Sunday, April 21, 2013

JELA MIAKA 30 KWA KUMBAKA KIKONGWE WA MIAKA 90


JELA MIAKA 30 KWA KUMBAKA KIKONGWE WA MIAKA 90
wacha Mungu wasema tuombe na kufunga
MAHAKAMA ya hakimu mkazi wilaya ya Mpanda mkoani Katavi imemuhukumu kifungo cha miaka thelathini jela Sindembela Msagi (26) baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka kikongwe mwenye umri wa miaka tisini mwenye ugonjwa wa kupooza
Hukumu hiyo iliyotolewa Ijumaa Aprili 19, 2013 na hakimu mfawidhi mkazi wa mahakama hiyo Chiganga Tengwa kufuatia tukio la ubakaji lilitokea Desemba 22, 2012 katika kijiji cha Bulembo katika makazi ya wakambizi ya Katumba wilaya ya Mlele
Awali akitoa maelezo mahakamani hapo mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi, Ally Bwijo alisema kuwa mtuhumiwa alifanya kosa hilo Desemba 22, 2012 majira ya usiku baada ya kumuingilia kikongwe huyo ambaye ni mgonjwa wa kupooza kwa muda mrefu
Aliiambia mahakama kuwa baada ya kumbaka kikongwe huyo mtuhumiwa aliweza kukimbia lakini baada ya wananchi kumuhoji kikongwe huyo aliweza kumtambua kwa sura na jina kwani alikuwa anamfahamu kabla ya tukio hilo la kinyama
Alisema kufuatia maelekezo ya kikongwe aliyefanyiwa unyama huo wananchi kwa kushirikiana na jeshi la polisi waliweza kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha katika vyombo vya sheria kwa hatua zaidi
Akitoa utetezi wake mahakamani hapo Sindembelea Msagi aliiambia mahakama kuwa imuonee huruma kwani alifanya kosa hilo kwa mara ya kwanza na kuwa alishawishiwa na tama ya pesa kutokana na kuwa na  anawategemezi wengi  wanaohitaji pesa za kuwahudumia
Baada ya kupata maelezo ya pande zote hakimu Chiganga Tengwa alisema mahakama yake imeridhishwa bila shaka yoyote na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka na hivyo mtuhumiwa anastahili adhabu
Chiganga alisema kwa kutumia kifungu sha sheria Namba 154 cha makosa ya ubakaji iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 mtuhumiwa atatumikia kifungo cha miaka thelathini jela ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia ya ubakaji