Monday, May 6, 2013

PAROKIA TEULE YA MT JOSEPH MFANYAKZI YAPIGWA BOMU

BREAKING NEWS ......

RAIS KIKWETE AMEKATISHA ZIARA YA KISERIKALI NCHINI KUWAIT

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mtawala wa Dola ya Kuwait Amiri Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah wakiingia sehemu ya mapokezi na kukagua gwaride rasmi mara tu alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kuwait City  jana  Mei 5, 2013 tayari kuanza ziara rasmi ya siku mbili katika nchi hiyo,ziara  ambayo  leo  amelazimika  kukatisha na kurejea nchini
......................................................................
Taarifa ambazo zimeufikia mtandao maarufu wa www.francisgodwin.blogspot.com hivi punde zinadai kuwa Rais Dkt Jakaya Kikwete wa Tanzania amekatisha ziara yake ya kiserikali   ya siku mbili nchini Kuwait kufuatia mlipuko wa bomu katika kanisa la Mt Joseph mfanyakazi Arusha ambapo katika tukio  hilo  watu  wawili  hadi  sasa  wanadaiwa  kufa baada ya majeruhi mmoja  kufariki leo .

RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU AWATAKA WAKRISTO NCHINI KUONGEZA KASI YA SALA



Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa

=====================================
Na Gustav Chahe, Iringa              
RAIS wa Baraza la Maakofu Tanzania (TEC) Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa amewataka waamini wakristo kutokuwa na moyo wa kuhamaki kutokana na kitendo kilipuliwa Kanisa Katoliki huko Arusha.
Amezungumza hayo katika mahojiano maalum mtandao  huu wa www.sumiampanda.blogspot.com mahojiano  yaliyofanyika ofisini kwake Iringa juu ya vitendo vinanyoendelea kutokea nchini vikiwemo vya kuchomwa makanisa na kuuawa wachungaji wa kiroho huku vikihusishwa na imani za kidini.
Amesema kama ilivyoutamaduni wa Kikristo, yanapotukia matukio ya kusikitisha kama hayo silaha iliyo kubwa ni sala kumuomba Mungu atoe jibu kwa wanaohusika na mateso kama hayo.
“Kasi ya sala iendelee, ili Mungu wetu wa Amani ajenge fikira za upendo na haki katika mioyo yetu” alisema.
Amesema waamini wasikate tamaa na kuacha kusali kwa kuwa Mungu ndiye mwenye jibu na atatoa majibu kadiri atakavyo kwa wale wote wanaowatesa wenzao kwa sababu zao binafsi.
Hata hivyo alisema licha ya kuwa kila mtu amepokea kwa mshituko na maumivu makubwa, roho za watu zinazoteswa na wengine Mungu atazifariji na kuziponya lakini mtesaji atapata majibu yake.
Alisema waliopoteza maisha katika mlipuko huo Mungu atawarehemu na kuwafariji majeruhi wote.
“Waliopoteza maisha wapokee Rehema ya Mungu na waliojeruhiwa wafarijiwe na uwezo wa Mungu” alisema.
Hali kadhalika amesema upendo na haki ni zawadi kutoka kwa Mungu na hivyo, anayedhurumu wengine zawadi hiyo atapata pigo kubwa.
Aidha amesema wakati uliopo sasa ni wakutafakari na kumkabidhi Mungu yale yote yanayowasumbua wanadamu na kuongeza nguvu ya sala ili majibu ya Mungu yapatikane kwao.
“Tulieni na kufanya tafakari kasha mwambie Mungu hayo yote ayafanyie kazi kwa uweza wake. Sisi binadamu tunategemea nguvu kutoka kwake” alisema.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya tukio la leo, Jumapili, Mei 5, 2013 la mlipuko kwenye Kanisa Katoliki la Mt. Joseph Mfanyakazi la Olasiti Jijini Arusha. 
 Tukio hilo la kigaidi limesababisha mtu mmoja kupoteza maisha na wengine 40 kujeruhiwa.  Rais Kikwete analaani vikali shambulio hilo lililofanywa na mtu au watu katili, waovu na wenye dhamira mbaya na nia mbaya kwa Tanzania na watu wake. 


Rais Kikwete ameagiza vyombo vya usalama nchini kumsaka mtu au watu waliohusika na kitendo hicho kiovu na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.   
Vile vile Rais Kikwete amewataka wananchi wote kuwa watulivu wakati Serikali na vyombo vyake inaendelea kufuatilia tukio hili.  Tutawasaka popote walipo na kupambana nao bila huruma.  
 Aidha, tutakabiliana na aina yoyote ya uhalifu nchini iwe ni ugaidi au aina yoyote ya uhalifu wa namna hiyo au wa namna nyingine, uwe na chimbuko lake ndani ya nchi ama nje ya nchi yetu.
  Kamwe hatutakubali kuwaacha wavuruge amani na usalama wa Tanzania na watu wake. Rais anaamini kuwa Serikali, kwa msaada na ushirikiano wa wananchi, watu hao watapatikana na kuadabishwa ipasavyo.


Aidha, Rais Kikwete anatoa rambirambi za dhati ya moyo wake kwa wafiwa na wale wote ambao wamejeruhiwa katika tukio hilo.
 Anaungana nao katika machungu na msiba. Rais pia anawaombea wote walioumia katika tukio hili wapate nafuu ya haraka na waendelee na shughuli zao za ujenzi wa taifa.


Rais Kikwete vilevile anatoa pole nyingi kwa viongozi na waumini wa Kanisa Katoliki kwa tukio hili la kusikitisha na kuvurugika kwa ibada na shughuli yao muhimu ya uzinduzi wa Kanisa lao.


Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

IKULU,

DAR ES SALAAM

 5 Mei, 2013

KANISA KULIPULIWA ARUSHA ,ASKOFU DKT MDEGELLA ATAKA MAKANISA KULINDWA



Kufuatia shambulio la  kulipuliwa  kwa kanisa katoliki la Olasit nje kidogo ya mji wa Arusha na kupelekea  watu zaidi ya 30  kujeruhiwa na mmoja  kusadikika kupoteza maisha yake ,askofu wa kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania (K.K.K.T) Dayosisi ya Iringa Dkt Owdenburg Mdegella amesema  kuwa  wanafanya  hivyo ni watu  ama mtu anayetaka  kuvuruga amani ya Tanzania na kutaka  nyumba zote za ibada  kuwa na ulinzi .

Askofu Dkt Mdegella ametoa kauli  hiyo leo  wakati akizungumza katika mahojiaono maalum na mtandao huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com kuhusiana na tukio la kulipuliwa kwa kanisa mkoani Arusha.

Kwani  alisema  alishapata   kukutana na vyombo  vya habari  kufuatia tukio la kuchomwa kwa kanisa Zanzibar na  tukio la  kuuwawa kwa  Paroko  kwa  risasi  huko  huko  Zanzibar ila ushauri  wake  alioutoa kwa  serikali  kuwa  hivi  sasa  nchi  inakundi la watu  wanaoendesha ugaidi ,na  kutaka  vyombo  vya  usalama  kusaidia  kupambana na kundi  hilo.

Kwani  amesema  kuwa hivi  sasa  amani ya Taifa  inazidi  kuwa hatarini zaidi  kutokana na watu hao  wanaoendesha  vitendo vya  kigaidi  kuingia kwa kasi kubwa  kushambulia makanisa na kuwa  ni vema  vyombo  vya ulinzi na usalama  kusaidia  kulinda  nyumba  za ibada ili  kunusuru njama  hizo  za  kigaidi.

Mbali ya  kuvitaka  vyombo  vya usalama  kusaidia  kulinda makanisa  bado alishauri  waumini wa  makanisa  hapa nchi kuwa makini  zaidi na ikiwezekana  kuongeza  ulinzi zaidi katika makanisa  yao hasa  siku za ibada  .

Askofu  Dkt  Mdegella alisema  kuwa  yawezekana  ni kundi la  watu  wanaotumia ugaidi kuhatarisha amani ya  Tanzania  ila  pia yawezekana mambo  haya ya machafuko  yanafanywa na  kundi furani la kisiasa  kwa lengo la  kuichafua  serikali ya  CCM iliyopo madarakani kama njia ya kuchinganisha umma kuona kama Rais Jakaya  Kikwete na chama  chake nchi imemshindwa jambo ambalo halipaswi kuungwa mkono na mtanzania yeyeto kwa  watu kuchafua amani ili  wapate  kuingia Ikulu.

Bila  kutaja  jina la chama  cha  siasa kinachofanya  hivyo wala  mtu anayefadhili vitendo  hivyo vya kigaidi askofu Dkt Mdegella aliwataka  wana  siasa na  wananchi  kuwa  kitu  kimoja katika kulinda amani ya Taifa hili.

 Pia  aliulaumu  uongozi  wa kanisa  Katoliki Arusha  kwa  kushindwa  kuimarisha  ulinzi kwa  siku ya leo ambapo  walitambua  wazi  wana tukio  kubwa na tayari  kumekuwepo na vitisho  mbali mbali na  kuwa  iwapo  ulinzi  ungewekwa  eneo hilo yaliyotokea  huenda  yasingetokea.

KANISA LALIPULIWA ARUSHA ,MMOJA AKAMATWA KUHUSISHWA NA TUKIO HILO

Mungu uwe upande wetu
Majeruhi wa Mlipuko huo akipata huduma ya kwanza mapama baada ya tukio hilo
eneo lenye utepe ndipo kinachohisiwa kuwa bomu ndipo kilipotua na kulipuka katika Kanisa la Mt Joseph Olasiti Arusha ambapo Balozi wa Papa alikuwa akihudhuria ibada ya Kuzindua Parokia kanisani hapo....eneo lenye utepe ndipo kinachohisiwa kuwa bomu ndipo kilipotua na kulipuka katika Kanisa la Mt Joseph Olasiti Arusha ambapo Balozi wa Papa alikuwa akihudhuria ibada ya Kuzindua Parokia kanisani hapo....

 Hii ni njia ya kuelekea olasiti kanisani ambapo mlipuko mkubwa umetokea leo asubuhi wakati wa misa ya ufunguzi wa kigango ambapo mgeni rasmi alikuwa ni balozi wa papa nnchini tanzania
Umati wa  wananchi wa mkoa wa Arusha wakiwa njiani kuelekea kuangalia ndugu na jamaa zao waliokuwamo kwenye ibada hiyo inasadikika majeruhi zaidi ya thelathini na watano wapo hospitali huku kukiwa hakuna taarifa ya vifo.
 Kanisa lililolipuliwa likiwa linaonekana kwa mbali huku wananch wakilitazama kwa mbali kutokana na tishio la kutokea kwa milipuko mingine ...Mtu mmoja  amekamatwa kuhusiana na tukio hilio wakati wengine wanasadikika kukimbia.
 Waumini  pamoja na baadhi ya wanacchi wakiwa katika hali ya taharuki  wasiamini nini kilichotokea  kutokana na mlipuko mkubwa  uliotokea asubuhi ya leo.



 Polisi wakijaribu kuchunguza eneo bomu lilipolipukia  leo asubuhi wakati wa misa ya kuzindua kigango hicho.iliyo katika kata ya olasiti na parokia ya burka.
Polisi waki imarisha doria eneo la tukio   baada ya majeruhi kukimbizwa hospitali kupatiwa matibabu zaidi ...Mpaka tunaondoka eneo la tukio Viongozi mbali mbali akiwemo mmbunge wa arusha walikuwemo eneo hilo.


Majeruhi wa tukio hilo wakiwa katika hali mbaya..






DSCN2215


KANISA Katoliki Parokia Teule ya Mt. Joseph Mfanyakazi Olasiti la jijini Arusha limelipuliwa na mlipuko unaodhaniwa kuwa ni bomu la kurushwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ACP, Liberatus Sabas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea majira ya saa tano asubuhi wakati watu wakiwa katika Ibada ya Ufunguzi wa Parokia hiyo teule ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi. 

Hadi sasa mtu mmoja anashikiliwa na polisi kutokana na tukio hilo ambapo inasemekana alirusha mlipuko huo akitokea nyuma ya umati wa waumini.

Kamanda Sabas alisema watu wapatao 30 wamejeruhiwa majeraha madogomadogo na wengine 3 wamejeruhiwa majeraha makubwa na ambapo mpaka sasa wanatibiwa katika hospitali za Mount Meru, Seriani na hospitali nyingine.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa amesema kuwa Vikosi vyote vya Ulinzi na Usalama vinafanya kazi ili kugundua mlipuko huo ni wa aina gani na kuwataka watanzania wote kuwa watulivu na wenye usikivu ili kuifanya kazi hiyo kufanyika kwa ufasaha. 

Pia amewataka wakristo wote kuondoa hali ya wasiwasi na mashwari kwani vikosi hivyo vitatoa majibu ya uhakika.

Ibada hiyo iliyokuwa ya Uzinduzi wa Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi ilikuwa ikiongozwa na Mhashamu askofu Josephat Leburu na Balozi wa Papa Fransisco Montesilo.