Tuesday, April 30, 2013

MTOTO MIGUU SENTIMITA TANO

Mpanda
MTOTO wa ajabu alizaliwa jana mchana katika hospitali ya wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi akiwa na uzito wa kilogramu  nne, miguu na mikono yenye urefu wa sentimita tano tu na kichwa kikubwa
Taarifa zilizopatikana mara baada ya kuzaliwa mtoto huyo zilidai kuwa mtoto huyo alizaliwa akiwa hai lakini baada ya dakika tano akafariki dunia alikuwa na uzito wa kilogramu nne, miguu yenye urefu wa sentimita tano, mikono ina urefu wa sentimita tano na kichwa kikubwa
Akizungumza hospitalini hapo muuguzi mkuu wa hospitali ya wilaya ya Mpanda, Alexander Gervas Kasagula alisema mama wa mtoto huyo anaitwa Johari Rafaeli (35) mkazi wa mtaa wa Makanyagio mjini Mpanda ambaye alijifungua kwa njia ya upasuaji April 30, 2013 majira ya saa sita na robo mchana.
Kasagula alisema mama huyo alikuwa akipata huduma ya upimaji (kliniki) katika zahanati ya Afya Dispensary iliyoko katika eneo la Makanyagio hadi miezi tisa ilipotimia wakamuelekeza akajifungulie hospitali ya wilaya ingawa hawakuweza kubainisha kama mama huyo alikuwa na tatizo lolote
Alisema baada ya kumpokea mama huyo April 29, 2013 waganga walimpangia kuwa afanyiwe upasuaji mkubwa baada ya kubaini kuwa huyo mama alikuwa na mtoto mkubwa (big baby) hivyo asingeweza kujifungua kwa uwezo wake mwenyewe
Alifafanua kuwa majira ya saa tatu walimuandaa na kumpeleka chumba cha upasuaji na kumfanyia upasuaji ambao ulikamilika majira ya saa sita mchana na kubaini kuwa kiumbe aliyekuwa tumboni alikuwa na hali ya kimaumbile isiyo ya kawaida
Akizungumzia hali ya mama mwenye huyo Kasagula alisema kuwa baada ya upasuaji mama anaendelea vema chini ya uangalizi wa wauguzi katika wodi ya tatu ambayo ni wodi ya wazazi ingawa kiumbe kilifariki dakika tano baada ya kuzaliwa
Ndugu anayemuuguza mama huyo katika hospitali ya wilaya alipoulizwa juu ya maisha ya mgonjwa wake nyumbani licha ya kuomba jina lake lihifadhiwe alisema kuwa mama huyo ana vizazi vitano lakini watoto walio hai wako watatu na wawili wamefariki akiwemo wa jana
Alisema mtoto wa kwanza ni wa kike yupo hai na wa pili ni wa kike na wa tatu ni wa kiume ambapo mama huyo aliweza kupoteza kizazi chake cha nne na cha tano kwani wote walifariki baada ya upasuaji na wote walikuwa wa kiume