Wednesday, January 15, 2014

FUNGUA www.habarikatavi.wordpress.com

USIPOTEZE MUDA FUNGUA www.habarikatavi.wordpess.com
Katavi

BARAZA la madiwani la Halmashauri ya Mji wa Mpanda Mkoa wa Katavi  limepitisha bajeti ya shilingi Bil 36 katika mapato  yake  ya 2014 na 2015

Kwa mujibu wa ndugu Suleimani Lukanga ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, halmashauri yake inatarajia kujipatia kiasi cha shilingi 36, 229,866,934 katika mwaka wa fedha wa 2014/15.

Lukanga alibainisha  hayo katika kikao  maalumu  cha Baraza  la   Madiwani  kilichofanyika  Jumatano Januari 15, 2014 katika  ukumbi wa  Chuo  Kikuu Huria cha Mkoa wa Katavi mjini Mpanda

Alisema ofisi yake imeandaa Bajeti hiyo kwa kuzingatia mwongozo wa Bajeti ya Taifa ya kuondoa umasikini ambapo kati ya  Fedha  hizo  Sh 8,192, 020,461  ni  mishahara ya watumishi  ruzuku ya kutoka Serikali kuu.

Aidha alisema matumizi  mengine ya fedha za Maendeleo ni  Sh 25,535,581,473 na fedha  za makusanyo ya ndani na makusanyo  ya huduma za afya na  na ada za Sekondari halmashauri hiyo inatarajia kukusana  Sh 1,285,460 

Alisema  pia alimashauri hiyo imeomba  maombi maalumu  nje ya ukomo wa Bajeti  shilingi  3,302 500,000 na kufanya bajeti hiyo kufikia   Sh 39,532,366,934

Alisema Bajeti ya mwaka wa 2013 na 2014  Halmashauri ya mji wa Mpanda iliidhinisha  jumla ya  shilingi  12,833,792,818 lakini hadi kufikia Novemba  2013 Halmashauri ilikuwa imepokea  jumla ya Sh  4,165,656,732 ambazo ni sawa na  asilimia 28  ya Bajeti  iliyoidhinishwa  kwa mwaka wa fedha wa 2013  na 2014-01-15

Aidha  alieleza kuwa  ongezeko hilo la Bajeti  limeongezeka kutokana na ongezeko la  watumishi wa ajira mpya  na ongezeko la miradi ya maendeleo katika kata zote tisa za Halmashauri hiyo  pamoja na huduma mbalimbali

Hata  hivyo Lukanga  alisema  Bajeti ya msimu uliopita ya mapato ya ndani ilikuwa ni  Tsh  Milioni  926,422 wakati msimu wa Fedha wa mwaka huu  mapato ya ndani ni  Tsh Bilioni 1,285,460,000 ambalo ni  sawa la ongezeko la asilimia  38.8  ya Bajeti ya Halmashauri ya msimu uliopita
mwisho

No comments: