Wednesday, March 27, 2013

ZITO AKANUSHA PAKUBWA YA GAZETINI


March 27, 2013

SIRI YA KUUAWA ZITTO'-SIO KWELI"

 
SIRI YA KUUWAWA ZITTO

Katika gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna habari yenye kichwa chenye maneno ‘ SIRI YA KUUAWA ZITTO YAFICHUKA’ na vichwa vidogo ‘yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini’ dk. Slaa atajwa kumtuma Saanane kummaliza’. Habari hii imeniletea usumbufu mkubwa kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wangu, wamejazwa na wasiwasi mkubwa sana kwamba ninaweza kuuwawa. Napenda kusema yafuatayo:

Moja, sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa Ben Saanane na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa Hoteli ya Lunch Time ambayo sio tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi. Haijawahi kutokea mimi kufanya kikao cha pamoja na Ben Saanane, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika na hivyo naomba mwandishi ahakikishe kuwa vyanzo vyake vya habari vimempa habari sahihi.

Pili, Siamini kamwe kuwa Katibu Mkuu wa chama changu anaweza kupanga kuniua maana hana sababu ya kufanya hivyo. Napenda kurudia kusema kwamba mimi ninaamini kuwa kila nafsi itaonja mauti. Kila mtu atakufa. Kama nitakufa kwa kuuwawa na mtu mwingine ndio itakuwa nimeandikiwa hivyo na Mungu. Ndio maana hata siku moja silalamiki kuhusu vitisho vya kuuwawa nk. Kama kuna mtu anafikiria kuwa kumuua Zitto ndio furaha ya maisha yake atakuwa anajidanganya tu maana Zitto anaweza kufa kimwili lakini mawazo, fikra na maono ya Zitto yataishi tu. Siogopi kufa maana maisha niliyoyachagua ndio haya ambayo yamejaa vitisho. Muhimu kwangu ni kufanya kazi zangu kwa bidii, uhodari na uaminifu. Siku zote nitasimamia ukweli bila kujali uchungu wa ukweli huo.

Tatu, nawashauri watu ambao wamehama CHADEMA na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena. Kama mtu kaamua kuhama CHADEMA anapoteza haki ya kujadili masuala ya CHADEMA maana kama angekuwa anapenda kuyajadili asingehama. Naonya mtu yeyote ambaye anatumia jina langu ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. CHADEMA sio pango la watesaji wala wauaji. Kama kuna mwanachama wa chama kingine cha siasa anayedhani kuna mtu ndani ya CHADEMA anapanga mipango ovu aende kwenye vyombo vya sheria kumshtaki. Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi.

Nne, Nawashauri viongozi wa CHADEMA na hasa wanachama tutumie muda wetu kujenga mshikamano ndani ya chama. Fitna, majungu, uongo, uzandiki nk kamwe havijengi chama. Chama chetu lazima kiwe mfano bora wa kuheshimu demokrasia na haki za binaadamu. Wananchi hawawezi kutoa dola kwa chama chenye mifarakano. Tusiruhusu kugawanywa kwa matakwa ya watu wachache. Tusimamie misingi ya kuanzishwa chama chetu.
Kabwe Zuberi Zitto, Mb
Dar-es-Salaam
Jumatano, Machi 27, 2013

Monday, March 25, 2013

NMB YAKABIDHI DAWATI KAKESE MPANDA






















BENKI ya NMB tawi la Mpanda katika mkoa wa Katavi imekabidhi madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 9.5 katika shule ya msingi Kakese Mbugani iliyoko mjini Mpanda mkoani humo

Akizungumza katika makabidhiano hayo mkuu wa kitengo cha wajasiliamali wadogo na wa kati wa benki hiyo, Filbert Mponzi alisema benki ya NMB imekuwa ikitoa msaada wa madawati katika shule nyingi hapa nchini kutokana na uhitaji mkubwa uliopo wa madawati na baadhi ya mahitaji katika sekta ya elimu nchini

Alisema msaada huo ni sehemu ya azimio la benki hiyo kuwa karibu na jamii kwa kupitia sekta ya elimu ambapo hivi sasa imeanzisha huduma ya elimu ya fedha kwa wanafunzi mashuleni ili kuwajenga wanafunzi kukua katika mzingira yenye taaluma ya mambo ya fedha na hatimae kujenga kizazi chenye uelewa wa masuala ya fedha

Akipokea msaada huo kutoka NMB mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Mpanda, Joseph Mchina alisema shule hiyo inahitaji madawati 345 na yaliyopo shuleni hapo ni madawati 54 mapungufu ni madawati 291 hivyo baada ya NMB kukabidhi madawati 100 upungufu umebaki madawati 191.

Mkurugenzi huyo wa Mji aliishukuru benki ya NMB kwa msaada huo kwani umetolewa katika sekta inayohitaji sana msaada huo na hivyo alitoa wito kwa taasisi zingine za kibenki na zisizo za kibenki kutoa msaada wa madawati na vitu vingine katika shule zilizopo hapa nchini ili kupunguza baadhi ya mahitaji ya shule

Mchina alisema katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa madawati ofisi yake imziagiza shule kutumia asilimia ishirini ya fedha za uendeshaji kutengeneza madawati ambapo katika kipindi cha miezi sita shule ya msingi Kakese mbugani itakuwa imetengeneza madawati 100 hivyo kuwataka wazazi kupitia kamati ya shule nao kuwajibika kuchangia mchango wa madawati shuleni hapo ili kukamilisha pengo la madawati tisini na moja lililobakia

Afisa elimu wa halmashauri ya Mji wa Mpanda Vicent Kayombo alisema halmashauri yake inahitaji madawati 6313 na yaliyopo ni madawati 3213 hivyo kuwepo kwa upungufu wa madawati 3100 ili shule zote ziwe na madawati katika halmashauri yake ambapo alisema mikakati ya kuondoa kero hiyo ni kuwa kila shule itumie mgao wa uendeshaji shuleni pamoja na pesa za ukarafati asilimia ishirini kutengeneza madawati 

Kayombo alisema katika mikakati waliyoipanga katika halmashauri yake wanategemea kuondoa tatizo la uhaba wa madawati katika halmashauri yake kabla ya mwezi julai mwaka huu.

















ZAWADI YA SIKU KUU YA MATAWI 2013

AIFA STARS YAICHAPA MOROCCO BAO 3-1

 Ubao wa Matokeo unavyosomeka mara baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Timu ya Taifa ya Morocco uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.
 Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars),Thomas Ulimwengu akiwatoka Golikipa na Beki wa Timu ya Taifa ya Morocco wakati wa Mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe ya Dunia Mwaka 2014 kule nchini Brazil,uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.Taifa Stars imeshinda Bao 3 - 1,mabao mawili yaliyotiwa kimiani na Mshambuliaji Machachari,Mbwana Samatha huku moja likifungwa na Thomas Ulimwengu.
Kiungo Mshambuliaji wa Timu ya Taifa (Taifa Stars),Shomari Kapombe akichuana vikali na Beki wa timu ya Morocco wakati wa Mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe ya Dunia Mwaka 2014 kule nchini Brazil,uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam.
Lango la timu ya Morocco ilikuwa ni hatari muda wote wa mchezo.
 Kipa wa Timu ya Morocco akiusindikiza kwa Macho mpira ulioingia wavuni,baada ta kuigwa na Mchezaji Mbwana Samatta wa Taifa Stars.

WAKRISTO WAFANYA KUMBUKUMBU YA MATAWI

Baadhi ya Wakristo wakatoliki wakiwa na matawi ya mizeituni kufunya kumbukumbu ya kumpokea mwokozi wao kama walivyofanya wana wa Yerusalemu.

Waamini wakiwa na matawi mbele ya jukwa la Kichangani wakisubiri Padre ayabariki ili kuanza maandamano kuelekea kanisani.


Waamini wakiwa kwenye maandamamo yaliyoanzia Kichangani kuelekea Kanisa Kuu la Kiaskofu Kihesa.

Wanakwaya wa Kwaya ya Mt. Cecilia Parokia ya Kihesa wakiwa kwenye maandamamo kuingia Kanisani.

Sunday, March 24, 2013

NMB YAKABIDHI DAWATI MIA SHULENI KAKESE



HALMASHAURI ya mji wa Mpanda imeishukuru benki ya NMB Tawi la Mpanda kwa kukabidhi madawati mia moja katika shule ya Msingi Kakese Mbugani yenye thamani ya shilingi milioni tisa na nusu na kupunguza kero ya uhaba wa madawati shuleni hapo

Akizungumza mara baada ya kupokea madawati hayo kutoka kwa benki hiyo Mkurugenzi wa mji wa Mpanda Joseph Mchina alisema mchango wa madawati mia kwa ajili ya shule ya Msingi Kakese mbugani kunasaidia juhudi za serikali za kuondoa kero ya uhaba wa madawati hapa nchini

Alisema katika halmashauri yake kuna uhitaji wa madawati 6313 wakati yaliyopo ni madawati 3213 na hivyo kuwa na upungufu wa madawati 3100 na kutokana na msaada wa benki wa madawati mia upungufu unabaki dawati 3000

Alitoa wito kwa taasisi zingine kurejesha sehemu fa faida yake kwa kusaidia jamii katika sekta ya elimu, afya na maendeleo ya wanawake na watoto

Akizungumza katika hafla hiyo mkuu wa kitengo cha wajasiliamali wadogo na wa kati wa NMB, Filbert Mponzi alisema hivi sasa benki yake imeanzisha utaratibu wa kutoa huduma ya elimu ya fedha mashuleni ili kuwajenga wanafunzi kukua katika elimu ya fedha

“Tunataka kuhakikisha tunajenga kizazi chenye uelewa na taaluma ya fedha kutoka shuleni hadi katik jamii’’
alisema afisa huyo wa benki