya msanii mwenzake, Kanumba.
Kumekuwa na utata uliojitokeza kuhusu umri wa Lulu. Wakati mwenyewe akieleza kuwa ana miaka 17, Jeshi la Polisi lilieleza kuwa umri wake ni miaka 18 na juzi Mahakama iliambiwa kuwa msanii huyo ana umri wa miaka 17 na baba yake akisema ana miaka 16.
Kwa upande wake, mama mzazi wa Lulu Lucresia Karugila, alisema tukio la kifo cha Kanumba na kukamatwa kwa binti yake  Lulu, limempa mshituko mkubwa na kumsababishia maradhi ya kisaikolojia na kimwili.
“Hayo yaliyotokea kwa kweli yamenifanya niumwe kabisa hapa sasa hivi nimelala naumwa…nimempa go ahead (ruksa), baba yake azungumze kwa sababu taarifa zote anazo. Naomba mimi mniache kwa sasa,”alisema.
Kimemeta aliliambia Mwananchi jana kuwa mwanawe huyo alizaliwa Aprili 17 mwaka 1995 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
“Nataka nikuambie (mwandishi) mwanangu atatimiza umri wa miaka 17 ifikapo Aprili 17 mwaka huu. Sasa ana umri wa miaka 16 na ni mtoto. Tunavyosikia Kanumba alikuwa mpenzi wake inatuuma sana,” alisema.
Baba huyo alisema alizaa na mama yake Lulu lakini hawakuwahi kuishi pamoja. "Mwanamke huyo alikuwa akifanya kazi Shirika la Ndege Tanzania (ATC) na muda wote Lulu alikuwa akiishi na mama yake jijini Dar es Salaam,"alisema Kimemeta.
Ameomba familia ya marehemu Kanumba ikubali kupokea pole ya familia ya Lulu kupitia gazeti hili kutokana na mazingira kutoruhusu familia hizo kukutana.
“Nasikitika mazingira ya tukio lenyewe mpaka sasa hayaruhusu familia yetu kwenda kutoa pole na kuifariji familia ya Kanumba kulingana na utamaduni wa mwafrika…tunaomba wapokee pole zetu kupitia njia hii,” alisema.
Kwa mujibu wa Kimemeta, hivi sasa wanahofia maisha yao kutokana na jamii kujenga mtazamo hasi juu ya tukio hilo hata bila ya kusubiri vyombo vya sheria kusikiliza ushahidi wa tukio hilo na kutoa hukumu yake.
Alisema kuwa jamii inapaswa ifahamu kuwa, kikatiba mtu yeyote anayeshitakiwa kwa kosa lolote haimaanishi tayari ni mkosaji, bali atahesabiwa kuwa mtuhumiwa hadi pale Mahakama itakapomtia hatiani.
“Yanasemwa mengi mara ooh Kanumba ndio alianza kumpiga mwanangu mara ooh Kanumba alisukumwa …mimi nasema tuiache Mahakama hata sisi hatupendi mtu auawe, lakini Mahakama iachwe itende haki,”alisisitiza.
Akizungumzia maisha ya mwanawe Lulu, Kimemeta alisema alipokuwa akitangaza Kipindi cha Watoto Televisheni ya ITV, walifarijika sana, lakini alipoanza kuingia kwenye sanaa ya filamu, walijua sasa wamempoteza.
“Baada ya kuingia kwenye sanaa ya maigizo niliona kabisa tumempoteza mtoto na nilimweleza mama yake kuwa wale aliokuwa nao katika maigizo akiwamo Kanumba mwenyewe, nilikuwa siwaamini hata kidogo,” alisema.
Kimemeta alidai kuwa siku moja mwanawe alimpigia simu akimwarifu kuwa alikuwa anakwenda jijini Arusha kurekodi filamu na Kanumba, yeye alipinga safari hiyo akitaka Kanumba amthibitishie usalama wa binti yake.
“Kwa sababu nilikuwa sipendezwi na hayo mambo nilimwambia mama yake azungumze na Kanumba na akatuhakikishia atamlinda na kambi yake ina maadili, lakini kumbe huo ndio ukawa mwanzo wa mwanaye kugeuzwa mpenzi wa msanii huyo,” Alidai Elizabeth Michael 'Lulu,'
Baba huyo mzazi alidai kutofanya vizuri darasani kwa mtoto wake huyo, kulichangiwa na hatua ya kuingia katika sanaa ya uigizaji.
“Lulu alikuwa mtoto mwenye tabia nzuri sana hata alipokuwa ITV kwa kweli alitutia moyo wazazi wake kwa jinsi ITV walivyokuwa wakimlea, lakini alipojiingiza tu kwenye uingizaji hapo ndipo mambo yalipoharibika,” alisema.
Alikanusha madai kuwa mwanawe hakumaliza kidato cha nne na kusisitiza kuwa Lulu alisoma Shule ya Kimataifa ya St Mary's na baadaye alihamia Shule ya Sekondari ya Midway High School na kumaliza kidato cha nne mwaka jana.
Alisisitiza kuwa katika mambo yaliyokuwa yakiwaumiza mioyo, ni namna mtoto huyo alivyozidi kuharibika kwa kuingia katika fani ya uigizaji filamu.
Alisema angependa kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili azungumze naye kama rafiki yake na watafute suluhisho la maadili kwa kizazi cha sasa na cha baadaye.
Alisema tayari ameanza mchakato wa kuonana na Rais Kikwete ili amweleze siri aliyodai ni ‘nzito’ na kudai tayari ametafuta wazee watatu wenye busara wa kumsindikiza, endapo Rais atakubali ombi lake.
Pia ameziomba taasisi zinazojishughulisha na masuala ya haki za binadamu na msaada wa kisheria, kujitokeza na kumsaidia mwanawe.
Lulu alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam juzi na kusomewa shitaka la kumuua Kanumba, tukio lililotokea Aprili 7 mwaka huu eneo la Sinza Vatican.
Msanii huyo hakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa Mahakama hiyo haina
mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mauaji na hivyo alipelekwa rumande Gegeza la Segerea hadi Aprili 23 mwaka wakati kesi hiyo itakapotajwa.
Kifo cha msanii huyo kimetikisa nchi  kutokana na umaarufu wake, akiwa ameigiza filamu 40 zilikuwa zikirushwa katika vituo mbalimbali vya televisheni ndani na nje ya nchi.

Kanumba alipanga kujenga shule

Katika hatua nyingine, Fidelis Butahe na Pamela Chilongola wanaripoti kuwa mchaguaji maeneo ya kupigia picha za filamu za msanii Kanumba, Rahim Khatib alisema marehemu Kanumba alinunua eneo la ekari 15 huko Mpiji mkoani Pwani kwa ajili ya ujenzi wa shule yake ya sekondari.
Khatib alisema Kanumba alikuwa na mpango huo muda mrefu na kwamba lengo lake lilikuwa kuwasaidia wanafunzi wa eneo hilo ambao hutembea muda mrefu kutokana na shule kuwa mbali na eneo hilo.
 “Kanumba alikuwa na mipango mizuri katika maisha yake, kuna eneo kubwa alilonunua Mpiji ili ajenge shule ya sekondari,” alisema Khatib.
Alifafanua kuwa hadi anafariki dunia, aliacha kiasi cha fedha zaidi ya Sh 40 milioni katika Kampuni yake ya Kanumba The Great.
“Marehemu ameacha fedha zaidi ya Sh 40 katika kampuni yake, magari matatu na hivi karibuni alinunua jingine aina ya Toyota Land Cruiser, ”alisema Khatib.
Katika hatua nyingine Khatib alisema kifo cha Kanumba ni pigo kwa watu waliokuwa wakifanya naye kazi akiwemo yeye mwenyewe kwa kuwa walikuwa wakimtegemea kwa kiwango kikubwa.
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu,Steven Kanumba likiwasili kwenye Viwanja vya Leaders Club,jijini Dar es Salaam siku ya mazishi ya msanii huyo wa filamu nchini.

Sintah naye alonga

Kwa upande wake msanii maarufu wa filamu nchini, Christina Manongi maarufu kama Sintah ambaye alikuwa mmoja wa wasanii wa kwanza kufika nyumbani kwa marehemu Kanumba muda mfupi baada ya msanii huyo kuanguka, alisema kuwa siku tano kabla ya Kanumba kufariki, alikuwa na hasira tofauti na alivyomzoea.
Sintah ambaye alikuwa na msanii huyo katika Viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam Jumapili ya Aprili mosi pamoja na mwigizaji mwingine, Steve Nyerere alisema kuwa kila alichokuwa akimuuliza Kanumba, alimjibu kwa ukali.
“Ni tofauti na nilivyomzoea, siku ile ya Jumapili tulikaa pale Leaders Club mpaka usiku sana na kila jambo nililokuwa nikizungumza naye alinijibu kwa mkato na ukali kweli, ilinishangaza,” alisema Sintah
Alifafanua kuwa moja ya mambo waliyokuwa wakizungumza na Kanumba ni pamoja na yeye kutaka kuacha uigizaji, suala ambalo marehemu Kanumba hakuliunga mkono na kumjibu kwa ukali kuwa asijitoe katika uigizaji.

JUMAPILI APRIL 15, 2012

Sunday, April 15, 2012

DIAMOND ASHINDA TUZO TATU KWA MPIGO KILIMANJARO MUSIC AWARD 2012

 Mwanamuziki Diamond (kulia)akipokea tuzo yake kutoka kwa George Kavishe meneja wa bia ya Kilimanjaro mara baada ya kutangazwa mshindi wa utunzi bora wa nyimbo katika hafla ya kukabidhi tuzo kwa wanamuziki bora  Kilimanjaro Music Award 2012 zinazofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam na kuhudhuria na waalikwa mbalimbali pamoja na wadau wa muziki kutoka ndani ya Tanzania  na nje ya nchi.
Msanii  Nassib Abdul ‘Diamond’ usiku huu ameng’ara kwenye tuzo za Kilimanjaro Music Award, baada ya kujinyakulia tuzo tatu.
“Namshukuru Mungu, wakati mwingine uvumilivu na subira ni mzuri. Mwaka jana sikupata tuzo, nikamshukuru Mungu, nikaongeza bidii, nikafanya kazi nzuri, leo ninachukua tuzo ya tatu sasa hivi, alisema Diamond baada ya kushinda tuzo ya Video Bora ya Mwaka, kupitia wimbo Moyo Wangu, ambayo ilikuwa ya tatu usiku huu.
Diamond alizishinda nyimbo za Hakunaga ya Suma Lee, Wangu ya Jay Dee, Ndoa Ndoana ya Kassim na Bongo Fleva ya Dully Sykes.
 Mwanamuziki Diamond akipiga picha na mama yake wa pili kutoka kushoto na Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka kutoka kulia pamona na wanenguaji wake mara baada ya kupokea tuzo yake ya utuzni bora wa nyimbo.
 Mwimbaji wa muziki wa Taarab ambaye ameshinda tuzo ya mburudishaji bora kwa wanawake Malkia Khadija Omar Kopa akitumbuiza katika hafla hiyo usiku huu.
 Malkia Khadija Omar Kopa akishukuru wapenzi wake mara baada ya kushinda tuzo ya mburudishaji bora, wa pili kutoka kushoto ni mume wake na wengine ni watoto wake.
 Watoto wa Malkia wa Mipasho Khadija Omar Kopa wakishuka jukwaani mara baada ya kumtunza mama yao wakati alipokuwa akitumbuiza katika hafla hiyo.
 Kulia ni Msanii Profesa Jay na kushoto ni Mkubwa Fella meneja wa kundi la TMK Family wakimkabidhi tuzo Roma Msanii wa muziki wa Hiphop aliyejishindia tuzo ya msanii bora wa Hiphop.
 Burudani kutoka THT zikiendelea
 Burudani zikiendelea kwa nguzu zote.
 

MAMBO YA TUZO ZA KILIMANJARO MUSIC AWARD 2012 MLIMANI CITY USIKU JANA

 Mwanamuziki Diamond katikati akiwa jukwaani na wenzake kabla ya kuimba wimbo wa msondo katika hafla ya kukabidhi tuzo za wanamuzikii bora za Kilimanjaro Music Award zainazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam kulia ni Khalid Chokoraa wa bendi ya mapacha watatu.
 Msanii HBaba akiwa amezungukwa na vimwana katika hafla hiyo
 Mtayarishaji wa muziki P. Funk kulia akiwa na msanii wa muziki wa Hiphop Jay Moo.
 Wakurugenzi wa ASET kutoka kulia ni Asha Baraka akiwa na kaka yake Baraka pamoja na mdau mwingine katika hafla hiyo.
 Kulia ni Dina Marios wa Clouds akiwa na Asma Makau kutoka Clouds pia.
 Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange Kaburu kulia akibadilishana mawazo na Mulamu Ghambi katika hafla hiyo.
Mohamed Nasor kushoto akiwa na Evance Aveva wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla hiyo usiku huu.

ORODHA YA WALIOTEULIWA KUGOMBEA UBUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI

(Inatolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 5(3) ya Nyongeza ya Pili ya Kanuni za Bunge Toleo la 2007)
_______________________________
1.0 Tarehe 9 Machi, 2012 nilitoa Tangazo kwa vyombo
vya habari na gazeti la Serikali juu ya kuwepo kwa nafasi Tisa wazi za Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki kufuatia kufikia ukomo wa maisha ya Bunge la sasa hapo 04 Juni, 2012.
Katika Tangazo hilo niliwaomba wananchi wenye sifa za kugombea nafasi hizo wafanye mchakato wa kugombea kupitia vyama vyao vya Siasa na fomu za wagombea waliopendekezwa zirejeshwe Ofisi ya Bunge kabla ya saa 10.00 jioni tarehe 10 Aprili, 2012 ambayo ndiyo siku ya uteuzi. Jumla ya Wagombea 34 kutoka Vyama vya Siasa vya CCM, CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI, TLP, UDP na TADEA wamerudisha Fomu.
2.0 Zoezi la uteuzi limekamilika, Wajumbe 33 wametimiza masharti ya uchaguzi kwa mujibu wa Mkataba wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kanuni za Bunge, hivyo, wameteuliwa kugombea nafasi hizo. Aidha, Mgombea mmoja hakutimiza masharti ya uchaguzi ya kuthibitisha uraia wake na kulipa ada ya uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni 5(3) na 6 ya Nyongeza ya Tatu ya Kanuni za Bunge, hivyo hakuteuliwa kugombea.
Ifuatayo ni Orodha ya Wagombea walioteuliwa na wasioteuliwa kugombea nafasi za Ubunge wa Afrika Mashariki:-
1. WAGOMBEA WALIOTEULIWA
KUNDI A: WAGOMBEA WANAWAKE
S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Angela Charles Kizigha
CCM
2.
Nd. Fancy Haji Nkuhi
CCM
3.
Dkt. Godbertha Kokubanza Kinyondo
CCM
4.
Nd. Janet Deo Mmari
CCM
5.
Nd. Janet Zebedayo Mbene
CCM
6.
Nd. Maryam Ussi Yahya
CCM
7.
Nd. Rose Daudi Mwalusamba
CUF
8.
Nd. Sebtuu Mohamed Nassor
CCM
9.
Nd. Shy-Rose Sadruddin Bhanji
CCM
10.
Nd. Sofia Ali Rijaal
CCM
KUNDI B: WAGOMBEA WA ZANZIBAR
S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Abdullah Ali Hassan Mwinyi
CCM
2.
Dkt. Ahmada Hamad Khatib
CCM
3.
Dkt. Haji Mwita Haji
CCM
4.
Nd. Khamis Jabir Makame
CCM
5.
Dkt. Said Gharib Bilal
CCM
6.
Nd. Zubeir Ali Maulid
CCM
KUNDI C: WAGOMBEA WA VYAMA VYA UPINZANI
S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Antony Calist Komu
CHADEMA
2.
Dkt. Fortunatus Lwanyantika Masha
UDP
4.
Nd. Juju Martin Danda
NCCR-MAGEUZI
5.
Nd. Micah Elifuraha Mrindoko
TLP
6.
Nd. Mwaiseje S. Polisya
NCCR-MAGEUZI
7.
Nd. Nderakindo Perpetua Kessy
NCCR- MAGEUZI
8.
Nd. Twaha Issa Taslima
CUF

No comments: