Saturday, May 5, 2012

HABARI NA MATUKIO MAPYA

Agosti 9, 2012

BALOZI MAHALU ASHINDA KESI


Balozi Profesa Mahalu katikati akitoka nje ya mahaka ya Kisutu huku akiwa ameongozana na mdogo wake Mirasi Rama kulia ni Wakili wa kujitegemea Mabere Nyaucho Marando,baada ya kushinda kesi iliyokuwa ikimkabili akidaiwa kununua nyumba ya Ubalozi wa Tanzania nchini Italia, Akisoma hukumu iliyosomwa kuanzia Saa sita leo na Hakimu Mfawidhi mkazi wa mahakama ya Kisutu Mh. Ilivin Mugeta imemtoa Balozi Profesa Mahalu katika hatia na kumwachia huru(picha na FullShangweblog)
 
NANE NANE 2012 JIJINI MBEYA YABOA, YAKOSA MSISIMKOA, RUKSA AMUACHIA RC IRINGA KUWA MGENI RASMI BADALA YAKE KWA UKATA WA TASO,







AZAM FC NA YANGA ZATINGA FAINALI YA KAGAME 


Mchezaji wa timu ya APR ya Rwanda Selemani Ndikumana akimiliki mpira mbele ya beki wa timu ya Yanga Oscar Joshua katika mchezo wa nusu fainali uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini DSM jana. FAINALI ni Yanga na Azamu Jumamosi
Diwani wa Kata ya Kwadelo, Alhaji Omari Kariati (wa tatu kushoto) akiwa kwenye trekta na wakulima wa Kata hiyo, Abdallah Ramadhani (kushoto), Gabriel Galahenga, baada ya kuwakabidhi wakulima hao matrekta manne, kwenye Ofisi za Shirika la Uchumi la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)-SUMA JKT, Mwenge jijini Dar es Salaam, jana Julai 26, 2012.

Wakulima wa kata hiyo ya Kwadelo,  Alifa Hurufya, Gabriel Galahenga (wapili kushoto) na Meneja wa Mradi wa SUMA JKT, Kanali Felix  Samillan katika makabidhiano ya matrekta ya kulimia.


4. Meneja wa Mradi wa SUMA JKT, Kanali Felix  Samillan akisalimiana na Diwani wa Kata ya Kwadelo, Kondoa mkoani Dodoma, Omar Kariati wakati wa hafla ya wakulima wa kata hiyo kukabidhiwa matrekta manne  kwenye Ofisi za Suma JKT, Mwenge Dar es Salaam, jana Julai 26, 2012.

Wanahabari nao hawakuwa nyuma kwenye hafla ya makabidhiano ya  matrekta ya wakulima






JULY 26, 2012

NI NANI WA KUSAIDIWA HAPA?

Mwanamke ambaye ni mlemavu akizunguka katika eneo la Posta jijini Dar es Salaam kuomba chochote kutoka kwa wasamaria wema huku akiwa amebeba mtoto wake mgongoni, sasa ni nani wa kusaidiwa hapa kati ya mtoto na mama?

WAZIRI MWANRI AGEUKA MBOGO KIGOMA

Naibu waziri wa TAMISEMI Aggrey Mwanri
Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggry Mwari amesema atashuka nao wazima wazima, watendaji wabovu na wanaokiuka maadili za kazi mkoani hapa.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa CCM, kwenye Uwanja wa Community Centre, uliopo mjini Mwanga mkoani Kigoma, Mwanri alisema, anazo tarifa kwamba wapo baadhi ya wafanyakazi katika baadhi ya vituo vya afya, zahanati na hospitali mkoani Kigoma ambao wamekuwa wakiwataka wanaojifungua kutoa fedha kwa ajili ya nyembe na glovu wakati wa kujifungua.

Mwanri alisema, tabia hiyo ni kinyume na utaratibu na maagizo ya serikali, kwa kuwa kina mama wanaojifungua, wazee, watoto na wenye magonjwa sugu hawapaswi kutozwa malipo wakati wa kupatiwa matibabu.

"Nimeisikia kero hii kwamba ipo pia kwenye hospitali zetu hapa Kigoma, sasa nawaambieni tafadhalini sana acheni tabia hii mara moja, na ninatangaza mbele ya kadamnasi hapa kwamba, tutakayempata anakiuka taratibu zetu nitamshukia mzima mzima na kumfukuza kazi mara moja", alisema Mwanri.

Alisema, Sserikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya kuhudumiwa watu wa kada hiyo bure, sasa haingii akilini anapotokea mtumishi wa umma anamdai fedha mwananchi mwenye fursa ya kuhudumiwa bure.

Akizungumzia kero ya wauza maandazi na mchicha kutozwa ushuru, Mwanri alizitaka Halmashauri za Miji hapa nchini kote ikiwemo ya mji wa Kigoma, kuacha mara moja kuwatoza ushuru watu hao kwa maelezo kwamba si wafanya biashara wanaopaswa kutozwa ushuru.

"Hawa kina mama wauza maandazi, mchicha na bamia hawa si wafanyabiashara ni wachuuzi tu wanaoganga njaa, sasa mkianza kukimbizana nao kuwadai ushuru mtasababisha waishi maisha magumu sana, naagiza hawa msiwatoze kabisa ushuru", alisema Mwanri.

Akituzungumzia kuhusu kupandishwa ushuru kwa wachuuzi mkoani Kigoma kutoka Sh. 200 hadi 300, Mwanri alisema, kiwango kilichopandishwa kinaonyesha kuwa mzigo mkubwa kwa wafanyabiashara kutozwa kila siku hivyo uongozi wa Halmashauri ukutane na kutanza namna nzuri itakayoweza kuweka viwango nafuu.

"Katika hili lililopitishwa kisheria zitaweza kulitolea uamuzi hapa hapa, lakini kwa kuwa linazusha malalamiko sana, nawaagiza watendaji wa halmashauri hii ya Kigoma/Ujiji mkutane haraka na kupitia taratibu za kusheria mtuletee viwango vingine vya ushuru", alisema Mwanri.

Pia Mwanri aliendeleza kauli yake ya kupiga marufuku, mtindo wa kuwafukuza watoto shuleni kutokana na wazazi kudaiwa michango ya shule.
Alisema, kimsingi hakatai michango mashuleni kama ina tija, lakini akasema, kama kichango hiyo imekubaliwa na wazazi katika vikao halali, wakumbana si mtoto ni mzazi mwenyewe.

"Nasema kuhusu hili watoto wetu hawa tutawalinda kama watoto wa kuku wanavyolindwa wasiraruliwe na mwewe, hatutakubali kabisa tabia hii ya kuwafukuza shule watoto eti kisa mzazi anadaiwa hela ya mchango wa shule, tabia hii ikome kabisa", alisema Mwanri.

Mbali na kupiga marufuku watoto kufukuzwa, Mwanri alizitaka shule kuhakikisha hazianzishi michango hovyo hovyo na kwamba shule haziruhusiwa kila moja kutangaza michango yake, badala yake mamlaka ya kutangaza michango ya shule yoyote ni kwa usimamizi wa mkoa tu.

Mwanri aliwataka wazazi nao kuwa makini na michango ya shule, kwa kuhakikisha wanahudhuria vikao vyote vya kamati za shule ili kama kuna michango isiyofaa waikatae.

Mkutano ulihudhuriwa pia na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano, Steven Wasira, Naibu Waziri wa Uchukuzi Dk. Charles Tzeba, Naibu Waziri wa Maji Dk. Birinith Mahenge, Mbunge wa Kigoma mjini Peter Serukamba, Mbunge wa Viti Maalum Kigoma, Josephine Ngenzabuke na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye ambaye ndiye alikuwa mkuu wa msafara huo.

Waziri Wasira, Tzeba na Mahenge nao walipata fursa kuelezea serikali inavyoshughulikia kumaliza kero zinazohusu sekta zao mkoani Kigoma na Tanzania kwa jumla.

Mkutano kama huo wa CCM unaohusisha mawaziri ni wa tatu, mingine ni ulifanyika jijini Dar es Salaam, kwenye Viwanja vya Jangwani na wapili ulifanyika hivi karibuni mkoani Rukwa.

Kwa mujibu wa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi CCM, lengo la mikutano hii ni kuwezesha watendaji wa serikali kueleza kinaga ubaga utendaji wao na namna wanavyoshughulikia kero mbalimbali zinazokuwepo kwenye sekta zao.

July 24, 2012


SAKATA LA WALI WA SHEREHE WENYE SUMU, POLISI YAWAKAMATA WATANO

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Peter Kakamba
SAKATA la watu zaidi ya 40 kula wali katika sherehe ya kutoa mahali unaosadikka kuwa na sumu limeendelea kuchukua sura mpya baada ya jeshi la polisi mkoani Iringa kuwakamata watu watano wakituhumiwa kuhusika na tukio hilo la kuweka sumu katika chakula hicho.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamhanda aliwaambia waandishi wa habari leo ofisini kwake kuwa watuhumiwa hao wanatuhumiwa kuweka sumu katika chakula hicho na kupelekea mtu mmoja Faruni Nyaupembwe (65) ambaye ni mkazi wa kijiji hicho cha Ibofye wilaya ya kilolo kufariki dunia na wengine kulazwa hospital.

Kamhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea Julay 23 majira ya jioni katika kijiji cha Ibofye wilaya ya kilolo mkoani Iringa ambako watu hao walikuwa katika sherehe ya kuoza binti na ndipo walipoandaliwa chakula hicho na baada ya kula kilionekana kuwaletea matatizo na kupelekea kifo cha mzee huyo ambaye anadaiwa kula zaidi wali huo.

Aliwataja waliokamatwa na jeshi la polisi kwa kutuhumiwa kuhusika na tukio hilo kuwa ni Wailes Ngaile(58) Edward NYaupumbwe (60), Eliutu Ilagila(78) Ibrahimu Nyombe(78) na Adelina Ilagila(60) wote ni wakazi wa Isoliwanya .

Alisema kuwa jeshi la polisi linaendelea kuwashikilia watuhumiwa hao pamoja na kufanya uchunguzi zaidi juu ya tukio hilo kabla ya watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani.

Wahanga wa tukio hilo ambao wamelazwa katika kituo cha afya cha Ipogolo mjini Iringa walimweleza mwandishi wa habari hizi kuwa tukio hilo lilitokea nyumbani Bw James Ngaile ambako kulikuwa na shughuli yta kupokea mahali na baada ya shughuli hiyo kiliandaliwa chakula na kinywaji hicho aina ya togwa kwa kwa ajili ya sherehe ya kuoza binti yake.

Alisema Yamile Mhehe ambaye amelazwa katika kituo hicho cha afya kuwa utaratibu wa chakula katika sherehe hiyo ilikuwa ni sahani moja kwa watu watatu na kuwa chakula kilichoandaliwa ni wali na ugali huku mboga ikiwa ni maharage na kabichi na baada ya chakula wageni walikuwa wakitumia kinywaji aina ya togwa kwa ajili ya kushushia chakula hicho.

Hata hivyo alisema baada ya kula chakula hicho muda wa saa moja usiku wananchi waliofika katika sherehe hizo walitawanyika kurejea majumbani kwao na kuwaacha walengwa wa sherehe hiyo wakiendelea na mapumziko ya usiku.

Alisema baada ya kufika nyumbani muda wa saa 2 usiku tumbo la kuharisha damu lilianza kumsumbua yeye na mke wake na hivyo kulazimika kukimbia kwa majirani kuomba msaada zaidi na baada ya kufika huku walikuta majirani zao nao wakisumbuliwa kama wao hali iliyowalazimu kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa kijiji ambaye pia alikuwa hajiwezi kutokana na kukumbwa na tatizo kama hilo.

Hivyo kutokana na hali hiyo kuonekana kuwakumba watu zaidi ya 20 katika kijiji hicho uongozi wa kijiji ulilazimika kukodisha daladala na kuwachukua wagonjwa wote na kuwapeleka kituo cha afya Ihimbo na baadhi yao ambao hali zao zilionekana kuwa mbaya walikimbizwa kituo cha afya Ipogolo na wengine Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Iringa.

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Godfrey Mtete alisema kuwa tukio hilo ni la kwanza kutokea katika kijiji hicho na kuwa hadi sasa bado hawajabaini tatizo lilikuwa katika chakula ,mboga ama togwa hiyo kwani alisema mbali ya tatizo hilo kuwakumba watu waliofika katika sherehe hiyo baadhi ya watoto kama watatu wamelazwa patwa na mkasa huo japo hawakula chakula wala kunywa kinywaji katika sherehe hiyo.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa idadi ya wananchi waliopatwa na tatizo hilo ni 40 na kuwa watu zaidi ya 38 ndio ambao walionekana kuwa mahututi zaidi na kukimbizwa kupatiwa matibabu huku baadhi ya wananchi wameendelea kufikishwa Hospitalin jana baada ya kuonekana kuathirika na chakula hicho.

Alisema hatua ambayo kijiji kimechukua kuhusu chakula hicho ni kuzuia chakula hicho kumwagwa wala kupewa nguruwe ili kiweze kuchunguzwa zaidi .

Monday, July 23, 2012


Siku ya Mashujaa kufanyika kitaifa katika viwanja vya Mnazi mmoja tarehe 25 Julai 2012 jijini Dar es salaam, mgeni Rasmi Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa Tanzania



Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki (katikati) akiongea na waandishi wa habari Katika viwanja vya Mnazi mmoja leo jijini Dar es Salaam kueleza namna mkoa ulivyojipanga kufanikisha sherehe za maadhimisho ya siku ya mashujaa itakayofanyika kitaifa tarehe 25, Julai 2012 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakitoa heshima kwenye mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa katika viwanja vya mnazi mmoja leo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sherehe za maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa.
Kiongozi wa mabalozi wan chi za Afrika wanaoishi nchini Tanzania Balozi Juma Mpango kutoka Congo DRC akiweka shada la maua kwenye mnara wa kumbukumbu ya mashujaa leo jijini Dar es salaam ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sherehe ya siku ya mashujaa itakayofanyika tarehe 25, Julai 2012.Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

Wananchi wa mkoa wa Dar es salaam wameombwa kujitokeza kwa wingi wakati wa sherehe za maadhimisho ya kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa itakayofanyika kitaifa katika viwanja vya Mnazi mmoja tarehe 25 Julai 2012 jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam , Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki amesema maandalizi ya maadhimisho hayo yamekamilika na kufafanua kuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.

Amesema katika maadhimisho hayo kwa upande wa mkoa wa Dar es salaam baadhi ya barabara zitafungwa ikiwemo barabara ya Nyerere, Uhuru na Bibi Titi Mohamed ili kuhakikisha usalama kwa wale wote watakaohudhuria maadhimisho hayo na kuongeza kuwa katika kuboresha maadhimisho hayo kamati ya maadhimisho itaweka luninga katika maeneo yote muhimu ili kuwawezesha wananchi kuona yanayotendeka wakati wa maadhimisho hayo.

Aidha Bw. Meck Sadiki amesema kuwa maadhimisho hayo ni kumbukumbu muhimu katika historia ya Tanzania kwa kuwaenzi mashujaa waliojitoa muhanga katika jitihada za kuikomboa na kuilinda Tanzania.

“ Maadhimisho haya ni kumbukumbu muhimu sana katika historia ya nchi yetu kwani tunawaenzi mashujaa wetu waliojitoa muhanga katika jitihada za kuikomboa, kuilinda na kudumisha amani na utulivu wan chi yetu

Dkt Rotich kufungua mafunzo ya Wapigapicha kesho Arusha

 



NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), anayeshughulikia Shirikisho la Kisiasa, Dkt. Julius Rotich (pichani) anataraji kufungua mafunzo ya siku tatu ya upigaji picha yajulikanayo kama ‘EAC-GIZ Master Class Photographers Training’ yatakayo anza Julai 23-26, 2012 mjini Arusha.
Juma la wapigapicha 10 kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki wanataraji kuhudhuria mafunzo hayo ya siku tatu ya Upigaji yatakayofanyika katika Hotel mjini Arusha.
Mafunzo hayo ya nadharia na vitendo yameandaliwa kwa ushirikiano kati ya Jumuia ya Afrika Mashariki na Shirika la Kijerumani (EAC) na GIZ yatahusiha wapigapicha hao kumi, wawili kutoka kila nchi.
Tanzania inawakilishwa na Mpigapicha Mwandamizi wa Magazeti na Habari za Mtandao, Mroki Mroki, Mwasisi na Mhariri Mkuu wa FATHER KIDEVU BLOG pamoja na Mwandshi wa Kampuni ya Mwanachi Comunication mjini Arusha, Filbert Rweyemamu.
Tayari wapigapicha hao wa Habari wapo mkoani Arusha wakiwasubiri wenzao wa Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi kuwasili kwa kuanza mafunzo hayo.
Mkufunzi wa mafunzo hayo ni Balozi wa Heshima wa Utalii nchini Kenya na Mwenyekiti wa mfuko wa 50 Treasures of Kenya, Hartmut Fiebig

Rais Kikwete afuturu na Viongozi wa Dini Mbeya


 

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa dini mbalimbali aliowaalika katika futari katika ikulu ya mjini Mbeya jana jioni.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika swala ya magharibi muda mfupi kabla ya futari ambayo aliwaalika viongozi mbalimbali wa dini mjini Mbeya jana(Picha na Freddy Maro)
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika swala ya magharibi muda mfupi kabla ya futari ambayo aliwaalika viongozi mbalimbali wa dini mjini Mbeya jana(Picha na Freddy Maro)

RC MANYANYA AMUOMBA WAZIRI WA MAJI PROF. JUMANNE MAGHEMBE KUUPA KIPAUMBELE MAALUM MKOA WA RUKWA KATIKA MIRADI YA MAJI



Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara ya waziri wa maji Prof. Jumanne Maghembe mkoani humo. kushoto ni katibu tawala wa mkoa Alhaj Salum Chima

NA RAMADHANI JUMA,
AFISA HABARI-SUMBAWANGA
MKUU wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya ameiomba serikali kuupatia kipaumbele maalum mkoa huo katika miradi ya maji kutokana na kukabiliwa na upungufu wa muda mrefu wa huduma hiyo.
Alitoa ombi hilo kwa waziri wa Maji Mh. Profesa Jumanne Maghembe wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya waziri huyo mkoa humo kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Alisema kuwa, licha ya tatizo hilo kuwa kubwa na la muda mrefu, huenda upungufu huo wa huduma ya maji safi ukaongezeka mara dufu mara baada ya ujenzi wa barabara zinazounganisha mkoa huo na ule wa Mbeya na Katavi kukamilika kwa kiwango cha lami, hali itakayosababisha idadi ya watu kuongezeka kutoakana na shughuli za kiuchumi kushamiri.
Manyanya alipendekeza serikali kutekeleza miradi midogomidogo ya maji ya visima mkoani humo ili kuwaharakishia wakazi wake huduma hiyo muhimu.
Kwa upande wake, waziri Profesa Maghembe iliahidi kuwa, serikali itatekeleza miradi ya maji katika vijiji 10 vya kila wilaya ya Mkoa huo ambazo ni Sumbawanga, Kalambo na Nkasi.
Alisema kuwa, utekelezaji wa mpango huo utaanza na vijiji vitatu katika kila wilaya na tayari shilingi bilioni 1.4 zimetengwa kwa ajili awamu ya kwanza kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika miji ya Laela, Matai na kijiji cha Nankanga.

July 23, 2012


BREAKING NEWS....WALI WA SHEREHE WAUA MMOJA 40 HOI IRINGA

Wahanga wa tukio hilo wakiwa hoi kituo cha afya Ipogolo Iringa
Mganga mfawidhi wa kituo cha afya Ipogolo Dkt mary Makundi
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Ibofye wilaya ya Kilolo Godfrey Mtete (kushoto) akiwa na mgonjwa mwingine ktk kituo cha afya Ipogolo walikolazwa kwa kula chakula chenye sumu

MTU mmoja mkazi wa kijiji cha Ibofye wilaya ya Kilolo mkoani Iringa amefariki dunia na wengine zaidi ya 40 wamelazwa katika Hospitali mbali mbali za mkoa wa Iringa kikiwemo kituo cha afya Ipogolo na Hospital ya rufaa ya mkoa wa Iringa baada ya kula wali na kunywa togwa zinazosadikika kuwa na sumu katika shehere ya kutoa mahali .

Wahanga wa tukio hilo ambao wamelazwa katika kituo cha afya cha Ipogolo mjini Iringa waliueleza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com leo kuwa tukio hilo lilitokea juzi jumamosi baada ya mkazi wa kijiji hicho Bw James Ngaile kuandaa chakula na kinywaji hicho aina ya togwa kwa kwa ajili ya sherehe ya kuoza binti yake.

Alisema Yamile Mhehe ambaye amelazwa katika kituo hicho cha afya kuwa utaratibu wa chakula katika sherehe hiyo ilikuwa ni sahani moja kwa watu watatu na kuwa chakula kilichoandaliwa ni wali na ugali huku mboga ikiwa ni maharage na kabichi na baada ya chakula wageni walikuwa wakitumia kinywaji aina ya togwa kwa ajili ya kushushia chakula hicho.

Hata hivyo alisema baada ya kula chakula hicho muda wa saa moja usiku wananchi waliofika katika sherehe hizo walitawanyika kurejea majumbani kwao na kuwaacha walengwa wa sherehe hiyo wakiendelea na mapumziko ya usiku.

Alisema baada ya kufika nyumbani muda wa saa 2 usiku tumbo la kuharisha damu lilianza kumsumbua yeye na mke wake na hivyo kulazimika kukimbia kwa majirani kuomba msaada zaidi na baada ya kufika huku walikuta majirani zao nao wakisumbuliwa kama wao hali iliyowalazimu kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa kijiji ambaye pia alikuwa hajiwezi kutokana na kukumbwa na tatizo kama hilo.

Hivyo kutokana na hali hiyo kuonekana kuwakumba watu zaidi ya 20 katika kijiji hicho uongozi wa kijiji ulilazimika kukodisha daladala na kuwachukua wagonjwa wote na kuwapeleka kituo cha afya Ihimbo na baadhi yao ambao hali zao zilionekana kuwa mbaya walikimbizwa kituo cha afya Ipogolo na wengine Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Iringa.

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Godfrey Mtete alisema kuwa tukio hilo ni la kwanza kutokea katika kijiji hicho na kuwa hadi sasa bado hawajabaini tatizo lilikuwa katika chakula ,mboga ama togwa hiyo kwani alisema mbali ya tatizo hilo kuwakumba watu waliofika katika sherehe hiyo baadhi ya watoto kama watatu wamelazwa patwa na mkasa huo japo hawakula chakula wala kunywa kinywaji katika sherehe hiyo.

Mtete alisema hadi sasa mtu mmoja ambaye yeye alikuwa akimwita mjombe wake aliyemtaja kwa jina la Wagila Nyaupumba amefariki dunia kabla ya kukimbizwa hospital kwa matibabu.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa idadi ya wananchi waliopatwa na tatizo hilo ni 40 na kuwa watu zaidi ya 38 ndio ambao walionekana kuwa mahututi zaidi na kukimbizwa kupatiwa matibabu huku baadhi ya wananchi wameendelea kufikishwa Hospitalin jana baada ya kuonekana kuathirika na chakula hicho.

Alisema hatua ambayo kijiji kimechukua kuhusu chakula hicho ni kuzuia chakula hicho kumwagwa wala kupewa nguruwe ili kiweze kuchunguzwa zaidi .

Aidha alisema mbali ya chakula hicho kuwakumba wageni waliofika katika shughuli hiyo ya kuona binti bado bibi harusi mtarajiwa na bwana harusi pamoja na wazazi wa pande zote mbili pia ni wahanga wa tukio hilo .

Mganga mfadhiwa wa kituo cha afya Ipogolo Dkt Mary Makundi alithibitisha kupokea wagonjwa 9 kati ya 40 katika kituo hicho na kuwataja wagonjwa waliolazwa katika kituo hicho kuwa ni Rafiki Kabogo, Beth Ngaile, Neema Ngaile, Emelia Mwalafi, Edina Mkemangwa, Costanzia Maliga, Ayubu Kaywanga Godfrey Mtete na Yamile Mhehe.

Huku akidai hali zao zinaendelea vizuri na kuwa wagonjwa wengine walifikishwa hospitali ya mkoa wa Iringa na kituo cha afya Ihimbo kwa matibabu zaidi .

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael kamhanda alipoulizwa na mtandao huu kwa njia ya simu jana kuhusu tukio hilo alisema bado halijafika ofisini kwake na kuwa pindi litakapomfikia atalitolea ufafanuzi.

MADIWANI MPANDA MJINI WAWABANA WATAALAMU WAZEEMBE

HIVI NDIVYO CCM ILIVYOFANYA MKUTANO WAKE KIGOMA JANA

Habibu Ally wa kikundi cha Ujiji cha Sebene akicharaza kinanda akiwa chali wakati wa mkutano huo
Mamia ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa CCM katika Uwanja wa Community Centre, Mwanga mkoani Kigoma


Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akituzwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba alipocharaza gita, kwenye mkutano wa CCM, Uwanja wa Communiy Cetre, Mwanga Kigoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala wa Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI,) Aggrey Mwanri akihutubia, kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma. ([picha zote na Bashir Nkoromo Kigoma)

ALAUMIWE NANI KATIKA HILI??????? , Ndani kuna WAKURUGENZI WAGOMEA TAMISEMI KUHUSU USHURU WA MCHICHA NA VITUMBUA.

WANAFUNZI wa shule mbili za msingi zilizoko mjini Mpanda katika mkoa wa Katavi wako hatarini kutokana na uwanja wa shule kutumika kama eneo la maegesho ya malori makubwa yanayobeba mizigo.

Blog hii imebaini kuwa uwanja wa shule ya msingi Mpanda na shule ya Msingi Muungano unatumika kama uwanja wa kuegeshea magari makubwa yanayofafanya kazi za usombaji wa mizigo ya mazao toka shambani hadi mjini Mpanda katika eneo la Mpandahoteli 

Imebainika kuwa idadi ya malori yanayoegesha eneo la uwanja huo inafikia hamsini kwa siku na wakati mwingine hata eneo la kuegesha malori hukosekana kabisa kutokana na uwanja kuzidiwa na idadi kubwa

Katika eneo hilo kumekuwa na kelele za magari, kelele za wapagazi, lugha chafu za matusi ambazo hazifai kwa taasisi za elimu hasa zinazolea vijana ambao watarajiwa kuwa viongozi na wanataaluma mbalimbali hapa nchini katika kipindi cha miaka ijayao
Baadhi ya wanafunzi waliohojiwa kuhusu hali hilo walidai kuwa walishalalamika kwa walimu wao lakini hakuna juhudi zozote za kuwaondoa wanaoegesha malori

Kwa upande wao walimu wa shule ya Msingi Muungano na shule ya msingi Mpanda walisema kuwa taarifa zilipelekwa halmashauri ya mji wa Mpanda katika idara ya elimu na mipangomiji lakini hakuna juhudi zozote kutoka halmashauri za kuyaondoa malri hayo.
Walimu hao walielezea kero wanakumbana nazo kuwa ni pamoja na kukosa vipindi cya michezo, ufundishaji kuwa mgumu wawapo darasani, wananfunzi kukosa utulivu wa kutafakari, masomo ya nje ya darasa, wanafunzi kujifunza matusi na lugha chafu pamoja na fursa ya michezo kwa wanafunzi.

Mkurugenzi wa Mji wa Mpanda, Josefu Mchina alipotakiwa kueleza ni kwa nini ofisi yake imebariki malori makubwa na magari mengine kutumia eneo la uwanja wa shule kama maegesho ya magari alitupia lawama zote kwa jeshi la polisi kuwa limekuwa halichukui hatua thabiti kukomesha hali hiyo licha ya ofisi yake kuwasilisha ombi la kuyaondoa malori katika eneo la uwanja wa shule ya msingi Mpanda na muungano










MHE. MWANRI UNACHEZEWA RAFU MIKOANI, HII NI KATAVI JE RUKWA NA KIGOMA....


SERIKALI imepiga marufuku halmashauri za jiji, manispaa, miji na wilaya nchini kuwatoza ushuru wachuuzi wadogowadogo wanaotafuta mahitaji ya kujikimu kupitia biashara ndogondogo.
Agizo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki na Naibu waziri kutoka ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa nchini, Mhe. Aggrey Mwanri alipokuwa katika ziara ya siku mbili katika mikoa ya Rukwa na Katavi kuelezea utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2012/15 akiambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Nape Nnauye, Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM, Mhe.  Lameck Mwigulu Nchemba, Waziri wa Maji, Mhe. Profesa Jumanne Maghembe na manaibu mawaziri wenzake wanne.
Mhe.  Mwanri alisema hivi sasa serikali imerejesha utaratibu wa kupeleka ruzuku katika halmashauri zote nchini kuziba pengo lilitokana na kufuta ushuru mdogo kwa wachuuzi wadogo wadogo wanaoendesha biashara za kujikimu kimaisha na hivyo hakuna halmashauri itakayosingizia kuwa ushuru mdogo ni sehemu ya vyanzo vya mapato ya ndani
Akihutubia katika mikutano ya hadhara mjini Sumbawanga na Mpanda Mhe. Mwanri alisema hakuna kuwatoza ushuru wauza vitumbua, wauza mchicha, nyanya, vitunguua vya mafungu, auza dagaa za mafungu na wanaouza samaki wa kukaanga katika sinia au nyungo ambao wanakuwa wachuuzi na siyo wauzaji wakubwa.
Alisema wale wanaopeleka mizigo sokoni kwa ujazo mkubwa kama vile wanakodisha fuzo na vyombo vingine vya busafirishaji watozwe ushuru kama kawaida isipokuwa wachuuzi wadogo wadogo wanaouza bidhaa ili wapate pesa ya mafuta ya taa, kibaba kimoja cha mafuta ya kula na chumvi hao waachwe mara moja wasitozwe ushuru
“Nakuagiza mkurugenzi, kuanzia kesho hakuna kumtoza ushuru mama muuza vitumbua, muuza mafungu ya mchicha, anayepanga nyanya za mafungu, muuza samaki wa kukaanga na wengine kama hao, mwiko kutoza ushuru walalahoi, ukitaka nishuke na wewe tangu hapo hadi chini endelea kutooza ushuru walalahoi, itakuwa nginja nginja na wewe mpaka kieleweke” alisema Mhe. Mwanri
Alisema serikali ya CCM haiwezi kuacha wananchi wakiburuzwa na halmashauri nchini kwa kuwatoza ushuru usio stahili na kusababisha chuki baina ya wananchi ya na serikali yao njema sana
Mwanri alitoa kauli hiyo huku akisimamiwa na Katibu wa uenezi na Itikadi wa CCM taifa Mhe. Aggrey Mwanri aliyemtaka kueleza kwa nini wananchi wanalalamika kuwa wanatozwa ushuru wa vitumbua na kupelekea hata kidogo wanachokipata kinaenda halmashauri pamoja na malalamiko ya kutozwa gharama za matibabu wanawake wajawazito na watoto licha ya serikali kutangaza kuwa matibabu ni bure kwa wajwazito na watoto.
Kuhusu gharama za matibabu Mhe. Mwanri alisema wananchi watoe taarifa pindi wanabaini kuwepo kwa mtumishi wa afya asiye mwaminifu ili achukuliwe hatua haraka ambapo aliwaagiza wakuu wa wilaya kushughulikia suala hilo kwa makini sana ili wananchi wasiendelee kuhangaikia matibabu
“Wananchi naomba mnielewe, akinamama wajawazito, watoto wenye umri chini ya miaka mitano hawatakiwi kuchangia chochote katika matibabu pindi wanapohitaji huduma katika vituo vya tiba vyote hapa nchini vinavyomilikiwa na serikali, inapotokea mnadaiwa wapeni taarifa wakuu wa wilaya ili nao wachukue hatua haraka na kuwashughulikia wakurugenzi na watumishi wao wenye tabia hiyo mbaya.” Alisema Mhe. Mwanri
Alisema maagizo hayo atayafuatilia kwa karibu kwani ndani ya kipindi cha miezi miwili ijayo atahakikisha anarejea kufanya ziara katika halmashauri za mikoa ya Rukwa na Katavi ili kuangalia utekelezaji wa maagizo hayo na itakapobainika kuwa hakuna utekelezaji atachukua hatua stahili.
Baadhi ya watendaji wa halmashauri za Sumbawanga na Mpanda walipoulizwa kuhusu utekelezaji wa maagizo hayo walionesha kubeza kauli ya Mhe. Mwanri kwa madai kuwa ni ya kisiasa zaidi.
Wachuuzi nao walisema katika siku nne za utekelezaji wa agizo hilo bado ameendeelea kuchangishwa na mawakala waliowekwa na halmashauri kukusanya ushuru kwa madai kuwa wao wametumwa na wakurugenzi kwa maadishi hivyo huyo aliyekataza aandike barua ya kukataza
Wakurugenzi waliohojiwa na mwandishi wa habari hii walikataa kutoa ushirkiano na kugoma kata kata kuzungumzia ushuru wa wachuuzi wadogo wadogo

USHURU WA VITUMBUA NA AGIZO LA TAMISEMI 

MPANDA MJINI





SENSA YA WATU NA MAKAZI MKOA KATAVI






JULAI 20, 2012     ---- KATAVI 

Hivi Tanzania ni Shamba la Bibi kweli?????????????????? 

WACHINA WAINGIA HADI NATIONAL PARK KUCHIMBA MADINI,

WADAI NI ENEO LAO SAHIHI, WATOA RAMANI YA KUCHONGA

MKUU WA MKOA ASEMA JAMBO JUU YAO



 

Na Willy Sumia, Katavi
MKUU wa mkoa wa Katavi, Dr Rajabu Rutengwe amewataka wawekezaji wanaokwenda kuwekeza katika sekta ya madini katika mkoa wa Katavi wawasiliane na ofisi za serikali mkoani humo kabla ya kuingia katika mikataba ya uendeshaji wa shughuli za uzalishaji katika maeneo husika
Wito huo umetolewa na mkuu kufuatia utapeli waliofanyiwa wawekezaji wa kutoka nchi ya China na kampuni yao ya Red Ore Mining Co. Ltd ya DSM na kupelekwa eneo la pori la akiba la Luafi mpakani na hifadhi ya Taifa ya Katavi kwa ajili ya kuendesha shughuli za uchimbaji wa madini ya chuma na shaba.
Taarifa zinasema kuwa kampuni hiyo yenye makao yake jijini DSM inayoendeshwa na Raia wa nchi ya China ilianza shughuli katika eneo hilo katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita hadi jana walipofika askari wa wanyamapori wa Pori la akiba la Rukwa / Lukwati/ Luafi na hifadhi ya Taifa ya Katavi kuwaamuru waondoke katika eneo hilo kwakuwa ni eneo lilitengwa kwa ajili ya uhifadhi wa mazingira na ustawi wa wanyama pori.
Askari hao walipozungumza na waandishi wa habari walisema kuwa awali walipowakuta raia hao wa China waliweza kuwahoji na kubaini kuwa walikuwa wameingizwa eneo hilo kimakosa na ofisi ya hifadhi hiyo iliwaandikia barua yenye Kumb Namba RLLGR/LGR.1/72/14 ya tarehe 06/06/2012 iliyokuwa akiwapa amri ya kuondoka eneo ndani ya siku saba tangu tarehe ya barua hiyo lakini hawakuweza kutekeleza agizo hilo
Askari hao wa wanyamapori walisema kutokana na kushindwa kutii agizo hilo waliamua kufika eneo husika kuwachukua viongozi wa kampuni hadi ofisi ya Mkuu wa mkoa kwa maamuzi zaidi kwani walibaini kuwa walipewa taarifa za uongo na mtu aliyewauzia hilo eneo kwani hilo eneo na eneo lisilotakiwa kufanyiwa shughuli yoyote ile
Walisema hata barua walizojibiwa na Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii yenye kumbukumbu namba HB 178/286/01/102 iliyosainiwa na ndugu J. Muya kwa niaba ya Katibu mkuu wa wizara hiyo ya tarehe 20/06/2012 pamoja na ile iliyotoka kwa wakala wa misitu Tanzania (TFS) yenye kumbukumbu namba TFSC.166/286/01/29 ya tarehe 25 Juni, 2012 ikieleza kuwa eneo hilo waliloomba kwa barua siyo eneo linaloruhusiwa kwa kufanya shughli yoyote ya kibinadamu isipokuwa kwa utafiti wa mafuta, gesi au madini ya uraniamu tu
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao na Wachina wamiliki wa Kampuni ya RedOre Mining Co. Ltd, mkuu wa mkoa wa Katavi, Dr Rajabu Rutengwe alisema kuwa katika mazungumzo na wawekezaji hao alibaini kuwa walitapeliwa na mtu aliyewauzia eneo hilo baada ya kuona kuwa eneo hilo haliruhusiwi kwa shuguli yoyote.
Alisema kutokana na hali iliyojitokeza inabidi sheria ichukue mkondo wake na huku wawekezaji hao wakiwa nje ya hifadhi kwani tayari eneo hilo limeshaharibiwa na kuingiza hasara kubwa Taifa hivyo ili kuepusha malalamiko ya kuwa wageni hao wameonewa na Watanzania hivyo mahakama ndiyo itakayoamua nani kakosea, wapi na namna gani kakosea ili kulinda utawala bora.
Akizungumzia juu ya aliyewatapeli wawekezaji hao mkuu wa mkoa alisema wao ndio wanamfahamu aliyewauzia na wanafahamu watampata wapi hivyo ni jukumu la wawekezaji kumtafuta wamuawajibishe kwa kuwatapeli  ambapo mkuu huyo wa mkoa alitoa ushauri kwa wawekezaji wengine wasiingie mkataba na mmiliki yeyote wa ardhi katika mkoa wa Katavi bila kuwasiliana na Halmashauri au ofisi ya madini ya kanda ya Magharibi iliyoko mjini Mpanda kwa ushauri na msaada wa taarifa za eneo husika.  
 











































 

RAIS KIKWETE ATAKA KUFUNGWA KWA KAMBI ZA WAKIMBIZI WA BURUNDI, WAKAZI WA MKOA WA KATAVI WAFURAHIA KAULI YA RAIS

Wakimbizi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Serikali itahakikisha kambi za wakimbizi wa Burundi katika Tanzania zinafungwa na wakimbizi wanarudi kwao kwa sababu hawana tena sababu ya kuendelea kuwa wakimbizi katika Tanzania.
Amesema kuwa hali ya usalama, amani na utulivu katika Burundi ni mazingira mwafaka kwa kila Mrundi kuishi kwao badala ya kuendelea kuwa mkimbizi katika Tanzania.
Rais Kikwete ameyasema hayo leo, Alhamisi, Julai 19, 2012, wakati alipokutana na kuzungumza na Sheikh Mohammed Rukara, Mjumbe Maalum wa Rais wa Burundi, Mheshimiwa Pierre Nkurunziza, Ikulu, mjini Dar es salaam. Sheikh Rukara pia ni Mkuu wa Uchunguzi wa Malalamiko ya Wananchi (Ombudsman) katika Burundi.
“Tutashughulika na wakimbizi kwa sababu hawana tena sababu ya kubakia Tanzania kama wakimbizi. Tutahakikisha kuwa kambi za wakimbizi wa Burundi katika Tanzania zinafungwa,” Rais Kikwete amemwambia Sheikh Rukara.
Rais pia ameisifu Burundi kwa mafanikio makubwa ambayo yamepatikana tokea amani irejee katika nchi hiyo jirani na hasa tokea Rais Nkurunziza alipoingia madarakani miaka saba iliyopita.
“Mmefanya kazi kubwa na nzuri sana katika ujenzi wa barabara, ujenzi wa shule, ujenzi wa vyuo vya elimu ya juu na zaidi ya yote ujenzi wa amani na umoja. Ni vyema kuwa macho na kuendelea kulinda amani,” amesema Rais.
Sheikh Rukara amemshukuru tena Rais Kikwete kwa mchango wake mkubwa katika kutafuta amani ya Burundi. “Mheshimiwa Rais ulituokoa sana,” amesema Sheikh Rukara.
Miongoni mwa mambo mengine, katika salamu zake maalum, Rais Nkurunziza amemshukuru Rais Kikwete kwa kuhudhuria Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Burundi zilizofanyika mjini Bujumbura Julai 2, mwaka huu, 2012.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
19 Julai, 2012
Na Willy Sumia, Katavi
MKUU wa mkoa wa Katavi,, Dr Rajabu Rutengwe hivi karibuni alisisitiza msimamo wa mkoa wa Katavi juu ya mustakabali wa wakimbizi toka nchi ya Burundi waishio katika makazi ya wakimbizi hao ya Mishamo na Katumba katika wilaya za Mpanda na Mlele mkoa wa Katavi.
Dr Rajabu ambaye awali alikuwa mkuu wa wilaya ya Mpanda kipindi hico makambi yote hayo yakiwa katika wilaya ya Mpanda kabla ya kugawanywa alisema kuwa msimamo wa mkoa wa Katavi juu ya suala la wakimbizi ni kuwa hakuna haja ya kujenga Burundi ndani ya Katavi na endapo itabidi wabaki Tanzania basi uandaliwe utaratibu wa kupelekwa mikoa mingine kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo suala zima la usalama
m
Mwishoni mwa wiki iliyopita wananchi wa mjini Mpanda waliitaka serikali kutoa kauli jyy ya hatima ya makazi ya wakimbizi Katumba na Mishamo kutokana na taarifa za kuwa kuna uwezekano wa wakimbizi hao kupewa uraia na kubaki katika makambi hayo hayo katika mkoa wa Katavi.
Akijibu hoja hiyo katika mkutano wa hadhara mjini Mpanda mwishoni mwa wiki, Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa nchini, Mhe. Aggrey Mwanri alisema suala hilo liko katika maamuzi ya Kitaifa kwani mkoa ulishamaliza kazi yake na kutoa msimamo kuwa hakuna haja ya kujenga Burundi ndani ya Katavi.
Mhe Mwanri alisema eneo lililokuwa likitumika kama kambi za wakimbizi litatafutiwa shughuli nyingne ya uzalishaji ikiwa ni pamoja na kuangalia uwezekano wa kuweka mwekezaji atakayeliendeleza kwa kuweka vitega uchumi ili kuongeza uzalishaji wa chakula sambamba na kutoa fursa kwa Chuo Kikuu cha kilimo cha Katavi (KUA) kutumia eneo hilo kama eneo la masomo kwa vitendo
Miezi miwili iliyopita mkuu wa mkoa wa Katavi Dr Rajabu Mtumwa Rutengwe alipotakiwa kutoa msimamo wa Mkoa juu ya mustaabali wa wakimbizi katika mkoa wake alipotembelewa na waandishi wa habari ofisini kwake alisema kuwa kwa sababu za kiusalama asingependa kujenga Burundi ndani ya Katavi
"Kutokana na uzoefu wangu kwa sababu nimekaa Mpanda awali kama Mkuu wa wilaya na sasa Mkuu wa Mkoa, ninachoweza kusema ni kuwa suala hilo liko ngazi za juu kwa maamuzi na utekelezaji, lakini msimamo wangu kama mkuu wa mkoa na msimamo wa mkoa wa Katavi ni kuwa hatuhitaji kujenga Burundi ndani ya Katavi, ni kwa sababu za kiusalama na zingine za kijamii" alisema Dr Rutengwe
Baadhi ya wananchi waliohojiwa na mwandishi wa habari mara baada ya kupata taarifa ya Mhe Rais jana alipokuwa akizungumza na ugeni toka Burundi walisema huo ndio uamuzi waliokuwa wakiusubiri toka kwa viongozi wakuu wa nchi akiwamo Mhe, Rais kwani mkoa ulishatoa maamuzi na wasinependa kutolewa maamuzi mengine nje ya yale waliyonayo viongozi wa mkoa wa Katavi.
 
ZIARA YA IDARA YA SIASA, ITIKADI NA UENEZI CCM TAIFA RUKWA NA KATAVI JULAI 13-14, 2012








Na Willy Sumia, Katavi
SERIKALI imepiga marufuku kwa halmashauri za manispaa, miji na wilaya nchini kuwatoza ushuru wachuuzi wadogowadogo wanaotafuta mahitaji ya kujikimu kupitia biashara ndogondogo.
Agizo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki na Naibu waziri kutoka ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa nchini, Mhe. Aggrey Mwanri alipokuwa katika ziara ya siku mbili katika mikoa ya Rukwa na Katavi kuelezea utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2012/15
Naib u waziri Mwanri alisema hivi sasa serikali imerejesha utaratibu wa kupeleka ruzuku katika halmashauri zote nchini kuziba pengo lilitokana na kufuta ushuru mdogo kwa wachuuzi wadogo wadogo wanaoendesha biashara za kujikimu kimaisha na hivyo hakuna halmashauri itakayosingizia kuwa ushuru mdogo ni sehemu ya vyanzo vya mapato ya ndani
Akihutubia katika mikutano ya hadhara mjini Sumbawanga na Mpanda Mhe. Mwanri alisema hakuna kuwatoza ushuru wauza vitumbua, wauza mchicha, nyanya, vitunguua vya mafungu, auza dagaa za mafungu na wanaouza samaki wa kukaanga katika sinia au nyungo ambao wanakuwa wachuuzi na siyo wauzaji wakubwa.
Alisema wale wanaopeleka mizigo sokoni kwa ujazo mkubwa kama vile wanakodisha fuzo na vyombo vingine vya busafirishaji watozwe ushuru kama kawaida isipokuwa wachuuzi wadogo wadogo wanaouza bidhaa ili wapate pesa ya mafuta ya taa, kibaba kimoja cha mafuta ya kula na chumvi hao waachwe mara moja wasitozwe ushuru
“Nakuagiza mkurugenzi, kuanzia kesho hakuna kumtoza ushuru mama muuza vitumbua, muuza mafungu ya mchicha, anayepanga nyanya za mafungu, muuza samaki wa kukaanga na wengine kama hao, mwiko kutoza ushuru walalahoi, ukitaka nishuke na wewe tangu hapo hadi chini endelea kutooza ushuru walalahoi, itakuwa nginja nginja na wewe mpaka kieleweke” alisema Mhe. Mwanri
Alisema serikali ya CCM haiwezi kuacha wananchi wakiburuzwa na halmashauri nchini kwa kuwatoza ushuru usio stahili na kusababisha chuki baina ya wananchi ya na serikali yao njema sana
Mwanri alitoa kauli hiyo huku akisimamiwa na Katibu wa uenezi na Itikadi wa CCM taifa Mhe. Aggrey Mwanri aliyemtaka kueleza kwa nini wananchi wanalalamika kuwa wanatozwa ushuru wa vitumbua na kupelekea hata kidogo wanachokipata kinaenda halmashauri pamoja na malalamiko ya kutozwa gharama za matibabu wanawake wajawazito na watoto licha ya serikali kutangaza kuwa matibabu ni bure kwa wajwazito na watoto.
Kuhusu gharama za matibabu Mhe. Mwanri alisema wananchi watoe taarifa pindi wanabaini kuwepo kwa mtumishi wa afya asiye mwaminifu ili achukuliwe hatua haraka ambapo aliwaagiza wakuu wa wilaya kushughulikia suala hilo kwa makini sana ili wananchi wasiendelee kuhangaikia matibabu
“Wananchi naomba mnielewe, akinamama wajawazito, watoto wenye umri chini ya miaka mitano hawatakiwi kuchangia chochote katika matibabu pindi wanapohitaji huduma katika vituo vya tiba vyote hapa nchini vinavyomilikiwa na serikali, inapotokea mnadaiwa wapeni taarifa wakuu wa wilaya ili nao wachukue hatua haraka na kuwashughulikia wakurugenzi na watumishi wao wenye tabia hiyo mbaya.” Alisema Mhe. Mwanri
Alisema maagizo hayo atayafuatilia kwa karibu kwani ndani ya kipindi cha miezi miwili ijayo atahakikisha anarejea kufanya ziara katika halmashauri za mikoa ya Rukwa na Katavi ili kuangalia utekelezaji wa maagizo hayo na itakapobainika kuwa hakuna utekelezaji atachukua hatua stahili.
Baadhi ya watendaji wa halmashauri za Sumbawanga na Mpanda walipoulizwa kuhusu utekelezaji wa maagizo hayo walionesha kubeza kauli ya Mhe. Mwanri kwa madai kuwa ni ya kisiasa zaidi.
Wachuuzi nao walisema katika siku nne za utekelezaji wa agizo hilo bado ameendeelea kuchangishwa na mawakala waliowekwa na halmashauri kukusanya ushuru kwa madai kuwa wao wametumwa na wakurugenzi kwa maadishi hivyo huyo aliyekataza aandike barua ya kukataza
Wakurugenzi waliohojiwa na mwandishi wa habari hii walikataa kutoa ushirkiano na kugoma kata kata kuzungumzia ushuru wa wachuuzi wadogo wadogo


















































 

May 25, 2012


UWEKEZAJI KWENYE MAENEO YA MALIAKALE UNARUHUSIWA

hapa ni Ismila Stone Age Iringa
TAARIFA KWA UMMA
UWEKEZAJI KWENYE MAENEO YA MALIAKALE UNARUHUSIWA
Wizara ya Maliasili na Utalii imefafanua kuwa kwa mujibu wa Sera ya Malikale ya mwaka 2008 (Kifungu cha 4.5 na 46), wananchi, taasisi mbalimbali, pamoja na wadau wengine wa uhifadhi wanaruhusiwa kumiliki, kulinda, kuhifadhi na kuendeleza urithi wa utamaduni nchini kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho kwa sababu za mafunzo, historia na utalii. Sera pia inaruhusu uwekezaji katika maeneo ya malikale ambao unalenga kuhifadhi na kutumia rasilimali za malikale kama vivutio vya utalii.
Ufafanuzi huu umetolewa kufuatia habari iliyoandikwa na gazeti moja la kila siku kuhusu mwekezaji kumilikishwa isivyo halali eneo lenye magofu ya kihistoria la kisiwa cha Chole kilichopo wilayani Mafia ambayo sasa yanatumika kama sehemu ya hoteli ya kitalii.
Wizara kupitia Idara ya Mambo ya Kale inatambua kuwa magofu ya kihistoria katika kisiwa cha Chole ni Kumbukumbu za Urithi wa Utamaduni yenye umuhimu kitaifa na kimataifa na Magofu haya yanalindwa na Sheria ya Mambo ya Kale Na. 10 ya mwaka 1964 na marekebisho yake Na 22 ya mwaka 1979. Idara inawajibika kusimamia uhifadhi na uendelelezaji wake kulingana na kanuni na miongozo ya uhifadhi na uendelelezaji.
Wizara inasisitiza kuwa siyo maeneo yote ya urithi wa utamaduni yanasimamiwa na Idara ya Mambo ya Kale moja kwa moja. Maeneo ya urithi wa utamaduni yenye sifa za kitaifa ni mengi lakini 12 tu ndiyo yanayomilikiwa na Serikali Kuu na kuendelezwa na Idara ya Mambo ya Kale. Maeneo yaliyo mengi yanamilikiwa na watu binafsi, taasisi za umma na binafsi na vijiji au wilaya. Kwa mfano, Magofu ya Chole, Mafia hayapo chini ya umiliki wa Idara ya Mambo ya Kale moja kwa moja bali yapo chini ya umiliki wa wilaya na serikali ya kijiji cha Chole.
Hivyo Wizara haijahusika kuimilikisha kampuni ya “Chole Mjini Conservation and Development Company Limited” eneo lenye magofu ya kihistoria la Chole wala kutoa kibali cha kujenga hoteli katika kijiji hicho.
Hata hivyo, kutokana na taratibu zilizopo Wizara ilihusika kutoa kibali cha ukarabati wa magofu hayo (Kumb. Na. EA. 270/297/01/33) baada ya mmiliki kutimiza masharti ya kuwasilisha taarifa zifuatazo:-
· Uhalali wa umiliki wa jengo au eneo;
· Taarifa ya kitalaamu inayoonyesha hali halisi ya jengo na mahitaji ya kufanyia ukarabati au mabadiliko ya matumizi;
· Michoro/ramani za jengo linavyoonekana sasa na ramani zinazoonyesha maboresho yatakayofanyika wakati ya ukarabati; na
· Albamu ya picha inayoonyesha hali ya jengo kwa sasa na maeneo ambayo yanahitaji kukarabatiwa au kuboreshwa.
Baada ya masharti kutimizwa Chole Mjini Conservation and Development Company Limited ilipata kibali cha ukarabati kilichoambatana na miongozo ya uhifadhi ambayo mwekezaji alitakiwa kuifuata, na kazi ya ukarabati ilifanyika chini ya usimimamizi wa Wizara. Wizara ilihusika ili kuhakikisha kuwa ukarabati unafanyika bila kubadilisha mwonekano wa majengo husika uliokuwepo hapo awali.
Wizara inawahamasisha watu binafsi, mashirika na asasi mbalimbali kuwekeza katika sekta ya malikale mradi taratibu za kisheria za kupata eneo husika na kulikarabati zifuatwe. Uwekezaji huo ni utekelezaji wa Sera ya Malikale ya mwaka 2008 inayotaka Idara ya Mambo ya Kale kushirikikisha wadau katika kuendeleza maeneo ya malikale.

[MWISHO]
George Matiko
MSEMAJI
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
25/05/2012

BEI YA MADAFU LEO BONGO LEO MEI 25, 2012

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXjOerFxr-zoj5qvTACOQeuM2CcEyLuDJQPkGsLqWKvHOBhh7qU5s_-c3Al6K3pQ184piIwbqJtImqGudD_QhA-BMhSeVKBFJrNjfDhKOZC786tPR_b8Oi0MJQ9nWhx73N08YzWtS0_oo/s640/blogger-image--1592252031.jpg  

 

mei 5, 2012


NJAMA ZA KUHAKIKISHA PINDA ANANG'OKA KATIKA KITI CHA UWAZIRI MKUU ZALETA MABADILIKO KATIKA BARAZA LA MAWAZIRI.

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI HILI HAPA , LUKUVI APETA , MAKALA ,Dkt MAHENGE ,DKT MGIWA AULA

Rais Dkt Jakaya Kikwete

PANGUA YA MAWAZIRI MWEZI MEI 2012 HII HAPA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI MAWAZIRI

1. OFISI YA RAIS Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Ndugu Stephen M. Wasira, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora) Ndugu George Mkuchika, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI) Ndugu Celina Kombani, Mb., 2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO) Ndugu Samia H. Suluhu, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA) Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb., 3. OFISI YA WAZIRI MKUU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Ndugu Mary M. Nagu, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Hawa Ghasia, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Ndugu William V. Lukuvi, Mb., 4. WIZARA Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ndugu Samuel J. Sitta, Mb., Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb., Waziri wa Ujenzi Dr. John P. Magufuli, Mb., Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb., Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb., Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ndugu Sophia M. Simba, Mb., Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Bernard K. Membe, Mb., Waziri wa Katiba na Sheria Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb., waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb., Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dr. David M. David, Mb., Waziri wa Kazi na Ajira Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb., Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame M. Mbarawa, Mb., Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb., Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe, Mb., Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum Prof. Mark Mwandosya, Mb., Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Eng. Christopher Chiza, Mb., Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe, Mb., Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dr. Fenella E. Mukangara, Mb., Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu Khamis Kagasheki, Mb., Waziri wa Viwanda na Biashara Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb., Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa, Mb., Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo, Mb., 5. NAIBU MAWAZIRI OFISI YA RAIS HAKUNA NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Charles Kitwanga, Mb., 7. OFISI YA WAZIRI MKUU Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb., Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Aggrey Mwanry, Mb., 8. WIZARA MBALIMBALI Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb., Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Ndugu Adam Malima, Mb., Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ndugu Pereira A. Silima, Mb., Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Ndugu Gregory G. Teu, Mb., Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb., Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb., Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb., Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb., Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb., Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb., Naibu Waziri wa Ujenzi Ndugu Gerson Lwenge, Mb., Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb., Naibu Waziri wa Nishati na Madini Ndugu George Simbachawene, Mb., Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Ndugu January Makamba, Mb., Naibu Waziri wa Uchukuzi Dr. Charles J. Tizeba, Mb., Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndugu Amos Makala, Mb., Naibu Waziri wa Maji Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb., Naibu Waziri Nishati na Madini Ndugu Stephen Maselle, Mb., Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb., Naibu Waziri wa Fedha Ndugu Janet Mbene, Mb., Naibu Waziri wa Fedha Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb., Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu. Dar es Salaam. 4 Mei, 2012

Mbunge wa jimbo la Ismani Iringa Wiliam Lukuvi ambaye ameachwa tena katika nafasi yake ya uwaziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa bunge
  mbunge wa jimbo la Makete mkoa mpya wa Njombe Eng. Dr. Binilith Mahenge, (kushoto) ambaye ameteuliwa kuwa naibu waziri wa maji akiwa na mkuu wa wilaya Dkt Norman Sigalla

Mbunge wa jimbo la Kalenga Dkt Wiliam Mgimwa aliyeteuliwa kuwa waziri wa fedha na uchumi leo ,hapa akisaini hundi kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari Lyandembela jimboni kwake
  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI MAWAZIRI 1. OFISI YA RAIS Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Ndugu Stephen M. Wasira, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora) Ndugu George Mkuchika, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI) Ndugu Celina Kombani, Mb., 2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO) Ndugu Samia H. Suluhu, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA) Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb., 3. OFISI YA WAZIRI MKUU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Ndugu Mary M. Nagu, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Hawa Ghasia, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Ndugu William V. Lukuvi, Mb., 4. WIZARA Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ndugu Samuel J. Sitta, Mb., Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb., Waziri wa Ujenzi Dr. John P. Magufuli, Mb., Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb., Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb., Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ndugu Sophia M. Simba, Mb., Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Bernard K. Membe, Mb., Waziri wa Katiba na Sheria Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb., waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb., Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dr. David M. David, Mb., Waziri wa Kazi na Ajira Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb., Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame M. Mbarawa, Mb., Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb., Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe, Mb., Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum Prof. Mark Mwandosya, Mb., Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Eng. Christopher Chiza, Mb., Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe, Mb., Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dr. Fenella E. Mukangara, Mb., Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu Khamis Kagasheki, Mb., Waziri wa Viwanda na Biashara Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb., Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa, Mb., Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo, Mb., 5. NAIBU MAWAZIRI OFISI YA RAIS HAKUNA NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Charles Kitwanga, Mb., 7. OFISI YA WAZIRI MKUU Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb., Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Aggrey Mwanry, Mb., 8. WIZARA MBALIMBALI Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb., Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Ndugu Adam Malima, Mb., Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ndugu Pereira A. Silima, Mb., Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Ndugu Gregory G. Teu, Mb., Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb., Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb., Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb., Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb., Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb., Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb., Naibu Waziri wa Ujenzi Ndugu Gerson Lwenge, Mb., Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb., Naibu Waziri wa Nishati na Madini Ndugu George Simbachawene, Mb., Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Ndugu January Makamba, Mb., Naibu Waziri wa Uchukuzi Dr. Charles J. Tizeba, Mb., Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndugu Amos Makala, Mb., Naibu Waziri wa Maji Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb., Naibu Waziri Nishati na Madini Ndugu Stephen Maselle, Mb., Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb., Naibu Waziri wa Fedha Ndugu Janet Mbene, Mb., Naibu Waziri wa Fedha Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb., Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu. Dar es Salaam. 4 Mei, 2012

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI MAWAZIRI 

1. OFISI YA RAIS Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Ndugu Stephen M. Wasira, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora) Ndugu George Mkuchika, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI) Ndugu Celina Kombani, Mb., 2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO) Ndugu Samia H. Suluhu, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA) Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb., 3. OFISI YA WAZIRI MKUU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Ndugu Mary M. Nagu, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Hawa Ghasia, Mb., Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Ndugu William V. Lukuvi, Mb., 4. WIZARA Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ndugu Samuel J. Sitta, Mb., Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb., Waziri wa Ujenzi Dr. John P. Magufuli, Mb., Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb., Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb., Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ndugu Sophia M. Simba, Mb., Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Bernard K. Membe, Mb., Waziri wa Katiba na Sheria Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb., waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb., Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dr. David M. David, Mb., Waziri wa Kazi na Ajira Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb., Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame M. Mbarawa, Mb., Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb., Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe, Mb., Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum Prof. Mark Mwandosya, Mb., Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Eng. Christopher Chiza, Mb., Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe, Mb., Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dr. Fenella E. Mukangara, Mb., Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu Khamis Kagasheki, Mb., Waziri wa Viwanda na Biashara Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb., Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa, Mb., Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo, Mb., 5. NAIBU MAWAZIRI OFISI YA RAIS HAKUNA NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Charles Kitwanga, Mb., 7. OFISI YA WAZIRI MKUU Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb., Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Ndugu Aggrey Mwanry, Mb., 8. WIZARA MBALIMBALI Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb., Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Ndugu Adam Malima, Mb., Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ndugu Pereira A. Silima, Mb., Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Ndugu Gregory G. Teu, Mb., Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb., Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb., Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb., Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb., Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb., Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb., Naibu Waziri wa Ujenzi Ndugu Gerson Lwenge, Mb., Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb., Naibu Waziri wa Nishati na Madini Ndugu George Simbachawene, Mb., Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Ndugu January Makamba, Mb., Naibu Waziri wa Uchukuzi Dr. Charles J. Tizeba, Mb., Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndugu Amos Makala, Mb., Naibu Waziri wa Maji Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb., Naibu Waziri Nishati na Madini Ndugu Stephen Maselle, Mb., Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb., Naibu Waziri wa Fedha Ndugu Janet Mbene, Mb., Naibu Waziri wa Fedha Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb., Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu. Dar es Salaam. 4 Mei, 2012


0 Maoni:

MAHAKAMA YATENGUA KITENDAWILI CHA HATIMA YA MBUNGE

MAHAKAMA kuu kanda ya Sumbawanga imefuta matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Sumbawanga mjini uliofanyika Oktoba 2010 kutokana na kukiukwa kwa baadhi ya taratibu za uchaguzi zilizoathiri matokeo
Hukumu hiyo imetolewa na jaji wa mahakama kuu kanda ya Sumbawanga, Mhe Bethuel Mmila katika hukumu ya kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyowasilishwa mahakamani hapo na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kikilalamikia kukiukwa kwa baadhi ya taratibu za uchaguzi huo na kupelekea matokeo yasiyo ya haki.
Katika hukumu hiyo iliyochukua kwa kipindi cha saa tatu na Jaji wa makama hiyo, Bethuel Mmila imeeleza kuwa katika kusikiliza shauri hilo mahakama imepokea vielelezo na ushahidi ulioweza kuthibitisha kuwa baadhi ya taratibu za uchaguzi zilikiukwa na hivyo kuathiri matokeo ya uchaguzi huo
Hukumu hiyo imesema kuwa makama imetengua ubunge wa Aeshi Hilary wa CCM aliyepewa ushindi katika uchaguzi wa Oktoba 2010 na kuwa mbunge wa jimbo la Sumbawanga mjini na kuwa kuanzia leo Aprili 30, 2012 siyo mbunge wa jimbo la Sumbawanga mjini katika mkoa wa Rukwa
Kutokana na matokeo hayo jimbo la Sumbawanga mjini liko wazi hadi taratibu za uchaguzi zitakapokamilika ambapo katika hatua nyingine shangwe zimelipuka katika manispaa ya Sumbawanga baada ya kutangazwa hukumu ya kesi hiyo ambapo vijana na baadhi ya watu wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa chama cha CHADEMA  wamekuwa wakipiga kelele na wengine kukimbiza pikipiki mitaani wakishangilia hukumu hiyo
Pamoja na shangwe hizo hali ya mji wa Sumbawanga imeelezewa kuwa salama kabisa licha ya kuwepo kwa shamrashamra zilizojitokeza ambazo zimeelezewa kuwa ni za kusherehekea hukumu hiyo na imeelezewa kuwa haina athari yoyote kiusalama kwa watu wengine wanaoendesha shughuli mbalimbali za kijamii mjini hapo.
Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Kanali John Anthony Mzurikwao amesema hali ni shwari na ameliagiza jeshi la polisi kudhibiti vibaka wanaoweza kujipenyeza katika shamra shamra hizo kwa lengo la kuiba au kuvunja mali za wananchi.

BARAZA LA MADIWANI WAWATUNISHIA MSULI WATAAMU

BARAZA la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa
wamezigomea taarifa zote za kamati za halmashauri hiyo jambo lililosababisha kikao cha baraza la madiwani  wa halmashuri hiyo kuvunjika.


Aidha mara baada ya kuvunjika kwa kikao hicho cha baraza la madiwani kilichokuwa kikifanyika  April 27, 2012  madiwani hao pia wamemuandikia barua  mwenyekiti wa halmashauri hiyo wakimtaka mwenyekiti huyo kuridhia  kuitishwa kikao cha kujadili mapungufu  mbalimbali  ya kiutendaji yaliyopo katika menejimenti ya halmashuari hiyo.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Bw Peter Mizinga  licha ya kukiri kuwepo kwa tukio hilo la madiwani kugomea taarifa zote amezitaja  taarifa za kamati zote zilizogomewa kuwa ni kamati ya Fedha, kamati ya Elimu Afya na Maji,
Kamati ya Uchumi, Mazingira   na ujenzi pamoja na Kamati ya Ukimwi.

Bw Mizinga amefafanua kuwa tukio hilo la kugomewa kwa taarifa hizo za kamati limefuatia tafsiri ya  madiwani hao ya kuwa wamekuwa wakipuuzwa na watendaji hao katika maazimio mbalimbali yanayotolewa katika mabaraza ya madiniwani kutokana na maazimio hayo kutotekelezwa  katika kipindi cha miezi mitatu mfululizo na kutokuandikwa kwa katika taarifa
zozote za vikao hivyo.

Amesema kuwa kumekuwepo na tabia endelevu inayofanywa na menejmenti hiyo ya halmashauri ya wilaya ya Nkasi ya kupuuza maazimio ya vikao jambo linaloonyesha ya kuwepo na uzembe wa wazi wa watendaji hao ambao ni wakuu wa idara mbali mbali za Halmashauri hiyo.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa halmashauri ya wilaya ya Nkasi amesema kuwa mpaka sasa amekwisha pokea barua toka kwa madiwani hao ikimtaka aridhie kuwepo kwa kikao cha madiwani  hao  cha kujadili  mapungufu yaliyopo katika menejimenti nzima ya halmashauri yake

Alipohojiwa kwa njia ya simu  kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw Emmanuel Kushoka alikataa kuwepo kwa tukio hilo la madiwani kugomea taarifa na kusema kuwa ‘kikao kilifanyika isipokuwa madiwani hao wameshauri kuwepo na marekebisho katika baadhi ya taarifa.

 KAMA UCHAFU HUU UTAACHWA KIPINDU PINDU NI HAKI YA WALAJI WA SOKO HILI

April 20, 2012



HOJA YA MH. ZITTO KABWE YA KUPIGA KURA ZA KUTOKUWA NA IMANI NA WAZIRI MKUU YAPIGWA CHINI NA KANUNI ZA BUNGE



Taarifa za hivi punde kutoka Bungeni Mjini Dodoma,zinaeleza kuwa Kusudio la Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe la kutaka kupiga kura za kuanzishwa kwa mjadala wa kutokuwa na imani na Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda,limepigwa chini na Spika wa Bunge,Mh. Anne Makinda.



Akisoma kanuni za Bunge,Mh. Spika alisema kwa mujibu wa kanuni za Bunge na Katiba ya Nchi,kusudio la kutaka kumuondoa Madarakani Waziri Mkuu kwa kupiga kura ya kutokuwa na Imani nae ambayo ni taarifa ya maandishi inapaswa kuwasilishwa kwake siku 14 kabla ya siku husika.



Hivyo kwakuwa ofisi yake haijapata taarifa ya maandishi ju ya zoezi hilo,basi zoezi hilo moja kwa moja litakuwa ni batili, na kwasababu kikao hicho cha Bunge kinatarajiwa kufungwa siku ya jumatatu,basi hakutakuwa na uwezekano wa zoezi hilo kukamilika.

Awali Mbunge wa Jimbo la Bumbuli,Mh. January Makamab aliomba muongozo wa Spika kuhusu jambo hilo ndipo Spika,Mh. Anne Makinda akasimama na kutoa ufafanuzi huo.Na www.issamichuzi.blogspot.com 

WAKUVANGA WA ORIJINO KOMEDY APAGAWISHWA NA ULANZI IRINGA

msanii wa Orijino Komedy Bw.Wakuvanga akinywa pombe ya asili ya mkoa wa Iringa Ulanzi eneo la Kihesa mjini Iringa jioni hii
Jasiri haachi asili ama mdharau kwao ni mtumwa ni vigumu sasa na wasanii kupenda pombe za asili kama hivi
Hapa wakipokezana lita ya ulanzi
Wakuvanga akiwa na wadau eneo la Kihesa mjini Iringa huku gari lao likiwa limechafuliwa kwa kuchorwa kwa tope
Wakuvanga akionyesha gari lake lilivyochafuliwa kwa tope